01-Buluwgh Al-Maraam: Kitabu Cha Mjumuisho: Mlango Wa Adabu

 

 

بُلُوغُ الْمَرام

Buluwgh Al-Maraam

 

كِتَابُ اَلْجَامِعِ

Kitabu Cha Mjumuisho

 

 

بَابُ اَلْأَدَبِ

01-Mlango Wa Adabu

 

 

 

 

1236.

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{حَقُّ اَلْمُسْلِمِ عَلَى اَلْمُسْلِمِ سِتٌّ: إِذَا لَقِيتَهُ فَسَلِّمْ عَلَيْهِ، وَإِذَا دَعَاكَ فَأَجِبْهُ، وَإِذَا اِسْتَنْصَحَكَ فَانْصَحْهُ، وَإِذَا عَطَسَ فَحَمِدَ اَللَّهَ فَسَمِّتْهُ وَإِذَا مَرِضَ فَعُدْهُ، وَإِذَا مَاتَ فَاتْبَعْهُ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Haki ya Muislaam juu ya Muislaam ni sita:[1] unapokutana naye msalimie, anapokualika muitike, anapokutaka nasaha mnasihi, anapopiga chafya na akamhimidi Allaah mrehemu, anapougua mtembelee na akifa msindiize.” [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

1237.

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ‏ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{انْظُرُوا إِلَى مَنْ هُوَ أَسْفَلَ مِنْكُمْ، وَلَا تَنْظُرُوا إِلَى مَنْ هُوَ فَوْقَكُمْ، فَهُوَ أَجْدَرُ أَنْ لَا تَزْدَرُوا نِعْمَةَ اَللَّهِ عَلَيْكُمْ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mtazameni ambaye yuko chini yenu[2] wala msimtazame ambaye yuko juu yenu, kwani kufanya hivyo hamtadharau neema za Allaah juu yenu.” [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1238.

وَعَنْ اَلنَوَّاسِ بْنِ سَمْعَانَ رضى الله عنه‏ قَالَ: سَأَلْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏عَنْ اَلْبِرِّ وَالْإِثْمِ؟ فَقَالَ: {اَلْبِرُّ: حُسْنُ اَلْخُلُقِ، وَالْإِثْمُ: مَا حَاكَ فِي صَدْرِكَ، وَكَرِهْتَ أَنْ يَطَّلِعَ عَلَيْهِ اَلنَّاسُ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa Anawwaas bin Sam’aan[3] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema nilimuuliza Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): “Kuhusu wema na dhambi, akasema: “Wema ni tabia njema,[4] na dhambi[5] ni inayotia shaka katika nafsi yako na ukachukia watu kuona.” [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

1239.

وَعَنْ اِبْنِ مَسْعُودٍ ‏ رضى الله عنه ‏ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏{إِذَا كُنْتُمْ ثَلَاثَةً، فَلَا يَتَنَاجَى اِثْنَانِ دُونَ اَلْآخَرِ، حَتَّى تَخْتَلِطُوا بِالنَّاسِ; مِنْ أَجْلِ أَنَّ ذَلِكَ يُحْزِنُهُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِمُسْلِمٍ.

Kutoka kwa Ibn Mas-‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mnapokuwa watatu, wawili wasinong’one bila yule mwingine (kusikia)[6] mpaka mchanganyike na watu, kwani hilo litamhuzunisha.” [Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Muslim]

 

 

 

1240.

وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ ‏رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا‏ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏{لَا يُقِيمُ اَلرَّجُلُ اَلرَّجُلَ مِنْ مَجْلِسِهِ، ثُمَّ يَجْلِسُ فِيهِ، وَلَكِنْ تَفَسَّحُوا، وَتَوَسَّعُوا} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mmoja wenu asimsimamishe mtu kwenye kikao chake kisha akaketi yeye,[7] lakini kunjukeni na toeni nafasi.” [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1241.

وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ ‏رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا‏ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ‏ صلى الله عليه وسلم ‏{إِذَا أَكَلَ أَحَدُكُمْ طَعَامًا، فَلَا يَمْسَحْ يَدَهُ، حَتَّى يَلْعَقَهَا، أَوْ يُلْعِقَهَا} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ.

Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Anapomaliza kula mmoja wenu asipanguse vidole vyake mpaka avirambe au avirambishe.”[8] [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1242.

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه ‏ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ‏ صلى الله عليه وسلم ‏{لِيُسَلِّمْ اَلصَّغِيرُ عَلَى اَلْكَبِيرِ، وَالْمَارُّ عَلَى اَلْقَاعِدِ، وَالْقَلِيلُ عَلَى اَلْكَثِيرِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

وَفِي رِوَايَةٍ لِمُسْلِمٍ: {وَالرَّاكِبُ عَلَى اَلْمَاشِي}

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mdogo amsalimie mkubwa, anayetembea amsalimie aliye kaa,[9] na wachache wawasalimie wengi.” [Bukhaariy, Muslim]

Na katika Riwaayah ya Muslim: “…na aliyepanda amsalimie anayetembea.”

 

 

 

1243.

وَعَنْ عَلِيٍّ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏{يُجْزِئُ عَنْ اَلْجَمَاعَةِ إِذَا مَرُّوا أَنْ يُسَلِّمَ أَحَدُهُمْ، وَيُجْزِئُ عَنْ اَلْجَمَاعَةِ أَنْ يَرُدَّ أَحَدُهُمْ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالْبَيْهَقِيُّ

Kutoka kwa ‘Aliy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kundi linatoshelezwa kwa mtu mmoja wao kusalimia, na mtu mmoja wao hutosheleza anapojibu salaam.”[10] [Imetolewa na Ahmad na Al-Bayhaqiyy]

 

 

 

1244.

 وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{ لَا تَبْدَؤُوا اَلْيَهُودَ وَالنَّصَارَى بِالسَّلَامِ، وَإِذَا لَقَيْتُمُوهُمْ فِي طَرِيقٍ، فَاضْطَرُّوهُمْ إِلَى أَضْيَقِهِ } أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Msianze kuwasalimia Mayahudi wala Manaswara,[11] munapokutana na mmoja wao njiani msogezeni upande wenye dhiki zaidi.”[12] [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

1245.

وَعَنْهُ عَنْ اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم ‏قَالَ: {إِذَا عَطَسَ أَحَدُكُمْ فَلْيَقُلْ: اَلْحَمْدُ لِلَّهِ، وَلْيَقُلْ لَهُ أَخُوهُ يَرْحَمُكَ اَللَّهُ، فَإِذَا قَالَ لَهُ: يَرْحَمُكَ اَللَّهُ، فَلْيَقُلْ: يَهْدِيكُمُ اَللَّهُ، وَيُصْلِحُ بَالَكُمْ} أَخْرَجَهُ اَلْبُخَارِيُّ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Akipiga chafya mmoja wenu aseme:

 اَلْحَمْدُ لِلَّهِ

Alhamdulillaah[13]

 na nduguye au mwenzie amuambie

 يَرْحَمُكَ اَللَّهُ

(Allaah Akurehemu).

Atakapomuambia

 يَرْحَمُكَ اَللَّهُ

naye amuambie:

 يَهْدِيكُمُ اَللَّهُ، وَيُصْلِحُ بَالَكُمْ

(Allaah Awaongeze na Awatengenezee mambo yenu).” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]

 

 

 

1246.

وَعَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏{لَا يَشْرَبَنَّ أَحَدٌ مِنْكُمْ قَائِمًا} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Asinywe mmoja wenu kwa kusimama.”[14] [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

1247.

وَعَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{إِذَا اِنْتَعَلَ أَحَدُكُمْ فَلْيَبْدَأْ بِالْيَمِينِ، وَإِذَا نَزَعَ فَلْيَبْدَأْ بِالشِّمَالِ، وَلْتَكُنْ اَلْيُمْنَى أَوَّلَهُمَا تُنْعَلُ، وَآخِرَهُمَا تُنْزَعُ}

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Anapovaa mmoja wenu viatu aanze kulia, na anapovua aanze kushoto. Upande wa kulia uwe wa kwanza kuvaliwa na wa mwisho kuvuliwa.”[15]

 

 

 

1248.

وَعَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{لَا يَمْشِ أَحَدُكُمْ فِي نَعْلٍ وَاحِدَةٍ، وَلْيُنْعِلْهُمَا جَمِيعًا، أَوْ لِيَخْلَعْهُمَا جَمِيعًا} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Asitembee mmoja wenu kwa kiatu kimoja, avae vyote au avue vyote.”[16] [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1249.

وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ ‏رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا‏ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏{لَا يَنْظُرُ اَللَّهُ إِلَى مَنْ جَرَّ ثَوْبَهُ خُيَلَاءَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Allaah Hamtazami anayeburuta nguo yake kwa kibri.”[17] [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1250.

وَعَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏قَالَ: {إِذَا أَكَلَ أَحَدُكُمْ فَلْيَأْكُلْ بِيَمِينِهِ، وَإِذَا شَرِبَ فَلْيَشْرَبْ بِيَمِينِهِ، فَإِنَّ اَلشَّيْطَانَ يَأْكُلُ بِشِمَالِهِ، وَيَشْرَبُ بِشِمَالِهِ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Anapokula mmoja wenu ale kwa mkono wa kulia. Na anapokunywa anywe kwa kulia kwake. Kwa hakika shaytwaan hula anapotumia kushoto na hunywa anapokunywa kwa kushoto kwake.”[18] [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

1251.

وَعَنْ عَمْرِو بْنِ شُعَيْبٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ جَدِّهِ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏{كُلْ، وَاشْرَبْ، وَالْبَسْ، وَتَصَدَّقْ فِي غَيْرِ سَرَفٍ، وَلَا مَخِيلَةٍ} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَأَحْمَدُ، وَعَلَّقَهُ اَلْبُخَارِيُّ

Kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb kutoka kwa baba yake, naye kutoka kwa babu yake amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kula, kunywa, vaa na utoe swadaqah bila ya israfu wala kibri.”[19] [Imetolewa na Abuu Daawuwd na Ahmad. Bukhaariy ameitaja kuwa ni Mu’allaq]

 

 

[1] Tunajifunza katika Hadiyth hii kuwa kusimamia majukumu haya ni wajibu. Baadhi ya Wanazuoni wanaona kuwa ni Mandub ambayo haitakiwi kuachwa hata mara moja.

[2] Hili ni hamasisho kwa watu kulinganisha hali zao kiuchumi na wale walio chini yao, kwani kufanya hivyo kunajenga iymaan na kuwa na taqwa zaidi katika moyo wa mtu. Mara nyingi kuwaangalia watu walio juu na hadhi kunapelekea katika tamaa, ambayo inapelekea katika hisia ya kutoridhika na husuda na wivu juu yao.

 

[3] Anawwaas bin Sam’aan bin Khaalid Al-Kilabi Al-‘Amiri alikuwa ni Swahaba katika watu wa Shaam. Inasemekana kuwa baba yake alimtembelea Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) ambaye alimuombea. Alimpa pea za ndara ambazo Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alizipokea.

 

[4] Tabia njema inahusisha utii kwa Allaah, kutoa swadaqah, kuwatendea watu vizuri, kuwavumilia wanaokukosea, kuhusubiana nao kwa wema, kuimarisha ujamaa na udugu na watu n.k.

 

[5] Kuna madhambi ya aina mbili: (a) Ni yale makatazo ya kishariy’ah yaliyokuwa wazi. Ni wajibu kwa watu wote kuachana nayo. (b) Ni yale ambayo makatazo yake hayako wazi ila ni mambo ambayo hayapendwi kufanywa, na watu wanayachukia na kuhusu uzito juu yake. Hivyo basi, ni bora kuyaacha.

 

[6] Hadiyth hii inathibitisha Uislaam kuheshimu hisia za watu. Watu hawatakiwi kufanya vitu vitakavyowaletea watu wengine hisia mbaya.

 

[7] Hii inathibitisha kuwa ni haki ya mtu aliyekaa katika kikao cha awali kuendelea kukaa pale mwanzo. Haruhusiwi mtu mwingine kukaa sehemu aliyokwisha kaa mwenzake hata kama atakuwa ametoka kidogo basi ni haki yake pale atakaporudi. Au hawezi kumuondoa sehemu aliyekwisha kaa isipokuwa kwa kuomba kusogezana nae apate nafasi.

 

[8] Sababu ya tukio hili limeelezwa na maneno ya Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): “Hujui ni sehemu gani katika chakula chako chenye baraka.”

 

[9] Hadiyth nyingine inaelezea kuwa waliopanda wawasalimie wanaotembea na anayepita amsalimie aliyesimama. Ikiwa kuna watu wawili wanatembea, mmoja inapasa amsalimie mwenzake. Hata hivyo, mbora ni yule anayeanza kutoa salaam. Wanazuoni wamekubaliana kuwa suala hili sio suala la mtu kutaka au kutotaka bali ni suala la lazima.

[10] Kuanza kutoa salaam ni suala la lazima kwa wote na kujibu ni suala la lazima kwa wote. Hata hivyo inatosheleza kama mmoja atasalimia na wengine kujibu.

 

[11] Wanazuoni wengi wa mwanzo wana rai kuwa Muislaam asitangulie kumsalimia kafiri. Akitoa salaam basi salaam yake ijibiwe. Wanazuoni wengine ni wenye rai kuwa ni ruhusa Waislaam kuanza kuwasalimia makafiri kama si jambo linaloweza kuzuilika.

[12] Kuwabana kwenye njia ya dhiki ni kutowapa heshima yao. Kama sehemu ina zahama basi amruhusu kwanza Muislaam apite kisha afuatie kafiri.

 

[13] Mtu anatakiwa aendelee kujibu hadi chafya ya tatu (zenye kufuatana). Chafya ikiongezeka zaidi ya hapo hatakiwi kujibu.

[14] Kunywa maji kwa kusimama hakuingii katika makatazo makubwa, bali ni makatazo ya kushauri, ila ikiwa mtu ana sababu za kishariy’ah.

 

[15] Kimsingi kila jambo zuri linatakiwa lianze kwa upande wa kuume, wakati mambo mengine ni kwa upande wa kushoto. Kwa mfano, kuvaa viatu, kuchana nywele na kuchukua ‘udwuu yote yanatakiwa yaanze kwa upande wa kuume, kuvua viatu, kujisafisha katika sehemu za siri yaanze upande wa kushoto.

[16] Hili vile vile ni katazo la kushauri, silo tatizo kubwa, na huu ndio muono wa Wanazuoni wengi.

 

[17] Mtu ambaye nguo yake inaburuza chini ya kifundo kwa kusahau au kwa kuwa tumbo lake ni kubwa kiasi cha kuwa hawezi kuzuia nguo yake kuanguka, ni watu wasio husika na hukumu hii. Pamoja na kuwa adhabu inahusisha suala la kibri lakini kuna makatazo ya jumla (bila hata kuhusisha kibri cha mtu) ya kutoruhusu nguo kuwa chini ya vifundo viwili, kulingana na Hadiyth zingine Swahiyh. Hukumu hii inawahusu wanaume peke yao, kwani wanawake wanaelekezwa washushe nguo zao kiasi cha kufunika miguu yao.

 

[18] Hadiyth hii inasisitiza matumizi ya mkono wa kulia kwa kulia na kunywea, ama makatazo ni kwa ajili ya mkono wa kushoto kufanyia mambo hayo.

[19] Katika Hadiyth hii tunapata maelezo ya ndani zaidi kuhusu aayah ya Qur-aan inayosema:

 وَكُلُوا وَاشْرَبُوا وَلَا تُسْرِفُوا

(…na kuleni na kunyweni…) [Al-A’raaf: 31].

Hadiyth hii inasisitiza maadamu ni haraam kufanya matumizi ya kupindukia kwa vitu vilivyokuwa ni halaal kwa mtu, iweje iruhusiwe kwa vitu ambavyo vimekatazwa kabisa. Matumizi haya ya kupindukia katika lugha ya Kiarabu yanaitwa Israaf.

Share