37-Fadhila Za Laa Ilaaha Illa-Allaah: Mema Yanayobakia Daima: Subhaana Allaah Wal-HamduliLLaah Wa Laa Ilaaha Illa-Allaah...

Hadiyth Kuhusu Fadhila Za Laa Ilaaha Illa Allaah

 

www.alhidaaya.com

 

 

37-Mema Yanayobakia Daima

 

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ : قَالَ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ : ((خُذُوا جُنَّتَكُمْ))  قُلْنَا يَا رَسُولَ اللهِ : مِنْ عَدُوٍّ قَدْ حَضَرَ ؟ ، قَالَ:    ((لاَ،   جُنَّتَكُمْ مِنَ النَّارِ، قُولُوا : سُبْحَانَ اللهِ، وَالْحَمْدُ لِلَّهِ  وَلاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ، وَاللَّهُ أَكْبَرُ، فَإِنَّهَا يَأْتِينَ يَوْمَ الْقِيَامَةِ مُنْجِيَاتٍ، وَمُقَدَّمَاتٍ ، وَهُنَّ الْبَاقِيَاتُ الصَّالِحَاتُ))

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Jikingeni!)) Tukasema: Ee Rasuli wa Allaah; Je adui ameshatufikia? Akasema: ((Hapana bali kinga yenu kutokana na moto. Semeni:

 

 

 سُبْحَانَ اللهِ، وَالْحَمْدُ لِلَّهِ  وَلاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ، وَاللَّهُ أَكْبَرُ

 

Subhaana-Allaah, wal-HamduliLLaah, wa laa ilaaha illa-Allaah, wa Allaahu Akbar

 

Utakasifu ni wa Allaah na Himdi Anastahiki Allaah, na  hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah, na Allaah ni Mkubwa

 

Kwani yatakuja zitakuja hizo (Adhkaar) Siku ya Qiyaamah kama ni kinga na kitangulizi, nazo ni Mema yanayobakia daima)) [An-Nasaaiy fiy Sunan Al-Kubraa (10684), Atw-Twabaraniy fiy Al-Mu’jim Al-Awsatw (4027), na ameisahihisha Al-Abaaniy katika Swahiyh Al-Jaami’ (3214), Swahiyh At-Targhiyb (1567), na kwa Riwaayah nyenginezo amesahihisha katika Swahiyh Al-Jaami’ (3264), (6/482)]  

 

 

 

  

 

 

 

Share