26-Zawadi Kwa Wanandoa: Tendo La Ndoa Ni Ibada

 

Zawadi Kwa Wanandoa

 

26-Tendo La Ndoa Ni Ibada

 

النّكاح عبادة

 

Uislamu umenyanyua hadhi ya suala la tendo la ndoa na kulifanya kuwa ni ibada, ibada ambayo wana ndoa wakiifanya hulipwa. Kwani kwa ndoa yao hii ya halali wamejiepusha na maasi na uchafu na wakaishi katika sakafu moja katika mazingira ya kufahamiana, kupendana, kushibana na mahusiano mazuri ya kubadilishana mapenzi yenye kulandana.

 

Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam)  juu yake amani na salamu anasema:

 

في بضع أحدكم صدقة

 

“…na katika kumuingilia mkeo ni sadaka.”(Muslim)

 

Tendo la ndoa ni sadaka anayotoa mume kwa mkewe, na katika ukamilifu wa neema ni mtu kuhisi kuwa haja zake zinashibishwa na ndipo hapo nafsi inapopata utulivu na malipo ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala).

 

Ibn al-Qayyim (Rahimahu Allaah)  anasema: kila ladha husaidia ladha ya siku ya mwisho, ladha hiyo hupendwa na Inaridhiwa na Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) na mtendaji hupata ladha katika sura mbili:

 

Upande wa mwanzo ni kule kustarehe na kujifurahisha na kupata utulivu wa macho.

 

Upande wa pili ni kule kumridhisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)  na huko ni  kuifikisha nafsi katika daraja la ladha iliyo bora zaidi.

 

Share