43-Zawadi Kwa Wanandoa: Kujua Fiqhi Ya Wanawake

 

Zawadi Kwa Wanandoa

 

43-Kujua Fiqhi Ya Wanawake

 

 الإلمام بفقه النسا

 

 

Ni kitu kinachopendeza kwa mume kujua na kufahamu au hata kujifunza hukumu za ki-Fiqh zinazohusiana na wanawake, kwa khofu ya kutoangukia katika haramu, na amfundishe mkewe kama hafahamu hukumu za twahara na Swalah na hedhi…

Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema:

 

يا أيها الذين آمنوا قوا أنفسكم وأهليكم نارا وقودها الناس والحجارة

 

“ Enyi mlioamini! Jiokoeni Nafsi zenu na watu wenu, na moto ambao kuni zake ni watu na mawe…” (At-Tahrym: 6)

 

 

Na ikitokea mwanamke hafahamu hukumu hizi za ki-Fiqh, au mumewe hakuweza kumfundisha ni juu yake kuwauliza Ahlu-Dhikri (wenye ujuzi) katika mabaraza ya ki-elimu yanayo jihusisha na wanawake.

 

 

Mtume (Swalla Llaahu 'alayhi wa sallam) amesema:

 

نعم  نساء الأنصار لم يمنعهنّ الحياء أن يتفقّهن في الدّين

 

“Wabora wa wanawake ni wanawake wa ki-Answaar ambao haikuwazuia haya katika kujifunza mambo ya Dini.” (Al-Bukhaariy na Muslim)

 

 

Share