34-Fadhila Za Laa Ilaaha Illa-Allaah: Du’aa Unaporudi Safarini: Laa Ilaaha Illa Allaahu Wahdahu …. Aaibuwna, Taaibuwna, ‘Aabiduwna, Saajiduwna Li-Rabbinaa Haamiduwna…

 

Hadiyth Kuhusu Fadhila Za Laa Ilaaha Illa Allaah

 

www.alhidaaya.com

 

34-Du’aa Unaporudi Safarini:  Laa Ilaaha Illa Allaahu Wahdahu …. Aaibuwna, Taaibuwna, ‘Aabiduwna, Saajiduwna Li-Rabbinaa Haamiduwna…

 

 

 

عنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عُمَرَ رضى الله عنهما أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم كَانَ إِذَا قَفَلَ مِنْ غَزْوٍ أَوْ حَجٍّ أَوْ عُمْرَةٍ يُكَبِّرُ عَلَى كُلِّ شَرَفٍ مِنَ الأَرْضِ ثَلاَثَ تَكْبِيرَاتٍ، ثُمَّ يَقُولُ: ((لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ وَحْدَهُ لاَ شَرِيكَ لَهُ، لَهُ الْمُلْكُ، وَلَهُ الْحَمْدُ، وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَىْءٍ قَدِيرٌ، آيِبُونَ تَائِبُونَ عَابِدُونَ سَاجِدُونَ لِرَبِّنَا حَامِدُونَ، صَدَقَ اللَّهُ وَعْدَهُ وَنَصَرَ عَبْدَهُ وَهَزَمَ الأَحْزَابَ وَحْدَهُ)) البخاري

  

 

Imepokelewa kutoka kwa Ibn ’Umar   (رضي الله عنهما) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) alikuwa pindi anaporudi vitani au kutoka Hajj au ’Umrah alikuwa katika kila akipanda mlima akileta Takbiyrah (Allaahu Akbar) mara tatu kisha akisema:

 

Laa ilaaha illa Allaahu Wahdahu laa shariyka Lahu, Lahul-Mulku walahul-Hamd, wa Huwa ’alaa kulli shay-in Qadiyr.  Aaibuwna taaibuwna, ’aabiduwna, saajiduwna, li-Rabbinaa haamiduwna. Swadaqa-Allaahu Wa’dahu, wa Naswara ’Abdahu, wa Hazzamal-ahzaaba Wahdahu

 

Hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah, hali ya kuwa Peke Yake, wala hana mshirika. Ufalme ni Wake, na Himdi ni Zake, na Yeye juu ya kila kitu ni Muweza. Tunanarudi hali ya kuwa tunatubia, tunaabudu, tunasujudu, tunamhimidi Rabb wetu. Amesadikisha Allaah ahadi Yake, na Amemnusuru mja Wake, na Amevishinda vikosi peke Yake [Al-Bukhaariy katika Kitaab Al-Hajj, Kitaab Al-’Umrah, Kitaab Al-Maghaazi, Kitaab Al-Jihaad Was-Sayr (7/163) [1797], Muslim Kitaab Al-Hajj (2/980) [1344].

 

Share