22-Wewe Pekee Tunakuabudu: Tawassul Zinazokubalika: Kutawassal Kwa Du'aa Ya Mja Mwema Aliye Hai

 

إِيَّاكَ نَعْبُدُ وَإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ

Wewe Pekee TunakuabuduNa Wewe Pekee Tunakuomba Msaada

 

Tawassul Zinazokubalika

 

22-Kutawasali Kwa Du'aa Ya Mja  Mwema Aliye Hai

 

 

 

 

Inafaa Muislamu kumwomba nduguye Muumini aliye hai amkumbuke kwa du’aa. Maswahaba (Radhwiya Allaahu ‘anhum) walikuwa wakimuomba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) awaombee katika   mas-alah mbali mbali. Mfano pale mtu alipomwendea Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) awaombee mvua baada ya kufikwa na ukame mkubwa uliosababisha balaa ya kuharibikiwa mali zao:

 

عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ، أَنَّ رَجُلاً، دَخَلَ الْمَسْجِدَ يَوْمَ جُمُعَةٍ مِنْ بَابٍ كَانَ نَحْوَ دَارِ الْقَضَاءِ، وَرَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَائِمٌ يَخْطُبُ، فَاسْتَقْبَلَ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَائِمًا ثُمَّ قَالَ: "يَا رَسُولَ اللَّهِ هَلَكَتِ الأَمْوَالُ وَانْقَطَعَتِ السُّبُلُ، فَادْعُ اللَّهَ يُغِيثُنَا" فَرَفَعَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَدَيْهِ ثُمَّ قَالَ: ((اللَّهُمَّ أَغِثْنَا، اللَّهُمَّ أَغِثْنَا، اللَّهُمَّ أَغِثْنَا)). قَالَ أَنَسٌ: وَلاَ وَاللَّهِ مَا نَرَى فِي السَّمَاءِ مِنْ سَحَابٍ، وَلاَ قَزَعَةً، وَمَا بَيْنَنَا وَبَيْنَ سَلْعٍ مِنْ بَيْتٍ وَلاَ دَارٍ‏.‏ قَالَ فَطَلَعَتْ مِنْ وَرَائِهِ سَحَابَةٌ مِثْلُالتُّرْسِ، فَلَمَّا تَوَسَّطَتِ السَّمَاءَ انْتَشَرَتْ ثُمَّ أَمْطَرَتْ، فَلاَ وَاللَّهِ مَا رَأَيْنَا الشَّمْسَ سِتًّا، ثُمَّ دَخَلَ رَجُلٌ مِنْ ذَلِكَ الْبَابِ فِي الْجُمُعَةِ وَرَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَائِمٌ يَخْطُبُ، فَاسْتَقْبَلَهُ قَائِمًا فَقَالَ: "يَا رَسُولَ اللَّهِ هَلَكَتِ الأَمْوَالُ وَانْقَطَعَتِ السُّبُلُ، فَادْعُ اللَّهَ يُمْسِكْهَا عَنَّا"‏.‏  قَالَ:  فَرَفَعَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَدَيْهِ ثُمَّ قَالَ: ((اللَّهُمَّ حَوَالَيْنَا وَلاَ عَلَيْنَا، اللَّهُمَّ عَلَى الآكَامِ وَالظِّرَابِ وَبُطُونِ الأَوْدِيَةِ وَمَنَابِتِ الشَّجَرِ)) ‏ قَالَ: فَأَقْلَعَتْ وَخَرَجْنَا نَمْشِي فِي الشَّمْسِ‏.‏ قَالَ شَرِيكٌ: سَأَلْتُ أَنَسَ بْنَ مَالِكٍ أَهُوَ الرَّجُلُ الأَوَّلُ فَقَالَ مَا أَدْرِي‏.‏

Imepokelewa kutoka kwa Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba mtu mmoja aliingia Masjid siku ya Ijumaa kupitia mlango ulioelekea Daar Al-Qadhwaa na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa amesimama akikhutubia. Akasimama mbele ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kisha akasema: “Ee Rasuli wa Allaah! Wanyama wameteketea na njia zimekatika, basi muombe Allaah Atuteremshie mvua.” Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akanyanyua mikono akaomba: ((Allaahumma Aghithnaa, Allaahumma Aghithnaa, Allaahumma Aghithanaa - Ee Allaah tubarikie kwa mvua))”. Anas amesema:  Wa-Allaahi hakukuwa na mawingu mbinguni na hakukuwa na nyumba au jengo baina yetu na baina ya mlima wa Sal’i.  Basi wingu kubwa kama ngao lilitokea nyuma yake.  Lilipofika katikati lilienea kisha ikanyesha mvua. Basi wa-Allaahi, hatukuona jua siku sita. Kisha Ijumaa iliyofuatia aliingia mtu kupitia mlango huo huo na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akikhutubia khutbah ya Ijumaa, akasimama mbele yake akasema: “Ee Rasuli wa Allaah!  Mifugo ya nyama inateketea na njia zimekatika, muombe Allaah Atuzuilie mvua!” Anas akasema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akanyanyua mikono oyake akaomba: ((Allaahumma Hawaalaynaa walaa ‘alaynaa.” - Ee Allaah! Pembezoni mwetu na si juu yetu. Eee Allaah juu ya majabali, na vilimani, na ndani ya mabonde na juu ya sehemu zinazoota miti)) Anas akasema: Mvua ikasita na tukatoka tukitembea katika jua.  Shariyk alimuuliza Anas kama huyo mtu alikuwa ni yule yule wa kwanza? Akajibu kuwa hajui. [Al-Bukhaariy, Kitaab Al-Istisqaa]

 

 

Imaam Ibn ‘Uthaymiyn ameeleza kama hayo, kisha akataja Hadiyth ya ‘Ukaashah kisha akasema: “Basi hii ni tawassuli inayojuzu nayo ni kumuomba mtu unayetaraji kutakabaliwa kwake amuombee kwa Allaah Ta’aalaa, lakini ambalo linalopasa ni kwamba muulizaji anakusudia hayo yamfanye yeye nafsi yake na yamfae pia nduguye ambaye anamuomba amuombeee na si kukusudia kujinufaisha yeye pekee kwa sababu unapotaka kumnufuisha nduguyo na kujinufaisha nafsi yako huwa ni kumfanyia ihsaan. Basi mtu anapomuombea nduguye du’aa kwa siri Malaika husema: “Aamiyn nawe upate mfano wake.” Kwa hiyo naye huwa katika wafanyao ihsaan kwa du’aa hii, na Allaah Anapenda wafanyao ihsaan.” [Fataawaa Imaam Ibn ‘Uthaymiyn, Hukmu At-Tawassul]  

 

 

 

Share