19-Wewe Pekee Tunakuabudu: Tawassul Zinazokubalika: Kutawassal Kwa ‘Iymaan na Tawhiyd na ‘Amali Za Kimatendo

 

إِيَّاكَ نَعْبُدُ وَإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ

Wewe Pekee Tunakuabudu Na Wewe Pekee Tunakuomba Msaada

 

Tawassul Zinazokubalika

 

19-Kutawassal Kwa ‘Iymaan na Tawhiyd na ‘Amali Za Kimatendo

 

 

 

 

Inafaa pia kutawassal kwa ‘amali za kimoyoni kama kumwamini Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na kumpwekesha (Tawhiyd) mfano kusema: “Ee Allaah!  Hakika mimi natawassal Kwako kwa iymaan yangu kwamba Wewe ni Mwabudiwa wa haki, Huna mshirika, nifarijie jambo langu kadhaa, au nijaalie kadhaa au nighufurie dhambi zangu.”

 

Au mfano kusema:

 

“Ee Allaah!  Hakika mimi natawassal Kwako kwa mapenzi yangu Kwako pamoja na kumpenda Nabiy Wako (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kuamini yote aliyokuja nayo na kuwapenda Maswahaba wote, nijaalie kadhaa wa kadhaa.” Dalili ni kauli za Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) zifuatazo:

 

الَّذِينَ يَقُولُونَ رَبَّنَا إِنَّنَا آمَنَّا فَاغْفِرْ لَنَا ذُنُوبَنَا وَقِنَا عَذَابَ النَّارِ ﴿١٦﴾ 

Wale wasemao: “Rabb wetu, hakika sisi tumeamini, basi Tughufurie madhambi yetu na Tukinge na adhabu ya moto.” [Aal-‘Imraan: 16]

 

Na kama walivyoomba Al-Hawaariyyuwn (wafuasi watiifu) wa Nabiy ‘Iysa ('Alayhis-Salaam):   

رَبَّنَا آمَنَّا بِمَا أَنزَلْتَ وَاتَّبَعْنَا الرَّسُولَ فَاكْتُبْنَا مَعَ الشَّاهِدِينَ ﴿٥٣﴾

 “Rabb wetu, tumeamini Uliyoyateremsha na tumemfuata Rasuli basi tuandike pamoja na wanaoshuhudia (haki).” [Aal-‘Imraan: 53]

 

 

Au kama alivyotawassal Nabiy Yuwsuf ('Alayhis-salaam) akataja kwanza neema na fadhila za Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) juu yake Alizomneemesha, kisha akamtukuza Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kisha ndio akaomba kufishwa akiwa katika hali ya Uislamu na kukutanishwa na waja wema, aliomba:

 

رَبِّ قَدْ آتَيْتَنِي مِنَ الْمُلْكِ وَعَلَّمْتَنِي مِن تَأْوِيلِ الْأَحَادِيثِ ۚ فَاطِرَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ أَنتَ وَلِيِّي فِي الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ ۖتَوَفَّنِي مُسْلِمًا وَأَلْحِقْنِي بِالصَّالِحِينَ ﴿١٠١﴾

 “Rabb wangu kwa yakini Umenipa katika utawala, na Umenifunza katika tafsiri za masimulizi (ya ndoto na matukio). Muanzilishi wa mbingu na ardhi. Wewe ni Mlinzi, Msaidizi wangu duniani na Aakhirah. Nifishe hali ya kuwa Muislamu na Unikutanishe na Swalihina.” [Yuwsuf: 101]

 

 

Au kama walivyotawassal Maswahaba kwa Tawhiyd ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) katika uumbaji Wake na kumwamini na kuamini Siku ya mwisho na kukhofu moto wa Aakhirah. 

 

الَّذِينَ يَذْكُرُونَ اللَّـهَ قِيَامًا وَقُعُودًا وَعَلَىٰ جُنُوبِهِمْ وَيَتَفَكَّرُونَ فِي خَلْقِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ رَبَّنَا مَا خَلَقْتَ هَـٰذَا بَاطِلًا سُبْحَانَكَ فَقِنَا عَذَابَ النَّارِ ﴿١٩١﴾ 

Ambao wanamdhukuru Allaah kwa kusimama  na kwa kukaa na kwa kulala ubavuni mwao na wanatafakari katika kuumbwa mbingu na ardhi (wakisema): “Rabb wetu, Hukuumba haya bure, Subhaanak! (Utakasifu ni Wako) tukinge na adhabu ya moto.”

 

 

رَبَّنَا إِنَّكَ مَن تُدْخِلِ النَّارَ فَقَدْ أَخْزَيْتَهُ ۖ وَمَا لِلظَّالِمِينَ مِنْ أَنصَارٍ ﴿١٩٢﴾

 “Rabb wetu, hakika Umuingizaye motoni, kwa yakini Umemhizi. Na madhalimu hawana yeyote mwenye kuwanusuru.”

 

رَّبَّنَا إِنَّنَا سَمِعْنَا مُنَادِيًا يُنَادِي لِلْإِيمَانِ أَنْ آمِنُوا بِرَبِّكُمْ فَآمَنَّا ۚ رَبَّنَا فَاغْفِرْ لَنَا ذُنُوبَنَا وَكَفِّرْ عَنَّا سَيِّئَاتِنَا وَتَوَفَّنَا مَعَ الْأَبْرَارِ ﴿١٩٣﴾

 “Rabb wetu, hakika sisi tumemsikia mwitaji anaita kwenye iymaan kwamba ‘mwaminini Rabb wenu’ basi tukaamini.  Rabb wetu, Tughufurie madhambi yetu na Tufutie makosa yetu na Tufishe pamoja na Waumini wema.”

 

 رَبَّنَا وَآتِنَا مَا وَعَدتَّنَا عَلَىٰ رُسُلِكَ وَلَا تُخْزِنَا يَوْمَ الْقِيَامَةِ ۗ إِنَّكَ لَا تُخْلِفُ الْمِيعَادَ ﴿١٩٤﴾

 “Rabb wetu na Tupe Uliyotuahidi kupitia Rusuli Wako, wala Usituhizi Siku ya Qiyaamah; hakika Wewe Huendi kinyume na miadi.” [Aal-‘Imraan: 191-194]

 

Baada ya kauli zao na du’aa zao hizo, Allaah Akawaitikia na kuwaghufuria na kuwaruzuku mazuri zaidi:

 

فَاسْتَجَابَ لَهُمْ رَبُّهُمْ أَنِّي لَا أُضِيعُ عَمَلَ عَامِلٍ مِّنكُم مِّن ذَكَرٍ أَوْ أُنثَىٰ ۖ بَعْضُكُم مِّن بَعْضٍ ۖ فَالَّذِينَ هَاجَرُوا وَأُخْرِجُوا مِن دِيَارِهِمْ وَأُوذُوا فِي سَبِيلِي وَقَاتَلُوا وَقُتِلُوا لَأُكَفِّرَنَّ عَنْهُمْ سَيِّئَاتِهِمْ وَلَأُدْخِلَنَّهُمْ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ ثَوَابًا مِّنْ عِندِ اللَّـهِ ۗ وَاللَّـهُ عِندَهُ حُسْنُ الثَّوَابِ ﴿١٩٥﴾

Basi Rabb wao Akawaitikia  “Hakika Mimi Sipotezi ‘amali za mtendaji yeyote yule miongoni mwenu akiwa mwanamume au mwanamke, nyinyi kwa nyinyi. Basi wale waliohajiri na wakatolewa majumbani mwao na wakaudhiwa katika njia Yangu, wakapigana na wakauliwa; bila shaka Nitawafutia makosa yao na bila shaka Nitawaingiza Jannaat zipitazo chini yake mito, ni thawabu kutoka kwa Allaah.  Na kwa Allaah kuna thawabu nzuri kabisa.” [Aal-‘Imraan: 195]

 

 

Pia inafaa kutawassal kwa ‘amali njema yoyote ile. Mfano kusema:

 

“Ee Allaah hakika mimi natawassal kwako kwa kumsaidia jirani yangu katika hali yake ya shida kadhaa wa kadhaa Basi ee Allaah, nitakabalie haja yangu kadhaa, au niepushe na shari kadhaa.” 

 

Au mfano kusema:

"Ee Allaah, hakika mimi natawassal kwako kwa 'amali yangu ya kumsamehe deni ndugu yangu, au natawassal kwa swadaqah yangu niliyoitoa kwa masikini na wenye kuhitaji, unitakabalie haja yangu zangu kadhaa."

 

Au mfano kusema:

“Ee Allaah, hakika mimi natawassal kwako kwa kuwatendea wema wazazi wangu kuwafanyia kadhaa wa kadhaa unitakabalie haja zangu kadhaa au nijaalie kadhaa” Dalili ni Hadiyth swahiyh ifuatayo iliyotaja kisa cha watu watatu waliokwama pangoni wakakaribia kukata tamaa kuokoka:

 

عن عبدِ الله بنِ عمرَ بن الخطابِ رضيَ اللهُ عنهما، قَالَ: سمعتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم، يقول: ((انطَلَقَ ثَلاثَةُ نَفَرٍ مِمَّنْ كَانَ قَبْلَكُمْ حَتَّى آوَاهُمُ المَبيتُ إِلى غَارٍ فَدَخلُوهُ، فانْحَدرَتْ صَخْرَةٌ مِنَ الجَبَلِ فَسَدَّتْ عَلَيْهِمُ الغَارَ، فَقالُوا: إِنَّهُ لا يُنْجِيكُمْ مِنْ هذِهِ الصَّخْرَةِ إِلا أنْ تَدْعُوا اللهَ بصَالِحِ أعْمَالِكُمْ. 
قَالَ رجلٌ مِنْهُمْ: اللَّهُمَّ كَانَ لِي أَبَوانِ شَيْخَانِ كبيرانِ، وكُنْتُ لا أغْبِقُ قَبْلَهُمَا أهْلًا ولا مالًا، فَنَأَى بِي طَلَب الشَّجَرِ يَوْمًا فلم أَرِحْ عَلَيْهمَا حَتَّى نَامَا، فَحَلَبْتُ لَهُمَا غَبُوقَهُمَا فَوَجَدْتُهُما نَائِمَينِ، فَكَرِهْتُ أنْ أُوقِظَهُمَا وَأَنْ أغْبِقَ قَبْلَهُمَا أهْلًا أو مالًا، فَلَبَثْتُ، والْقَدَحُ عَلَى يَدِي، أنتَظِرُ اسْتِيقَاظَهُما حَتَّى بَرِقَ الفَجْرُ والصِّبْيَةُ يَتَضَاغَوْنَ عِنْدَ قَدَميَّ، فاسْتَيْقَظَا فَشَرِبا غَبُوقَهُما.اللَّهُمَّ إنْ كُنْتُ فَعَلْتُ ذلِكَ ابِتِغَاء وَجْهِكَ فَفَرِّجْ عَنّا مَا نَحْنُ فِيهِ مِنْ هذِهِ الصَّخْرَةِ، فانْفَرَجَتْ شَيْئًا لا يَسْتَطيعُونَ الخُروجَ مِنْهُ. 

قَالَ الآخر: اللَّهُمَّ إنَّهُ كانَتْ لِيَ ابْنَةُ عَمّ، كَانَتْ أَحَبَّ النّاسِ إليَّ،

 وفي رواية:

 كُنْتُ أُحِبُّها كأَشَدِّ مَا يُحِبُّ الرِّجَالُ النساءَ، فأَرَدْتُهَا عَلَى نَفْسِهَا فامْتَنَعَتْ منِّي حَتَّى أَلَمَّتْ بها سَنَةٌ مِنَ السِّنِينَ فَجَاءتْنِي فَأَعْطَيْتُهَا عِشْرِينَ وَمائةَ دينَارٍ عَلَى أنْ تُخَلِّيَ بَيْني وَبَيْنَ نَفْسِهَا فَفعَلَتْ، حَتَّى إِذَا قَدَرْتُ عَلَيْهَا،

 وفي رواية:

فَلَمَّا قَعَدْتُ بَينَ رِجْلَيْهَا، قالتْ: اتَّقِ اللهَ وَلا تَفُضَّ الخَاتَمَ إلا بِحَقِّهِ، فَانصَرَفْتُ عَنْهَا وَهيَ أَحَبُّ النَّاسِ إليَّ وَتَرَكْتُ الذَّهَبَ الَّذِي أعْطَيتُها. اللَّهُمَّ إنْ كُنْتُ فَعَلْتُ ذلِكَ ابْتِغاءَ وَجْهِكَ فافْرُجْ عَنَّا مَا نَحْنُ فيهِ، فانْفَرَجَتِ الصَّخْرَةُ، غَيْرَ أَنَّهُمْ لا يَسْتَطِيعُونَ الخُرُوجَ مِنْهَا. 

وَقَالَ الثَّالِثُ: اللَّهُمَّ اسْتَأْجَرْتُ أُجَرَاءَ وأَعْطَيْتُهُمْ أجْرَهُمْ غيرَ رَجُل واحدٍ تَرَكَ الَّذِي لَهُ وَذَهبَ، فَثمَّرْتُ أجْرَهُ حَتَّى كَثُرَتْ مِنهُ الأمْوَالُ، فَجَاءنِي بَعدَ حِينٍ، فَقالَ: يَا عبدَ اللهِ، أَدِّ إِلَيَّ أجْرِي، فَقُلْتُ: كُلُّ مَا تَرَى مِنْ أجْرِكَ: مِنَ الإبلِ وَالبَقَرِ والْغَنَمِ والرَّقيقِ، فقالَ: يَا عبدَ اللهِ، لا تَسْتَهْزِئْ بي! فَقُلْتُ: لا أسْتَهْزِئ بِكَ، فَأَخَذَهُ كُلَّهُ فاسْتَاقَهُ فَلَمْ يتْرُكْ مِنهُ شَيئًا. الَّلهُمَّ إنْ كُنتُ فَعَلْتُ ذلِكَ ابِتِغَاءَ وَجْهِكَ فافْرُجْ عَنَّا مَا نَحنُ فِيهِ، فانْفَرَجَتِ الصَّخْرَةُ فَخَرَجُوا يَمْشُونَ))  مُتَّفَقٌ عليهِ

Imepokelewa kutoka kwa 'Abdullaah bin ‘Umar bin Al-Khattwaab (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Nilimsikia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Waliondoka watu watatu, miongoni mwa watu waliokuwa kabla yenu waliosafiri hadi wakaingia pangoni ili walale.

 

Likaviringika jiwe kutoka juu ya jabali likawafungia pango. Wakasemezana: Hakuna kitakachowaokoa kutokana na jiwe hili isipokuwa mumuombe Allaah kwa ‘amali zenu njema.

 

Mmoja miongoni mwao akaanza kuomba: “Ee Allaah. Nilikuwa nina wazazi wawili wazee wakongwe, nilikuwa sitangulizi (kabla yao kunywa maziwa) familia wala watumwa. Siku moja haja ya kutafuta kuni ikanipeleka mbali, sikuweza kuwarudia (mapema) mpaka wakalala. Nikawakamulia maziwa yao, nikawakuta wameshalala. Nikachukia kuwaamsha na (nikachukia pia) kuwapa maziwa familia na watumwa kabla yao. Nikawa na (bilauri) imo mikononi mwangu mpaka waamke, hadi alfajiri ikatokeza huku watoto wakipiga kelele kwa njaa miguuni mwangu; wakaamka na wakanywa maziwa yao. Ee Allaah. Ikiwa nilifanya hivyo kwa kutaka radhi Zako, basi tufariji katika dhiki tuliyonayo ya jiwe hili.”

 

Kukafunguka kidogo kidogo kwa namna ambayo hawawezi kutoka.

 

Mwengine akasema: “Ee Allaah. Nilikuwa nina bint wa ‘ammi yangu, nilikuwa nikimpenda mno...”

 

Riwaayah nyingine imesema:

“Nilikuwa nikimpenda kama vile wanaume wanavyopenda mno wanawake. Nikamtaka (kuzini nae), akanikatalia. Mpaka alipokuja mwaka wa ukame, akanijia nikampa dinaar 120 ili niwe naye faragha. Akakubali. Nilipokuwa nimeshamuweza...”

 

Riwaayah nyingine inasema:

“Nilipoketi baina ya miguu yake akanambia: Mche Allaah, usiivunje pete ila kwa haki yake. Nikamuondokea nikiwa nampenda mno (wala sikumfanya chochote), na nikamuachia dhahabu niliyompa. Ee Allaah, Ikiwa nilifanya hivyo kwa ajili ya kupata radhi Zako, basi tufariji katika dhiki tuliyonayo.”

 

Jiwe likafunguka, lakini walikuwa hawawezi kutoka.

 

Mtu wa tatu akasema:

 

“Ee Allaah. Mimi niliwaajiri wafanyakazi, nikawapa ujira wao isipokuwa mtu mmoja, aliuacha ujira wake na akaenda. Nikauzalisha ujira wake mpaka ukawa ni mali nyingi. Baada ya muda akanijia na kuniambia: Ee mja wa Allaah, nipe ujira wangu! Nikamwambia: Kila unachokiona katika ngamia, ng’ombe, mbuzi na watumwa ni ujira wako! Akaniambia: Ee mja wa Allaah, usinifanyie istihzai (usinikebehi)!  Nikamwambia: Sikufanyii istihzai. Akachukua mali yote na akayachunga na wala hakubakisha mali yoyote. Ee Allaah. Ikiwa nilifanya hivyo kwa kutaka radhi Zako, basi tufariji katika dhiki tuliyonayo.”

 

Jiwe likafunguka wakatoka zao.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

 

Share