27-Wewe Pekee Tunakuabudu: Tawassul Za Shirki Kufru Bid’ah: Kutawassal Kwa Du'aa Kanzul-'Arsh (Ganjul-Arsh)

 

إِيَّاكَ نَعْبُدُ وَإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ

Wewe Pekee Tunakuabudu Na Wewe Pekee Tunakuomba Msaada

 

Tawassul Za Shirki Kufru Na Bid’ah

 

27-Kutawassal Kwa Du'aa Ya Kanzul-‘Arsh  (Ganjul-‘Arsh)

 

 

 

 

 Kanzul-‘Arsh (Ganjul-‘Arsh) - كنز العرش

 

Du'aa au uradi huo wa “Kanzul-‘Arsh” (Hazina ya ‘Arsh ya Allaah) inajulikana  katika jamii yetu ya Kiswahili kama “Ganjul-‘Arsh” na hivyo kwa sababu  ndivyo inavyotamkwa katika jamii za Bara la Hindi.

 

Ndani yake kuna mkusanyiko wa du’aa na maneno ambayo yaliyokusanywa kwa wale ‘Muridu’ wa ki-Sufi wazisome na kuzirudia katika nyakati maalum na kwa muundo fulani na kwa idadi maalum inayojulikana kwao.

 

Kadhaalika, du'aa hiyo vilevile imo katika vitabu vya Kishia na wanachangia sana kuieneza.

 

 

Shaykhul-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah) amesema:

“Hapana shaka kwamba adkhaar na du’aa ni ‘ibaadah bora kabisa, na ‘ibaadah ni jambo mojawapo ambalo hakuna upenyo wa mtu kuleta rai zake. Inatupasa tufuate aliyotufunza Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na si hawaa na matamanio yetu au uzushi. Du’aa na adhkaar za Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ni bora zaidi kuliko zozote nyinginezo. Na mwenye kuzifuata atabakia salama na kutenda yaliyo sahihi, na manufaa na matokeo mazuri atakayochuma ni mengi hata hayaelezeki.

 

Du’aa na adhkaar zozote nyinginezo zinakuwa ni haramu au makruhu kwani zinaweza kuhusiana na shirk japokuwa watu wengi hawatambui hilo. Maelezo yake ni marefu mno kuyaelezea hapa.

 

Mtu hana haki kufundisha watu du’aa au adhkaar zozote zisizokuwa katika Sunnah, au kuzifanya kuwa ni ‘ibaadah ya mazoea ambayo anategema watu kuifanya kama wafanyavyo Swalaah tano. Huu ni uzushi katika Dini ambao Allaah Hajautolea idhini. Ama kupanga uradi au kusoma kwa kudumisha adhkaar ambazo hazikuamrishwa katika shariy’ah, ni jambo lisiloruhusiwa.

 

Du’aa na adhkaar zilizoamrishwa katika shariy’ah, ni bora zaidi kwa yeyote kuzitaraji na kuzipata na hakuna anayezipuuza kwa kufadhilisha zilizo mpya za uzushi, au adhkaar za uzushi isipokuwa ambaye ni mjinga au mtendaji makosa.” [Majmuw’ Al-Fataawa (22/510/511)]

 

 

Uradi au du’aa hiyo ya Kanzul-‘Arsh imetangulia kutajwa katika kijitabu chake:   

 

الدعاء المكتوب حول عرش الرحمن ، اقرأ هذا الدعاء ولو مرة واحدة في حياتك  وياحبذا لو قرأته في حب الله وليس في حب الثواب، قيل أن جبريل عليه السلام أتى النبي صلى الله علية وسلم فقال: يا محمد، السلام يُقرئك السلام، ويخصك بالتحية والإكرام، وقد أوهبك هذا الدعاء الشريف!  يا محمد، ما من عبد يدعو وتكون خطاياه وذنوبه مثل أمواج البحار، وعدد أوراق الأشجار، وقطر الأمطار، وبوزن السموات والأرض، إلا غفر الله تعالى ذلك كله له -  يا محمد، هذا الدعاء مكتوب حول العرش، ومكتوب على حيطان الجنة وأبوابها، وجميع ما فيها...يا محمد أنزل بالوحي ببركة هذا الدعاء وأصعد به، وبهذا الدعاء تُفتح أبواب الجنة يوم القيامة، وما من ملك مقرب إلا تقرب إلى ربه ببركته!

 

Du’aa imeandikwa kuizunguka ‘Arshi ya Ar-Rahmaan. Soma du’aa hii japo mara moja katika uhai wako. Ee laiti ukaisoma kwa kupata mapenzi ya Allaah na si kwa mapenzi ya thawabu.

Inasemekana kwamba Jibriyl ('Alayhis-Salaam) alimwendea Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: “Ee Muhammad! As-Salaam Anakutolea salaam, na Anakuamkia kwa maamkizi na heshima, na Amekutunukia du’aa hii tukufu.

Ee Muhammad, hakuna mja atakayeiomba hali yakuwa ana makosa yake na dhambi zake zinafikia mawimbi ya bahari, na yanafikia idadi ya majani katika miti yote, na matone ya mvua, na kwa uzito wa mbingu na ardhi isipokuwa Allaah Atamghufuria yote.

Ee Muhammad! Du’aa hii imeandikwa kuizunguka ‘Arshi na katika kuta za Jannah na milango yake, na yote yaliyomo humo.

Ee Muhammad (Allaah) Ameteremsha wahyi kwa baraka ya du’aa hii na Anapandisha kwa baraka ya du’aa hii, na kwa baraka ya du’aa, milango ya Jannah itafunguliwa Siku ya Qiyaamah, Na hakuna Malaika aliyekurubishwa isipokuwa atajikurubisha kwa Mola Wake kwa baraka ya du’aa hii."

 

ومن قرأ هذا الدعاء أمِن من عذاب القبر، ومن الطعن والطاعون، وينتصر ببركته على أعدائهـا يا محمد، من قرأ هذا الدعاء تكون يدك في يده يوم القيامة، ومن قرأ هذا الدعاء يكون وجهه كالقمر ليلة البدر عند تمامها، والحلق في عرسات القيامة ينظرون إليه كأنه نبي من الأنبياء

 

Na Atakayeisoma du’aa hii atasalimika na adhabu ya kaburi, na atasalimika na maradhi ya tauni na atanusurika na maadui wake kutokana na baraka yake (hii du'aa). Ee Muhammad! Atakayeisoma du’aa hii, basi mkono wako utakuwa katika mkono wake Siku ya Qiyaamah, na atakayeisoma du’aa hii uso wake utakuwa kama uso wa mwezi usiku wa mwezi kuwa kamilifu na mkusanyiko katika viwanja vya Qiyaamah wakimtazama kama kwamba yeye ni miongoni mwa Manabii. 

 

 

Haijuzu kuisoma du’aa au uradi huo wa Kanzul-‘Arsh  kwa sababu zifuatazo:

 

1. Ni uzushi na uzushi ni dhambi na unamuandalia makazi ya motoni mwenye kuzua na mwenye kuisambaza. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

 

((مَنْ كَذَبَ عَلَيَّ مُتَعَمِّدًا فَلْيَتَبَوَّأْ مَقْعَدَهُ مِنْ النَّارِ)) البخاري

((Atakayenizulia uongo kwa makusudi, basi ajiandalie makazi yake motoni.)) [Al-Bukhaariy]

 

 

2. Du’aa hiyo imevuka mipaka katika kuitukuza ‘Arshi ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa).

 

 

3. Uradi huo ni uzushi wa Masufi na Mashia wa “Kanzul-‘Arsh” au “Ganjul-‘Arsh” kama wengine wanavyoiita na ambayo yamenukuliwa humo kuhusu fadhila zake; ni uzushi achilia mbali kuwa ina mambo yanayokwenda kinyume na matini (nuswuws) za Qur-aan na Sunnah.

 

4. Miongoni mwayo ni kumpa majina Allaah kwa majina yasiyothibiti katika Kitabu cha Allaah wala Sunnah za Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Mfano: Al-Burhaan (dalili). As-Swaafiy (halisi), Al-Mu’jiz (Wa Miujiza), Al-Qadiym (Wa Kale), Al-Mukhlis (Anayetakasa wengineo), Al-Faadhwil (Anayefadhilisha).  Majina yote haya si miongoni mwa Majina Mazuri ya Allaah na Sifa Zake.

 

 

5. Baada ya utafiti, imetambulika kuwa du’aa hiyo ya uzushi imenukuliwa kwa kauli mbali mbali tofauti na baadhi ya maneno yasiyofahamika maana yake na mengine makosa kataika uandishi wa Kiarabu, na hii ni dalili tosha kuwa kuwa ni uzushi wa kutupwa.

 

 

Mfano kuna wanaosema inaanza na:

 

لا إله إلا الله الملك الحق المبين،لا إله إلا الله العدل اليقين،لا إله إلا الله ربنا ورب آبائنا الأولين،سبحانك إني كنت من الظالمين،لا إله إلا الله  وحده لا شريك له،له الملك وله الحمد يُحيي ويُميت وهو حي لا يموت، بيده الخير وإليه المصير، وهو على كل شيء قدير.

 

Wengine wamenukuu:

 

لا إله إلا الله الحليم الكريم لا إله إلا الله العلي العظيم لا إله إلا الله الملك الحق المبين لا إله إلا الله الحق العدل اليقين لا إله إلا الله ربنا و رب آبائنا الأولين لا إله إلا أنت سبحانك إني كنت من الظالمين لا إله إلا الله وحده لا شريك له له الملك و له الحمد يحيي و يميت و يميت و يحيي و هو حي لا يموت بيده الخير و هو على كل شي‏ء قدير  

 

Wengine wamenukuu:

 

اللهم اني اسالك باسمك الذي اذا ذكرت به تزعزعت منه السماوات وانشقت منه الارضون وتقطعت منه السحاب وتصدعت منه الجبال وجرت منه الرياح وانتقصت منه البحار واضطربت منه الامواج وغارت منه النفوس ووجلت القلوب وزلت منه الاقدام وصمت منه النفوس ووجلت منه القلوب وزلت منه الاقدام وصمت منه الاذان وشخصت منه الابصار وخشعت منه الاصوات وخضعت له الرقاب وقامت له الارواح وسجدت له الملائكة

 

Wengine wamenukuu:

 

بسم الله الرحمنِ الرحيمِ ولا حول ولا قوة إلا بالله العلي العظيم لا إله إلا الله محمدٌ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم*  أستغفرُ اللهَ العظيمَ الذي لا إله إلا هو الحيَّ القيُّومَ بديعَ السماواتِ والأرضِ وما بينهما غفَّـارَ الذنوبِ سَتَّـارَ العيُوبِ مقلِّبَ القلُـوبِ كشَّافَ الكرُوبِ علاَّمَ الغيُوبِ * وأتوبُ إليهِ توبةَ عبدٍ صَاغِرٍ ظالِمٌ لنفسِهِ ذليـلٌ لا يملِكُ لنفسهِ ضَرَّاً ولا نفعاً ولا حياةً ولا موتاً ولا نُشوراً* يا عزيزُ يا غفَّارُ يا كريمُ يا ستَّارُ يا بارُّ يا رَبِّ يا ربّ يا رّبِّ أنا عَصَيْتُ وأنا جَنَيْتُ وأنا خالفتُ وأنا أخطأتُ ، يا مُنجِّـي موسى ، والخليلُ إبراهيم ، والمصطفى محمَّدٍ عليهُمُ الصلاة والسلام ، أسألُك يااللهُ ياحَيُّ يا قيُّومُ يا عليُّ يا عظيمُ يا رحمنُ يا رحيمُ * أنْ لا إلهَ إلا أنتَ سُبحانَك إنِّي كنتُ من الظَّالمينَ يا من لا يَخْفَى عليهِ

 

Basi tazama jinsi uongo na uzushi unavyodhihirika kwa wazushi kwa jinsi wanavyotofautiana katika kuzusha!

 

 

Tahadhari Muislamu!

 

Waislamu wanapaswa kujihadhari sana na uzushi mwingi unaotungwa na Mashia na Masufi haswa katika kupitia mlango wa du'aa. Katika mlango huo, kumepenyezwa mengi ya kumzulia Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kuizulia Dini hii tukufu ya Kiislamu.

 

Tunawanasihi Waislamu wasio na maarifa ya kutosha kwenye Dini yao, wahakikishe jambo lolote linaloenezwa kuhusu Dini na haswa haswa haya mas-alah ya du'aa, wawaulize wajuzi kabla hawajaingia katika kusambaza haraka haraka wakidhania ni khayr na kuna kupata ujira na haswa zama hizi zenye njia nyepesi za usambazaji wa khabari kupitia Whatsapp, Telegram na mitandao mingine ya kijamii.

 

Na katika mambo ya kumfanya Muislamu atahadhari na azinduke haraka, ni pindi atakapoona ujumbe umeandikwa mwisho wake, "watumie watu 10 au 50", au "usibakishe ujumbe huu kwenye simu yako au inbox yako kama unampenda Mtume au kama unampenda Allaah", au "Katika saa moja hakikisha huu ujumbe unawafikia watu 500 au 1000", au "Tuma ujumbe huu na utaona maajabu au miujiza", au " Usipotuma ujumbe huu utapatwa na balaa kadhaa, na ukituma ujumbe huu utapata thawabu kadhaa"!!

 

Hizo zote ni katika alama za uzushi na ujumbe wa uzushi, tahadhari nazo jumbe kama hizo. Usiharakishe kueneza wala kutuma. Ukiwa huna uhakika, uliza wajuzi. Na ukiwa ni mwenye maarifa, wakanye wanaoeneza na waelimishe khatari ya kuzua na umuhimu wa kufuata mafundisho sahihi yaliyothibiti.

 

Kuna du'aa nyingi sana na adhkaar ambazo ni sahihi na zimethibiti katika Qur-aan na Sunnah na watu hawazijui wala hawawezi kuzimaliza kuzisoma au kuzihifadhi na wengi hawazijui, lakini wengi wanahangaika na du'a na adhkaar za uzushi zilizotungwa na wazushi wa Kishia na Kisufi! Na huu ndio katika moja ya mitihani iliyoikumba hii Dini yetu.

 

Tunamuomba Allaah afya na salama.

 

 

 

Share