09-Zawadi Kwa Wanandoa: Wasia wa Mume kwa Mkewe

 

 

Zawadi Kwa Wanandoa

 

09- Wasia wa Mume kwa Mkewe

 

وصية الزّ وج إلى زوجته

 

 

 

 

Amesema Abu Dardaai kumuusia mkewe: ‘Ukiniona mimi nimekasirika jaribu kuniridhisha, nami nikikuona umekasirika nitakuridhisha, vinginevyo hatutoweza kukaa pamoja.’

 

Na akasema mmoja wa waume kumwambia mke wake:

Chukua msamaha wangu yatadumu mapenzi yangu (mawadda),

Wala usizungumze katika kilele cha ghadhabu

pindi ninapo ghadhibika.

Wala usinigonge kwa mgongo wako hata mara moja

Kwani wewe hujui ni wapi jua linapozamia

Na wala usizidishe malalamiko na nguvu kuondoka

Na moyo wangu ukakukataa, na mioyo hugeuka

Nami nimeona mapenzi katika moyo na maudhi vile vile

Zikikutana, basi mapenzi hayakai yataondoka.”

 

 

Share