08-Wewe Pekee Tunakuabudu: Sababu Za Kutakabaliwa Du’aa

 

إِيَّاكَ نَعْبُدُ وَإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ

Wewe Pekee Tunakuabudu Na Wewe Pekee Tunakuomba Msaada

 

08- Sababu Za Kutakabaliwa Du’aa

 

 

 

 

1- Kumwabudu Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Pekee, Na Kumwomba Kwa Ikhlaasw

 

Sababu kuu ya mja kutakabaliwa du’aa ni kuwa na ikhlaasw na Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) kwa kumtegemea Yeye Pekee, na kuamini kwamba hakuna mwengine atakayepokea du’aa. Kila inapozidi ikhlaasw ndipo huongezeka matumaini ya kutakabaliwa du’aa. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

هُوَ الْحَيُّ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ فَادْعُوهُ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ ۗ الْحَمْدُ لِلَّـهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ﴿٦٥﴾

Yeye Ndiye Aliye hai daima hakuna Muabudiwa wa haki ila Yeye; basi muombeni Yeye wenye kumtakasia Dini. AlhamduliLLaah, Himidi Anastahiki Allaah Rabb wa walimwengu. [Ghaafir: 65]

 

 

 

2- Kuanza Kwa Thanaa Mwanzo Na Mwisho wa Du’aa Na Kumswalia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)

 

Thanaa maana yake ni: kumtukuza, kumsifu na kumshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa).

 

Kufanya hivyo  ni sababu mojawapo ya sababu kuu ya kukubaliwa du’aa kwa sababu bila ya kufanya hivyo du’aa huwa haifiki mbinguni kwa dalili:

 

عَنْ عُمَرَ بْنِ الْخَطَّابِ (رضي الله عنه)  قَالَ: "إِنَّ الدُّعَاءَ مَوْقُوفٌ بَيْنَ السَّمَاءِ وَالأَرْضِ لاَ يَصْعَدُ مِنْهُ شَيْءٌ حَتَّى تُصَلِّيَ عَلَى نَبِيِّكَ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)"

Imepokelewa kutoka kwa ‘Umar bin Khattwaab (Radhwiya Allaahu ‘anhu):  “Hakika du’aa inasimama baina ya mbingu na ardhi haipandi masafa yoyote mpaka umswalie Nabiy wako (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)." [Swahiyh At-Tirmidhiy (486), Swahiyh At-Targhiyb (1676)]

 

 

 

3- Kutumia Wasiylah

 

Kujikurubisha kwanza kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) kabla ya kuanza kuomba haja, kwa tawassul zilizothibiti katika Shariy’ah. na si zile za shirki. (Mlango wake utafuatia)

 

 

 

4- Kuwa Na Matumaini, Unyenyekevu Na Kuuhudhurisha Moyo Kwa Allaah (‘Azza wa Jalla)

 

‘Ibaadah zote zinahitaji unyenyekevu wa mwili, akili na moyo ndipo ‘ibaadah hiyo inapokuwa imemridhisha Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa).

  

Vipi mtu amkabili Rabb kwa haja kisha mawazo na akili yake iwe kwingine? Unapomuomba binaadamu mwenzio unamkabili kwa adabu na heshima na upole, na akili yote imo katika kutegemea akupe unachokihitaji kwake, seuze unapomkabili Mwenye uwezo pekee wa kukidhi haja zako?  

 

Hivyo basi usiwe mwenye kughafilika katika kuomba du’aa kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) na dalili ni: 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((ادْعُوا اللَّهَ وَأَنْتُمْ مُوقِنُونَ بِالإِجَابَةِ وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّهَ لاَ يَسْتَجِيبُ دُعَاءً مِنْ قَلْبٍ غَافِلٍ لاَهٍ))

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Muombeni Allaah huku mkiwa mna yakini kujibiwa, na jueni kwamba Allaah Hatakabali du’aa inayotoka katika moyo ulioghafilika au usiojali)) [Swahiyh At-Tirmidhiy (3479), Swahiyh Al-Jaami’ *245), Swahiyh At-Targhiyb (1653)]

 

Na Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

ادْعُوا رَبَّكُمْ تَضَرُّعًا وَخُفْيَةً ۚ إِنَّهُ لَا يُحِبُّ الْمُعْتَدِينَ ﴿٥٥﴾

Muombeni Rabb wenu kwa unyenyekevu na kwa siri, hakika Yeye Hapendi wenye kupindukia mipaka. [Al-A’raaf: 55]

 

 

 

5- Kuwa Na Dhana Nzuri Na Yakini Na Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa)

 

Inapasa kuwa na dhana nzuri kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) ipate du’aa kutakabaliwa kama Anavyoahidi katika Hadiyth Al-Qudsiy:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه)  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم): ((إِنَّ اللَّهَ يَقُولُ أَنَا عِنْدَ ظَنِّ عَبْدِي بِي وَأَنَا مَعَهُ إِذَا دَعَانِي))

Imepokelewa kutoka  kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema:  Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakika Allaah Anasema: Mimi Nipo pamoja na mja anaponidhania [dhana nzuri], Nami Nipo naye anaponiomba)) [Muslim]

 

Faida ziada za kuwa na dhana nzuri kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) kwamba mja anapotaka kufanya jambo basi Allaah (Subahanau wa Ta’aalaa) Humfanyia  wepesi kufikia atakacho kwa dalili:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ قَالَ قَالَ النَّبِيُّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ (( يَقُولُ اللَّهُ تَعَالَى: أَنَا عِنْدَ ظَنِّ عَبْدِي بِي وَأَنَا مَعَهُ إِذَا ذَكَرَنِي، فَإِنْ ذَكَرَنِي فِي نَفْسِهِ ذَكَرْتُهُ فِي نَفْسِي ، وَإِنْ ذَكَرَنِي فِي مَلَإٍ ذَكَرْتُهُ فِي مَلَإٍ خَيْرٍ مِنْهُمْ ، وَإِنْ تَقَرَّبَ إِلَيَّ بِشِبْرٍ تَقَرَّبْتُ إِلَيْهِ ذِرَاعًا، وَإِنْ تَقَرَّبَ إِلَيَّ ذِرَاعًا تَقَرَّبْتُ إِلَيْهِ بَاعًا، وَإِنْ أَتَانِي يَمْشِي أَتَيْتُهُ هَرْوَلَةً)) البخاري، مسلم، الترمذي وابن ماجه

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema: Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema, ((Allaah Ta’aalaa, Anasema: Mimi ni vile mja Wangu anavyonidhania. Niko pamoja naye Anaponikumbuka katika nafsi yake, Ninamkumbuka katika nafsi Yangu, anaponikumbuka katika hadhara, Ninamkumbuka katika hadhara bora zaidi. Na anaponikaribia shibiri Ninamkaribia dhiraa; anaponikaribia dhiraa, Ninamkaribia pima, anaponijia kwa mwendo (wa kawaida) ninamjia mbio)) [Al-Bukhaariy, Muslim, At-Tirmidhiy na Ibn Maajah]

 

Litakaloweza kumsaidia mja kuwa na dhanna nzuri na kuwa na yakini kwa Rabb wake ni kuzingatia Utukufu Wake, Ufalme Wake wa mbingu na ardhi, Ahadi Zake, Majina Yake Mazuri na Sifa Zake na zaidi katika du’aa kuzingatia Ukarimu na Fadhila Zake. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):     

 

لِيَجْزِيَهُمُ اللَّـهُ أَحْسَنَ مَا عَمِلُوا وَيَزِيدَهُم مِّن فَضْلِهِ ۗ وَاللَّـهُ يَرْزُقُ مَن يَشَاءُ بِغَيْرِ حِسَابٍ ﴿٣٨﴾

Ili Allaah Awalipe mazuri zaidi kutokana na yale waliyoyatenda, na Awazidishie katika fadhila Zake. Na Allaah Humruzuku Amtakaye bila ya hesabu. [An-Nuwr: 38]

 

 

Kama vile Maswahaba watatu ambao Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliwagomea kwa muda mrefu, wakawa katika dhiki kubwa lakini walimwekea dhana nzuri Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) wakatambua kuwa hakuna kimbilio ila kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Pekee ilivyothibiti katika Qur-aan Aliposema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

لَّقَد تَّابَ اللَّـهُ عَلَى النَّبِيِّ وَالْمُهَاجِرِينَ وَالْأَنصَارِ الَّذِينَ اتَّبَعُوهُ فِي سَاعَةِ الْعُسْرَةِ مِن بَعْدِ مَا كَادَ يَزِيغُ قُلُوبُ فَرِيقٍ مِّنْهُمْ ثُمَّ تَابَ عَلَيْهِمْ ۚ إِنَّهُ بِهِمْ رَءُوفٌ رَّحِيمٌ﴿١١٧﴾

Kwa yakini Allaah Amepokea tawbah ya Nabiy na Muhajirina na Answaar ambao wamemfuata (Nabiy صلى الله عليه وآله وسلم) katika saa ya dhiki baada ya nyoyo za kundi miongoni mwao zilikaribia   kuelemea mbali na haki Akapokea tawbah yao. Hakika Yeye kwao ni Mwenye huruma mno, Mwenye kurehemu.

 

 

وَعَلَى الثَّلَاثَةِ الَّذِينَ خُلِّفُوا حَتَّىٰ إِذَا ضَاقَتْ عَلَيْهِمُ الْأَرْضُ بِمَا رَحُبَتْ وَضَاقَتْ عَلَيْهِمْ أَنفُسُهُمْ وَظَنُّوا أَن لَّا مَلْجَأَ مِنَ اللَّـهِ إِلَّا إِلَيْهِ ثُمَّ تَابَ عَلَيْهِمْ لِيَتُوبُوا ۚ إِنَّ اللَّـهَ هُوَ التَّوَّابُ الرَّحِيمُ﴿١١٨﴾

Na (Akapokea tawbah) ya wale watatu waliobaki nyuma (wakajuta mno) mpaka ardhi ikadhikika kwao juu ya kuwa ni pana na zikadhikika nafsi zao, na wakatambua kwamba hakuna pa kumkimbia Allaah isipokuwa kuelekea Kwake; kisha (Allaah) Akapokea tawbah yao, ili watubie. Hakika Allaah Yeye Ndiye Mwingi wa kupokea tawbah, Mwenye kurehemu. [At-Tawbah: 117-118]

 

Amesema Abul-‘Abbaas Al-Qurtwubi katika ‘Al-Mafham’: “Ina maana kuwa na dhana katika kutakabaliwa du’aa na dhana ya kutakabaliwa tawbah, na dhana ya maghfirah katika istighfaar, na dhana ya kutabaliwa 'amali wakati wa kuzitenda kwa sharti ya kuambatanisha kusadiki ahadi Zake na wingi wa fadhila Zake”.

 

 

 

6- Kuomba Du’aa Kila Mara Katika Hali Ya Raha Na Shida   

 

Hadiyth ya Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy, Abuu Hurayrah na Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhum)

 

تعرَّفْ إلى اللهِ في الرَّخاءِ يعرفُك في الشدَّةِ

((Mtambue [mkumbuke] Allaah wakati wa raha Akukumbuke katika shida))  [Swahiyh Al-Jaami’(2961)]

 

Hivyo ndivyo ipasavyo, kumkumbuka Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) katika kila hali. Amewataja wafanyao kinyume chake; Anasema:

 

وَإِذَا أَنْعَمْنَا عَلَى الْإِنسَانِ أَعْرَضَ وَنَأَىٰ بِجَانِبِهِ وَإِذَا مَسَّهُ الشَّرُّ فَذُو دُعَاءٍ عَرِيضٍ﴿٥١﴾

Na Tunapomneemesha insani hukengeuka na kujitenga upande. Na inapomgusa shari, basi mara huwa mwenye du’aa refu refu. [Fusw-swilat: 51]

 

Na Anasema pia Allaah ('Azza wa Jalla):

وَإِذَا مَسَّ الْإِنسَانَ الضُّرُّ دَعَانَا لِجَنبِهِ أَوْ قَاعِدًا أَوْ قَائِمًا فَلَمَّا كَشَفْنَا عَنْهُ ضُرَّهُ مَرَّ كَأَن لَّمْ يَدْعُنَا إِلَىٰ ضُرٍّ مَّسَّهُ ۚكَذَٰلِكَ زُيِّنَ لِلْمُسْرِفِينَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ﴿١٢﴾

Na inapomgusa insani dhara hutuomba anapolala ubavu, au anapokaa au kusimama. Tunapomuondolea dhara, hupita kama kwamba hakutuomba dhara iliyomgusa. Hivyo ndivyo walivyopambiwa wapindukao mipaka yale waliyokuwa wakiyatenda. [Yuwnus: 12]

 

Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

وَإِذَا مَسَّ الْإِنسَانَ ضُرٌّ دَعَا رَبَّهُ مُنِيبًا إِلَيْهِ ثُمَّ إِذَا خَوَّلَهُ نِعْمَةً مِّنْهُ نَسِيَ مَا كَانَ يَدْعُو إِلَيْهِ مِن قَبْلُ

Na inapomgusa insani dhara, humwomba Rabb wake akirudiarudia kutubia Kwake, kisha Akimruzuku neema kutoka Kwake, husahau yale aliyokuwa akimwomba kabla, [Az-Zumar: 8]

 

 

 

7- Kuwa Na Iymaan na Taqwa

 

Kuwa na taqwa kwa maana; kumkumbuka Allaah na kumkhofu Allaah katika kila jambo atendalo binaadamu; ikiwa ni jambo ovu, basi kujiepusha nalo na ikiwa ni la khayr akimbilie kulitenda, Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

قَالَ إِنَّمَا يَتَقَبَّلُ اللَّـهُ مِنَ الْمُتَّقِينَ ﴿٢٧﴾

Akasema: “Hakika Allaah Anatakabalia wenye taqwa.” [Al-Maaidah: 27]

 

Na Anasema Subhaanahu wa Ta’aalaa:

وَلَوْ أَنَّ أَهْلَ الْقُرَىٰ آمَنُوا وَاتَّقَوْا لَفَتَحْنَا عَلَيْهِم بَرَكَاتٍ مِّنَ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ

Na lau kama watu wa miji wangeliamimi na wakawa na taqwa, bila ya shaka Tungeliwafungulia baraka kutoka mbinguni na ardhini, [Al-A’raaf: 96]

 

 

 

8- Kutenda ‘Amali Nyingi Za Khayr

 

Nabiy Zakariyyaa (‘Alayhis-Salaam) alitakabaliwa du’aa yake kuomba mtoto akiwa na umri mkubwa kwa kuwa sababu mojawapo ilikuwa ni kuharakiza kutenda amali za khayr. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

وَزَكَرِيَّا إِذْ نَادَىٰ رَبَّهُ رَبِّ لَا تَذَرْنِي فَرْدًا وَأَنتَ خَيْرُ الْوَارِثِينَ ﴿٨٩﴾

Na Zakariyyaa alipomwita Rabb wake: “Rabb wangu! Usiniache pekee; Nawe Ndiye Mbora wa wenye kurithi.”

 

 

فَاسْتَجَبْنَا لَهُ وَوَهَبْنَا لَهُ يَحْيَىٰ وَأَصْلَحْنَا لَهُ زَوْجَهُ ۚ إِنَّهُمْ كَانُوا يُسَارِعُونَ فِي الْخَيْرَاتِ وَيَدْعُونَنَا رَغَبًا وَرَهَبًا ۖ وَكَانُوا لَنَا خَاشِعِينَ ﴿٩٠﴾

Basi Tukamuitikia na Tukamtunukia Yahyaa, na Tukamtengenezea mke wake. Hakika wao walikuwa wakikimbilia katika mambo ya kheri, na wakituomba kwa raghba na khofu, na walikuwa wenye kutunyenyekea. [Al-Anbiyaa: 89-90]

 

 

9- Kuzidisha ‘Amali Za Nawaafil (Sunnah Za Ziada)

 

Kila mja anapozidisha ‘amali za Sunnah baada ya kutimiza fardhi zake, Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Humtakabalia du’aa zake:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((إِنَّ اللَّهَ قَالَ: مَنْ عَادَى لِي وَلِيًّا فَقَدْ آذَنْتُهُ بِالْحَرْبِ ، وَمَا تَقَرَّبَ إِلَيَّ عَبْدِي بِشَيْءٍ أَحَبَّ إِلَيَّ مِمَّا افْتَرَضْتُ عَلَيْهِ،  وَمَا يَزَالُ عَبْدِي يَتَقَرَّبُ إِلَيَّ بِالنَّوَافِلِ حَتَّى أُحِبَّهُ ،  فَإِذَا أَحْبَبْتُهُ كُنْتُ سَمْعَهُ الَّذِي يَسْمَعُ بِهِ، وَبَصَرَهُ الَّذِي يُبْصِرُ بِهِ، وَيَدَهُ الَّتِي يَبْطِشُ بِهَا، وَرِجْلَهُ الَّتِي يَمْشِي بِهَا، وَإِنْ سَأَلَنِي لأُعْطِيَنَّهُ ، وَلَئِنْ اسْتَعَاذَنِي لأُعِيذَنَّهُ، وَمَا تَرَدَّدْتُ عَنْ شَيْءٍ أَنَا فَاعِلُهُ تَرَدُّدِي عَنْ نَفْسِ الْمُؤْمِنِ يَكْرَهُ الْمَوْتَ وَأَنَا أَكْرَهُ مَسَاءَتَهُ))  

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema:  Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakika Allaah Amesema: Yeyote yule atakayefanya uadui kwa walii Wangu (kipenzi changu) Nitatangaza vita dhidi yake. Mja Wangu hanikaribii na kitu chochote Ninachokipenda kama ‘amali nilizomfaridhishia, na mja Wangu huzidi kunikaribia kwa ‘amali njema za Sunnah ili nimpende. Ninapompenda, huwa masikio yake yanayosikilizia, macho yake anayoonea, mikono yake anayoshikia, miguu yake anayotembelea nayo. Na kama angeniomba kitu bila shaka ningempa. Na kama angeniomba himaya bila shaka ningelimkinga, na Sisiti juu ya kitu chochote kama ninavyosita [kuichukua] roho ya mja Wangu Muumin, anachukia mauti nami Nachukia kumfanyia ubaya)) [Al-Bukhaariy]

 

 

 

10- Kuwaombea Waislamu

 

Muislamu ampendelee nduguye Muislamu khayr kwa kumuombea. Na khasa pale mwenziwe anapokuwa ameneemeshwa kwa neema fulani, basi ni khayr kumuombea Allaah Ambariki. Kufanya hivi ni bora kuliko kumuonea wivu, kwa sababu kumuonea wivu hakutomfaa kitu bali kutazidi kumnyima yeye khayr, kwa sababu kumuombea Muislamu mwenziwe kwa siri, kuna faida ya kuwa Malaika huitikia du’aa na humuombea muombaji apate khayr na barakah kama hizo anazomuombea mwenziwe kama ilivyothibiti katika Hadiyth ifuatayo:

 

عَنْ صَفْوَانَ بْنِ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ صَفْوَانَ (رضي الله عنه)  قَالَ وَكَانَتْ تَحْتَهُ ابْنَةُ أَبِي الدَّرْدَاءِ فَأَتَاهَا فَوَجَدَ أُمَّ الدَّرْدَاءِ وَلَمْ يَجِدْ أَبَا الدَّرْدَاءِ, فَقَالَتْ لَهُ: "تُرِيدُ الْحَجَّ الْعَامَ؟" قَالَ" "نَعَمْ" قَالَتْ: "فَادْعُ اللَّهَ لَنَا بِخَيْرٍ فَإِنَّ النَّبِيَّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) كَانَ يَقُولُ: ((دَعْوَةُ الْمَرْءِ مُسْتَجَابَةٌ لإَخِيهِ بِظَهْرِ الْغَيْبِ عِنْدَ رَأْسِهِ مَلَكٌ يُؤَمِّنُ عَلَى دُعَائِهِ كُلَّمَا دَعَا لَهُ بِخَيْرٍ قَالَ آمِينَ وَلَكَ بِمِثْلِهِ))  

Imepokelewa kutoka kwa Swafwaan bin ‘Abdillaah bin Swafwaan amesema:  alimwendea Abu Dardaa akawa hakumkuta bali alimkuta Ummu Dardaa ambaye alisema: “Je, unataka kuhiji mwaka huu?” Akasema: “Ndio”. Akasema: “Basi tuombee kwa Allaah khayr kwani Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akisema: ((Du’aa ya mtu anayomuombea nduguye kwa siri huweko Malaika juu ya kichwa chake akiitikia du’aa yake kila anapomuombea khayr, husema ‘Aamiyn nawe pia upate sawa nayo’)) [Ibn Maajah (2895), Asw-Swahiyhah (1339), Na riwayaah nyenginezo;  Swahiyh Al-Jaami’ (3381), Swahiyh Ibn Maajah (2358), Swahiyh Abiy Daawuwd (1534)]

 

 

 

11- Kuomba Maghfirah Kwa Wingi

 

Kuomba maghfirah kwa wingi kunampatia Muislamu faida kadhaa kwa dalili zifuatazo:

 

وَأَنِ اسْتَغْفِرُوا رَبَّكُمْ ثُمَّ تُوبُوا إِلَيْهِ يُمَتِّعْكُم مَّتَاعًا حَسَنًا إِلَىٰ أَجَلٍ مُّسَمًّى وَيُؤْتِ كُلَّ ذِي فَضْلٍ فَضْلَهُ ۖ 

Na kwamba: “Mwombeni Rabb wenu maghfirah kisha tubuni Kwake, Atakustarehesheni starehe nzuri mpaka muda maalumu uliokadiriwa; na Atampa kila mwenye fadhila, fadhila Zake.  [Huwd: 3]

 

 وَيَا قَوْمِ اسْتَغْفِرُوا رَبَّكُمْ ثُمَّ تُوبُوا إِلَيْهِ يُرْسِلِ السَّمَاءَ عَلَيْكُم مِّدْرَارًا وَيَزِدْكُمْ قُوَّةً إِلَىٰ قُوَّتِكُمْ

 “Na enyi kaumu yangu!  Mwombeni maghfirah Rabb wenu, kisha tubieni Kwake, Atakuleteeni mbingu zenye kunyesha mvua tele ya kumiminika na Atakuzidishieni nguvu juu ya nguvu zenu [Huwd: 52]

 

فَاسْتَغْفِرُوهُ ثُمَّ تُوبُوا إِلَيْهِ ۚ إِنَّ رَبِّي قَرِيبٌ مُّجِيبٌ﴿٦١﴾

 basi mwombeni maghfirah, kisha tubieni Kwake. Hakika Rabb wangu ni Yuko Karibu kwa ujuzi Wake, Mwenye kuitikia.” [Huwd: 61]

 

 

 Imaam Al-Qurtwuby katika Tafsiyr yake ya Suwrat Nuwh amesimulia:

 

“Katika Aayah hizi (za Suwrat Nuwh) na ambazo ziko katika (Huwd) ni dalili kwamba Istighfaar inateremsha kwayo rizki na mvua.

 

Ash-Sha‘biyy (Rahimahu Allaah) amesema:

 “Umar alitoka kuomba mvua, akawa hazidishi zaidi ya Istighfaar hadi aliporejea, kisha ikanyesha mvua. Walionyeshewa na mvua wakasema: “Hatukukuona ukiomba mvua!” Akasema: “Nimeomba mvua kwa ufunguo wake sahihi ambao unasababisha kuteremka mvua.” Kisha akasoma:

اسْتَغْفِرُوا رَبَّكُمْ إِنَّهُ كَانَ غَفَّارًا﴿١٠﴾

 “Ombeni maghfirah kwa Rabb wenu; hakika Yeye ni Mwingi mno wa kughufuria.

 

يُرْسِلِ السَّمَاءَ عَلَيْكُم مِّدْرَارًا﴿١١﴾

. “Atakutumieni mvua tele ya kuendelea.”

 

وَيُمْدِدْكُم بِأَمْوَالٍ وَبَنِينَ وَيَجْعَل لَّكُمْ جَنَّاتٍ وَيَجْعَل لَّكُمْ أَنْهَارًا﴿١٢﴾

“Na Atakuongezeeni mali na wana, na Atakupeni mabustani na Atakupeni mito.” [Nuwh: 10-12]

 

Na Al-Awzaa’iy (Rahimahu Allaah) amesema: 

 

 “Walitoka watu kuomba mvua, wakasimama kati yao Bilaal bin Sa’d, akamhimidi Allaah na Akamtukuza, kisha akasema: “Ee Allaah hakika sisi Tumekusikia Unasema:

مَا عَلَى الْمُحْسِنِينَ مِن سَبِيلٍ

Hapana njia ya kuwalaumu wafanyao ihsaan [At-Tawbah: 51]

 “Na tumeshakiri makosa yetu, basi je, unaweza msamaha wako kuwa kwa watu mfano wetu? Ee Allaah! Tughufurie na Turehemu na Tunyweshee mvua”. Akanyanyua mikono yake, wakanyanyua watu mikono yao, wakanyweshewa mvua.”

 

Imaam Qurtwuby akaendelea kutaja kisa cha watu waliyemshitakia Hasan Al-Baswriy (Rahimahu Allaah) kwa shida mbali mbali:

 

 “Mtu mmoja alimjia Hasan Al-Baswriy kumshitakia ukame, Akamwambia: “Omba maghfirah kwa Allaah”.  Siku nyingine akaja wa pili kumshtakia ufakiri, Akamwambia: “Omba maghfirah kwa Allaah”. Akamjia mwengine kumwambia: “Niombee Allaah Aniruzuku mtoto” Akamwambia:  “Omba maghfirah kwa Allaah”. Akaja mwengine kumshtakia ukosefu wa maji shambani mwake. Akamwambia: “Omba maghfirah kwa Allaah” (Wakastajaabu watu kuwa mahitaji kadhaa tofauti lakini utambuzi ni mmoja tu!) Akasema:  “Sikusema lolote kutoka kwangu, bali hakika Allaah Ta’aalaa Anasema:

اسْتَغْفِرُوا رَبَّكُمْ إِنَّهُ كَانَ غَفَّارًا﴿١٠﴾

 “Ombeni maghfirah kwa Rabb wenu; hakika Yeye ni Mwingi mno wa kughufuria.

يُرْسِلِ السَّمَاءَ عَلَيْكُم مِّدْرَارًا﴿١١﴾

 “Atakutumieni mvua tele ya kuendelea.”

وَيُمْدِدْكُم بِأَمْوَالٍ وَبَنِينَ وَيَجْعَل لَّكُمْ جَنَّاتٍ وَيَجْعَل لَّكُمْ أَنْهَارًا﴿١٢﴾

 “Na Atakuongezeeni mali na wana, na Atakupeni mabustani na Atakupeni mito.” [Nuwh: 10-12]

 

 

 

12- Kumshukuru Allaah Kwa Wingi Kuhusu Neema Zake

 

Neema za Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) ni nyingi mno hakuna awezaye kuzihesabu kama Anavyosema:

 

وَآتَاكُم مِّن كُلِّ مَا سَأَلْتُمُوهُ ۚ وَإِن تَعُدُّوا نِعْمَتَ اللَّـهِ لَا تُحْصُوهَا ۗ إِنَّ الْإِنسَانَ لَظَلُومٌ كَفَّارٌ ﴿٣٤﴾

Na Akakupeni kila mnachomuomba. Na mkihesabu neema za Allaah hamtoweza kuziorodhesha hesabuni.  Hakika insani ni mwingi wa dhulma, mwingi wa kukufuru akosaye shukurani. [Ibraahiym: 3]

 

 

Na Amesema pia Allaah ('Azza wa Jalla):

وَإِن تَعُدُّوا نِعْمَةَ اللَّـهِ لَا تُحْصُوهَا ۗ 

Na mkihesabu neema za Allaah hamtoweza kuziorodhesha hesabuni. [An-Nahl: 18]

 

 

Neema hizo ni aina mbili kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta''aalaa):

 

أَلَمْ تَرَوْا أَنَّ اللَّـهَ سَخَّرَ لَكُم مَّا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ وَأَسْبَغَ عَلَيْكُمْ نِعَمَهُ ظَاهِرَةً وَبَاطِنَةً ۗ 

Je, hamuoni kwamba Allaah Amekuitishieni vile vilivyomo mbinguni na vile vilivyomo ardhini, na Akakutimizieni kitimilifu neema Zake kwa dhahiri na siri?  [Luqmaan: 20]

 

 

Neema za dhahiri; kila kinachowezekana kuonekana katika Alivyoumba Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) mfano; ardhi, bahari, jua, mwezi, nyota, maji, mwili, siha, mali, watoto, wanyama, miti, na neema nyingi nyinginezo zisizo hesabika).

 

Neema za siri; ni kila kilichofichika (mfano; iymaan, taqwa, ikhlaasw, akili, Malaika, Jannah na mazuri yaliyoko Aakhirah na neema nyingi mno nyenginezo tusizozijua au kuziona ambazo hazihesabiki).

 

Kwa hiyo imewajibika kwetu kumshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) kwa wingi japokuwa shukurani zetu haziwezi kulingana uwingi wa neema Zake. Juu ya hivyo, Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):  

وَإِذْ تَأَذَّنَ رَبُّكُمْ لَئِن شَكَرْتُمْ لَأَزِيدَنَّكُمْ ۖ 

Na pindi Alipotangaza Rabb wenu: “Ikiwa mtashukuru, bila shaka Nitakuzidishieni (neema Zangu); [Ibraahiym: 7]

 

 

 

Share