02-Buluwgh Al-Maraam: Kitabu Cha Mjumuisho: Mlango Wa Wema Na Kuunga Kizazi

 

 

بُلُوغُ الْمَرام

Buluwgh Al-Maraam

 

كِتَابُ اَلْجَامِعِ

Kitabu Cha Mjumuisho

 

بَابُ اَلْبِرِّ وَالصِّلَةِ

02-Mlango Wa Wema Na Kuunga Kizazi

 

 

 

 

 

1252.

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{مَنْ أَحَبَّ أَنْ يُبْسَطَ عَلَيْهِ فِي رِزْقِهِ، وَأَنْ يُنْسَأَ لَهُ فِي أَثَرِهِ، فَلْيَصِلْ رَحِمَهُ} أَخْرَجَهُ اَلْبُخَارِيُّ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Anayependa kukunjuliwa rizki yake na kurefushwa umri wake na aunge kizazi chake.”[1] [Imetolewa na Al-Bukhaariy]

 

 

 

1253.

وَعَنْ جُبَيْرِ بْنِ مُطْعِمٍ رضى الله عنه‏ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏{لَا يَدْخُلُ اَلْجَنَّةَ قَاطِعٌ} يَعْنِي: قَاطِعَ رَحِمٍ.‏ مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Jubayr bin Mutw’im (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hataingia Jannah mkataji (yaani mkata udugu).”[2] [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1254.

وَعَنْ اَلْمُغِيرَةِ بْنِ سَعِيدٍ رضى الله عنه‏ عَنْ رَسُولِ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏قَالَ: {إِنَّ اَللَّهَ حَرَّمَ عَلَيْكُمْ عُقُوقَ اَلْأُمَّهَاتِ، وَوَأْدَ اَلْبَنَاتِ، وَمَنْعًا وَهَاتِ، وَكَرِهَ لَكُمْ قِيلَ وَقَالَ، وَكَثْرَةَ اَلسُّؤَالِ وَإِضَاعَةَ اَلْمَالِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Al-Mughiyrah bin Sa’iyd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakika Allaah Amewaharamishia kuwaasi mama (zenu), na kuzuia na kukusanya (mali), kuzika mabinti (wakiwa hai). Na Amechukia kwenu: maneno ya uzushi, kuuliza kwingi na kuharibu mali.” [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1255.

وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ عُمَرَ ‏رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا‏، عَنْ اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم ‏قَالَ: {رِضَا اَللَّهِ فِي رِضَا اَلْوَالِدَيْنِ، وَسَخَطُ اَللَّهِ فِي سَخَطِ اَلْوَالِدَيْنِ} أَخْرَجَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ وَالْحَاكِمُ

Kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Radhi ya Allaah iko katika radhi ya wazazi wawili, na hasira za Allaah ziko katika hasira za wazazi wawili.”[3] [Imetolewa na At-Tirmidhiy, na akaisahihisha Ibn Hibbaan na Al-Haakim]

 

 

 

1256.

وَعَنْ أَنَسٍ رضى الله عنه عَنْ اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم ‏قَالَ: {وَاَلَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ لَا يُؤْمِنُ عَبْدٌ حَتَّى يُحِبَّ لِجَارِهِ ‏ أَوْ لِأَخِيهِ‏ مَا يُحِبُّ لِنَفْسِهِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Anas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Naapa kwa Ambaye nafsi yangu imo Mkononi Mwake, haamini mja yeyote mpaka ampendelee jirani yake au nduguye (Muislamu) analopendelea nafsi yake.”[4] [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1257.

وَعَنْ اِبْنِ مَسْعُودٍ رضى الله عنه قَالَ سَأَلْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏أَيُّ اَلذَّنْبِ أَعْظَمُ؟ قَالَ: {أَنْ تَجْعَلَ لِلَّهِ نِدًّا، وَهُوَ خَلَقَكَ.‏ قُلْتُ ثُمَّ أَيُّ؟ قَالَ: ثُمَّ أَنْ تَقْتُلَ وَلَدَكَ خَشْيَةَ أَنْ يَأْكُلَ مَعَكَ.‏ قُلْتُ: ثُمَّ أَيُّ؟ قَالَ: ثُمَّ أَنْ تُزَانِيَ حَلِيلَةَ جَارِكَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Ibn Mas-‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema nilimuuliza Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): “Ni dhambi gani kubwa zaidi? Akasema: ni kumfanyia Allaah mshirika hali Yeye Amekuumba. Nikasema: kisha ni dhambi gani? Akasema: ni kumuua mwanao kwa kuogopa asije kula pamoja nawe. Nikasema: kisha ni dhambi gani? Akasema: ni kuzini na mke wa jirani yako.”[5] [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1258.

وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ عَمْرِو بْنِ الْعَاصِ ‏رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا‏ أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏قَالَ: {مِنْ اَلْكَبَائِرِ شَتْمُ اَلرَّجُلِ وَالِدَيْهِ.‏ قِيلَ: وَهَلْ يَسُبُّ اَلرَّجُلُ وَالِدَيْهِ؟ قَالَ: نَعَمْ.‏ يَسُبُّ أَبَا اَلرَّجُلِ، فَيَسُبُّ أَبَاهُ، وَيَسُبُّ أُمَّهُ، فَيَسُبُّ أُمَّهُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amr bin Al-‘Aasw (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Miongoni mwa madhambi makubwa ni mtu kutukana wazazi wake. Maswahaba wakasema: mtu anaweza kutukana wazazi wake? Akasema: “Ndiyo, atamtukana baba wa mtu naye anamtukana baba yake, na atamtukana mama wa mtu naye atamtukana mama yake.”[6] [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1259.

وَعَنْ أَبِي أَيُّوبَ رضى الله عنه أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ‏ صلى الله عليه وسلم ‏قَالَ: {لَا يَحِلُّ لِمُسْلِمٍ أَنْ يَهْجُرَ أَخَاهُ فَوْقَ ثَلَاثِ لَيَالٍ يَلْتَقِيَانِ، فَيُعْرِضُ هَذَا، وَيُعْرِضُ هَذَا، وَخَيْرُهُمَا اَلَّذِي يَبْدَأُ بِالسَّلَامِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Abuu Ayyuwb (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Si halaal kwa Muislaam kumhama nduguye zaidi ya siku tatu;[7] anakutana naye, huyu akampa mgongo na huyo akampa mgongo, na mbora kati yao ni yule anayeanza kutoa salaam.” [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1260.

عَنْ جَابِرٍ رضى الله عنه‏ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{كُلُّ مَعْرُوفٍ صَدَقَةٌ} أَخْرَجَهُ اَلْبُخَارِيُّ

Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kila jema ni swadaqah.”[8] [Imetolewa na Al-Bukhaariy]

 

 

 

1261.

وَعَنْ أَبِي ذَرٍّ رضى الله عنه‏ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{لَا تَحْقِرَنَّ مِنْ اَلْمَعْرُوفِ شَيْئًا، وَلَوْ أَنْ تَلْقَى أَخَاكَ بِوَجْهٍ طَلْقٍ}

Kutoka kwa Abuu Dharri (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Usidharau chochote katika wema[9] hata kama ni kukutana na nduguyo kwa uso mkunjufu.” [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

1262.

وَعَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{إِذَا طَبَخْتَ مَرَقَةً، فَأَكْثِرْ مَاءَهَا، وَتَعَاهَدْ جِيرَانَكَ} أَخْرَجَهُمَا مُسْلِمٌ

Kutoka kwa Abuu Dharri (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Unapopika mchuzi zidisha maji yake na umpe jirani yako.”[10] [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

1263.

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{مَنْ نَفَّسَ عَنْ مُؤْمِنٍ كُرْبَةً مِنْ كُرَبِ اَلدُّنْيَا، نَفَّسَ اَللَّهُ عَنْهُ كُرْبَةً مِنْ كُرَبِ يَوْمِ اَلْقِيَامَةِ ، وَمَنْ يَسَّرَ عَلَى مُعْسِرٍ، يَسَّرَ اَللَّهُ عَلَيْهِ فِي اَلدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ، وَمَنْ سَتَرَ مُسْلِمًا، سَتَرَهُ اَللَّهُ فِي اَلدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ، وَاَللَّهُ فِي عَوْنِ اَلْعَبْدِ مَا كَانَ اَلْعَبْدُ فِي عَوْنِ أَخِيهِ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kumfariji katika dhiki Muumini miongoni mwa dhiki za duniani,[11] Allaah Atamfariji katika dhiki miongoni mwa dhiki za Siku ya Qiyaamah. Mwenye kumrahisishia mwenye uzito, Allaah Atamrahisishia duniani na Aakhirah. Mwenye kumsitiri Muislaam, Allaah Atamsitiri duniani na Aakhirah. Allaah Yumo katika kumsaidia mja madamu mja huyo yumo katika kumsaidia nduguye.” [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

1264.

وَعَنْ أَبِي مَسْعُودٍ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏{مَنْ دَلَّ عَلَى خَيْرٍ، فَلَهُ مِثْلُ أَجْرِ فَاعِلِهِ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa Abuu Mas-‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kujulisha kheri atapata mfano wa ujira (malipo) wa mwenye kuifanya.” [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

1265.

وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ ‏رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا‏ قَالَ: عَنِ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم ‏قَالَ: {مِنْ اسْتَعَاذَكُمْ بِاَللَّهِ فَأَعِيذُوهُ، وَمَنْ سَأَلَكُمْ بِاَللَّهِ فَأَعْطُوهُ، وَمَنْ أَتَى إِلَيْكُمْ مَعْرُوفًا فَكَافِئُوهُ، فَإِنْ لَمْ تَجِدُوا، فَادْعُوا لَهُ} أَخْرَجَهُ اَلْبَيْهَقِيُّ.‏

Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kujilinda kwenu kwa Allaah, basi mlindeni na mwenye kuwaomba kwa Jina la Allaah mpeni, na mwenye kuwatendea wema mlipeni, msipopata cha kumlipa muombeeni du’aa.” [Imetolewa na Al-Bayhaqiy]

 

[1] Swali linalojitokeza hapa ni kuwa maadamu ya kuwa umri ulishapangwa, iweje wema kwa ndugu na jamaa kutaongeza umri wa mtu? Jibu la swali hili ni kuwa umri wa mtu upo katika elimu ya Allaah, hubaki wala haubadiliki, lakini ule ambao upo katika elimu ya Malaika muhusika wa maisha ya watu unaweza kupungua na kuongezeka vivyo hivyo. Kwa maneno mengine ni kuwa, Malaika wanapewa elimu ya Qadar iliyowekwa na siyo ile ya mwisho na yenyewe kabisa. Kwa mfano, anaambiwa ikiwa mtu fulani anawafanyia wema jamaa zake, atapewa umri wa miaka mia moja, vinginevyo utapunguzwa hadi miaka sitini.

[2] Hiki ni kitisho kikali kwa mwenye kukata udugu. Neno la Kiarabu linalotumika ni Rahm, neno hili linakusanya mahusiano yote na watu ambao ni Mahram na wale wote wenye haki ya kurithi.

[3] Kutomtii mzazi ni katika madhambi makubwa, madamu tu hakukulazimisha kufanya jambo linalopingana na Shariy’ah.

 

[4] Hadiyth hii inaelezea majukumu makubwa aliyonayo mtu kwa jirani zake.

[5] Hadiyth hii inatupa mafundisho kuwa madhambi makubwa yanatofautiana, kulingana na adhabu zake. Madhambi ya kuzini yanakatazwa kwa ujumla, lakini kulifanya jambo hilo kwa mke wa jirani ni jambo baya zaidi.

[6] Hukmu inayopatikana katika Hadiyth hii ni kuwa jambo lolote ambalo linapelekea katika makatazo linakatazwa vile vile. Hata kama aliyefanya jambo lile hakukusudia kufanya jambo lililokatazwa.

 

[7] Ikiwa sababu ya jambo hilo ni mambo binafsi, haitakiwi mfarakano huo udumu zaidi ya masiku tatu. Lakini ikiwa jambo hilo linahusiana na jambo la Dini, hakuna makadirio ya muda kwani jambo hilo ni sehemu ya iymaan.

[8] Swadaqah haina maana finyu ya mtu kutoa chochote tu katika mali yake. Bali maana yake ni pana, yaani mtu kufanya tendo lolote zuri na kuacha jambo lolote baya nayo ni Swadaqah.

 

[9] Bashasha inaweza kuonekana ni jambo dogo machoni mwa watu, jambo hili limepewa nafasi kubwa katika malipo na fadhila zake.

[10] Hukumu hii inakuwa ni ya faradhi ikiwa jirani yako ni mtu maskini. Ikiwa jirani ni tajiri basi hukumu hii inakuwa ni kwa kufadhilisha na kupendezesha zaidi. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kila Jibriyl anaposhuka kwangu huniusia kuhusu kumfanyia wema jirani kiasi cha kufikiri kuwa huenda jirani akanirithi.”

 

[11] Mahimizo tunayoyapata hapa ni ule ubora na umuhimu wa kumsaidia Muumini.

Share