05-Buluwgh Al-Maraam: Kitabu Cha Mjumuisho: Mlango Wa Mahimizo Ya Akhlaaq (Tabia) Njema

 

بُلُوغُ الْمَرام

Buluwgh Al-Maraam

 

كِتَابُ اَلْجَامِعِ

Kitabu Cha Mjumuisho

 

بَابُ اَلتَّرْغِيبِ فِي مَكَارِمِ اَلْأَخْلَاقِ

05-Mlango wa Mahimizo Ya Akhlaaq (Tabia) Njema

 

 

 

1313.

عَنِ اِبْنِ مَسْعُودٍ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {عَلَيْكُمْ بِالصِّدْقِ، فَإِنَّ اَلصِّدْقَ يَهْدِي إِلَى اَلْبِرِّ، وَإِنَّ اَلْبِرَّ يَهْدِي إِلَى اَلْجَنَّةِ، وَمَا يَزَالُ اَلرَّجُلُ يَصْدُقُ، وَيَتَحَرَّى اَلصِّدْقَ، حَتَّى يُكْتَبَ عِنْدَ اَللَّهِ صِدِّيقًا، وَإِيَّاكُمْ وَالْكَذِبَ، فَإِنَّ اَلْكَذِبَ يَهْدِي إِلَى اَلْفُجُورِ، وَإِنَّ اَلْفُجُورَ يَهْدِي إِلَى اَلنَّارِ، وَمَا يَزَالُ اَلرَّجُلُ يَكْذِبُ، وَيَتَحَرَّى اَلْكَذِبَ، حَتَّى يُكْتَبَ عِنْدَ اَللَّهِ كَذَّابًا} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Ibn Mas-‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Shikamaneni na ukweli. Hakika ukweli unaongoza kwenye wema na wema unaongoza Jannah. Mtu hataacha kusema kweli na anachagua ukweli mpaka aandikwe mbele ya Allaah kuwa ni mkweli. Nawatahadharisheni na uongo. Hakika uongo huongoza kwenye uovu, na uovu huongoza motoni. Mtu hataacha kudanganya na anaendelea kudanganya mpaka aandikwe mbele ya Allaah kuwa ni mdanganyifu.” [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1314.

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {إِيَّاكُمْ وَالظَّنَّ، فَإِنَّ اَلظَّنَّ أَكْذَبُ اَلْحَدِيثِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ   عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Tahadharini na dhana, hakika dhana ni mazungumzo ya uongo.” [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1315.

وَعَنْ أَبِي سَعِيدٍ اَلْخُدْرِيِّ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {إِيَّاكُمْ وَالْجُلُوسَ بِالطُّرُقَاتِ. قَالُوا: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! مَا لَنَا بُدٌّ مِنْ مَجَالِسِنَا، نَتَحَدَّثُ فِيهَا.‏ قَالَ " فَأَمَّا إِذَا أَبَيْتُمْ، فَأَعْطُوا اَلطَّرِيقَ حَقَّهُ. قَالُوا: وَمَا حَقُّهُ؟قَالَ:" غَضُّ اَلْبَصَرِ، وَكَفُّ اَلْأَذَى، وَرَدُّ اَلسَّلَامِ، وَالْأَمْرُ بِالْمَعْرُوفِ، وَالنَّهْيُ عَنْ اَلْمُنْكَرِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Tahadharini kukaa njiani.[1] Wakasema: Ee Rasuli wa Allaah! Hatuna budi na vikao vyetu. Akasema: “Iwapo mtakataa isipokuwa kukaa basi ipeni njia haki yake. Wakasema: Ni ipi haki ya njia? Akasema: ni kuinamisha macho (kutotazama yalio haramishwa), kuondoa udhia, kurudisha salaam, kuamrisha mema na kukataza mabaya.” [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1316.

وَعَنْ مُعَاوِيَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {مَنْ يُرِدِ اَللَّهُ بِهِ خَيْرًا، يُفَقِّهْهُ فِي اَلدِّينِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Mu’aawiyah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Anayemtakia Allaah kheri Humjaalia ufaqihi (‘ilmu ya kina) katika Dini.”[2] [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1317.

وَعَنْ أَبِي اَلدَّرْدَاءِ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {مَا مِنْ شَيْءٍ فِي اَلْمِيزَانِ أَثْقَلُ مِنْ حُسْنِ اَلْخُلُقِ} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَاَلتِّرْمِذِيُّ وَصَحَّحَهُ

Kutoka kwa Abuu Ad-Dardaa (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakuna jambo zito katika mizani ya Muumini Siku ya Qiyaamah kama khulqa (tabia) njema.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na At-Tirmidhiy na akaisahihisha]

 

 

 

1318.

وَعَنِ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {اَلْحَيَاءُ مِنْ اَلْإِيمَانِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hayaa ni katika iymaan.”[3] [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1319.

وَعَنْ أَبِي مَسْعُودٍ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {إِنَّ مِمَّا أَدْرَكَ اَلنَّاسُ مِنْ كَلَامِ اَلنُّبُوَّةِ اَلْأُولَى: إِذَا لَمْ تَسْتَحِ، فَاصْنَعْ مَا شِئْتَ} أَخْرَجَهُ اَلْبُخَارِيُّ

Kutoka kwa Abuu Mas-‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakika miongoni mwa waliyopata watu kutoka katika mafundisho ya Manabiy wa mwanzo ni: usipostahi fanya utakalo.”[4] [Imetolewa na Al-Bukhaariy]

 

 

 

1320.

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {اَلْمُؤْمِنُ اَلْقَوِيُّ خَيْرٌ وَأَحَبُّ إِلَى اَللَّهِ مِنْ اَلْمُؤْمِنِ اَلضَّعِيفِ، وَفِي كُلٍّ خَيْرٌ، اِحْرِصْ عَلَى مَا يَنْفَعُكَ، وَاسْتَعِنْ بِاَللَّهِ، وَلَا تَعْجَزْ، وَإِنْ أَصَابَكَ شَيْءٌ فَلَا تَقُلْ: لَوْ أَنِّي فَعَلْتُ كَانَ كَذَا وَكَذَا، وَلَكِنْ قُلْ: قَدَّرَ اَللَّهُ وَمَا شَاءَ فَعَلَ; فَإِنَّ لَوْ تَفْتَحُ عَمَلَ اَلشَّيْطَانِ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Muumini mwenye nguvu ni bora na anapendeza mno kwa Allaah[5] kuliko Muumini dhaifu, na katika wote (hao) muna kheri. Jali linalokunufaisha na muombe Allaah msaada wala usichoke. Utakapopatwa na jambo usiseme ‘Lau ningalifanya kadha wa kadha’ isipokuwa sema:

قَدَّرَ اَللَّهُ وَمَا شَاءَ فَعَلَ

‘Allaah Amekadiria, na Atakalo huwa’

 

kwani neno ‘lau’ hufungua amali ya shaytwaan.” [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

1321.

وَعَنْ عِيَاضِ بْنِ حِمَارٍ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ  صلى الله عليه وسلم {إِنَّ اَللَّهَ أَوْحَى إِلَيَّ أَنْ تَوَاضَعُوا، حَتَّى لَا يَبْغِيَ أَحَدٌ عَلَى أَحَدٍ، وَلَا يَفْخَرَ أَحَدٌ عَلَى أَحَدٍ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa ‘Iyaadw bin Himaar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakika Allaah Amenifunulia Wahy kwamba nyenyekeeni ili yeyote asimdhulumu yeyote wala yeyote asijifakhiri juu ya yeyote.”[6] [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

1322.

وَعَنْ أَبِي اَلدَّرْدَاءِ رضى الله عنه عَنْ اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {مَنْ رَدَّ عَنْ عِرْضِ أَخِيهِ بِالْغَيْبِ، رَدَّ اَللَّهُ عَنْ وَجْهِهِ اَلنَّارَ يَوْمَ اَلْقِيَامَةِ} أَخْرَجَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَحَسَّنَهُ

وَلِأَحْمَدَ، مِنْ حَدِيثِ أَسْمَاءَ بِنْتِ يَزِيدَ نَحْوُهُ

Kutoka kwa Abuu Ad-Dardaa (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Atakayerudisha heshima ya nduguye asiyekuwepo,[7] Allaah Ataepusha uso wake dhidi ya moto siku ya Qiyaamah.” [Imetolewa na At-Tirmidhiy na amesema ni Hasan. Ahmad ana Hadiyth inayofanana kutoka kwa Asmaa[8] bint Yaziyd]

 

 

 

1323.

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {مَا نَقَصَتْ صَدَقَةٌ مِنْ مَالٍ، وَمَا زَادَ اَللَّهُ عَبْدًا بِعَفْوٍ إِلَّا عِزًّا، وَمَا تَوَاضَعَ أَحَدٌ لِلَّهِ إِلَّا رَفَعَهُ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Swadaqah haijapunguza mali, Allaah Hamzidishii mja kwa msamaha ila utukufu, na hanyenyekei yeyote kwa ajili ya Allaah isipokuwa Allaah (عز وجل) Atamuinua.”[9] [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

1324.

وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ سَلَّامٍ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {يَا أَيُّهَا اَلنَّاسُ! أَفْشُوا اَلسَّلَام، وَصِلُوا اَلْأَرْحَامَ، وَأَطْعِمُوا اَلطَّعَامَ، وَصَلُّوا بِاللَّيْلِ وَالنَّاسُ نِيَامٌ، تَدْخُلُوا اَلْجَنَّةَ بِسَلَامٍ} أَخْرَجَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ وَصَحَّحَهُ

Kutoka kwa ‘Abdullaah bin Salaam (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Enyi watu! Enezeni salaam, na lisheni chakula, na ungeni kizazi na mswali (usiku) hali ya watu wamelala, mtaingia Jannah kwa amani.” [Imetolewa na At-Tirmidhiy na akaisahihisha]

 

 

 

1325.

وَعَنْ تَمِيمٍ الدَّارِيِّ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ  صلى الله عليه وسلم {اَلدِّينُ اَلنَّصِيحَةُ " ثَلَاثًا.‏ قُلْنَا: لِمَنْ يَا رَسُولَ اَللَّهِ؟ قَالَ:" لِلَّهِ وَلِكِتَابِهِ وَلِرَسُولِهِ وَلِأَئِمَّةِ اَلْمُسْلِمِينَ وَعَامَّتِهِمْ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa Tamiym Ad-Daariy[10] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Dini ni nasaha.[11] Amesema mara tatu. Tukasema: ‘kwa nani Ee Rasuli wa Allaah! Akasema: “Hiyo ni kwa ajili ya Allaah, na Kitabu Chake, Rasuli Wake, viongozi wa Waislaam na watu wote.” [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

1326.

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {أَكْثَرُ مَا يُدْخِلُ اَلْجَنَّةَ تَقْوى اَللَّهِ وَحُسْنُ اَلْخُلُقِ} أَخْرَجَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mengi yanayowaingiza watu Jannah ni kuwa na taqwa Allaah[12] na khulqa (tabia)  njema.” [Imetolewa na At-Tirmidhiy na akaisahihisha Al-Haakim]

 

 

 

1327.

وَعَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {إِنَّكُمْ لَا تَسَعُونَ اَلنَّاسَ بِأَمْوَالِكُمْ، وَلَكِنْ لِيَسَعْهُمْ بَسْطُ اَلْوَجْهِ، وَحُسْنُ اَلْخُلُقِ} أَخْرَجَهُ أَبُو يَعْلَى، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Nyinyi hamuwezi kuwatosheleza watu kwa mali zenu, lakini iwatoshe wao kutoka kwenu uchangamfu wa uso na khulqa (tabia) njema.” [Imetolewa na Abuu Ya’laa na akaisahihisha Al-Haakim]

 

 

 

1328.

وَعَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {اَلْمُؤْمِنُ مِرْآةُ اَلْمُؤْمِنِ} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ بِإِسْنَادٍ حَسَنٍ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Muumini ni kioo[13] cha ndugu yake Muumini.” [Imetolewa na Abuu Daawud kwa isnaad Hasan]

 

 

 

1329.

وَعَنِ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {اَلْمُؤْمِنُ اَلَّذِي يُخَالِطُ اَلنَّاسَ، وَيَصْبِرُ عَلَى أَذَاهُمْ خَيْرٌ مِنْ اَلَّذِي لَا يُخَالِطُ اَلنَّاسَ وَلَا يَصْبِرُ عَلَى أَذَاهُمْ} أَخْرَجَهُ اِبْنُ مَاجَهْ بِإِسْنَادٍ حَسَنٍ، وَهُوَ عِنْدَ اَلتِّرْمِذِيِّ: إِلَّا أَنَّهُ لَمْ يُسَمِّ اَلصِّحَابِيَّ

Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Muumini anayetangamana na watu na anasubiri maudhi yao, ni bora kuliko Muumini asiyetangamana na watu wala hasubiri maudhi yao.” [Imetolewa na Ibn Maajah kwa Isnaad Hasan nayo iko kwa At-Tirmidhiy lakini hakutaja Swahaba]

 

 

 

1330.

وَعَنِ اِبْنِ مَسْعُودٍ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {اَللَّهُمَّ كَمَا أَحْسَنْتَ خَلْقِي، فَحَسِّنْ خُلُقِي} رَوَاهُ أَحْمَدُ وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّان َ

Kutoka kwa Ibn Mas-‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema:

اَللَّهُمَّ كَمَا أَحْسَنْتَ خَلْقِي، فَحَسِّنْ خُلُقِي

 

“Ee Allaah! Kama Ulivyofanya umbo langu kuwa bora nitengenezee tabia yangu.” [Imetolewa na Ahmad na akaisahihisha Ibn Hibbaan]

 

[1] Majukumu matano ya kuketi njiani yametajwa hapa. Kadhalika kuna mengine yaliyotajwa kama vile kumuelekeza mpita njia na kumjibu mwenye kupiga chafya n.k. majukumu haya yanafikia kumi na nne. katika lugha ya Kiarabu غَضُّ اَلْبَصَرِ ina maana kuinamisha macho chini na kutowaangalia wanawake, na mengine yaliyoharamishwa.

 

[2] Elimu ya halaal na haraam katika Shariy’ah inaitwa Fiqh. Maelezo haya yanaonesha utukufu na ukubwa wa somo hili muhimu. Kilichoelezwa hapa ni elimu ya Qur-aan na Sunnah ya Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ), siyo mijadala ya kifalsafa yaliyopo katika masomo ya Shariy’ah leo hii, ambayo hayawezi kufahamika na akili ya mtu wa kawaida.

[3] Hadiyth hii inaonyesha kuwa kutojikweza kwa mtu na hayaa ni katika mambo yanayomsaidia na kutofanya madhambi, au kushindwa kutekeleza haki za wengine, kwa hakika hili linamfanya afikirie jina lake katika jamii lau baadhi ya madhambi yake yatadhihirika. Katika lugha nyingine, khulqa (tabia) njema na mtu kuwa na hayaa yanamfanya kutokariri mambo mabaya. Kwa hakika hayaa ni msingi wa khulqa (tabia) njema na ni sehemu katika iymaan ya mja.

[4] Pamoja na kuwa Shariy’ah za Rasuli waliyopita zimetenguliwa, suala la staha, ambalo ni moja ya taratibu zilizopita haikufutwa. Staha ni kigingi kinachomsaidia mtu katika kujizuia na kufanya mambo yoyote ayatakayo.

[5] Nini maana ya Muumini mwenye nguvu? Hii haimaanishi nguvu za kiwili wili. Badili yake inatujulisha utashi wa mtu kwa anayoyafanya katika mambo mema na kutaraji thawabu na malipo huko Aakhirah.

 

[6] Katika Hadiyth hii tunaona kuwa dhulma, kibr ni khulqa (tabia) zisizopendeza kwa mtu. Katika Hadiyth mojawapo inaelezwa kuwa dhulma ni katika mabaya zaidi ambayo mtu anaadhibiwa kwayo zaidi hapa duniani na huko Aakhirah. Hata hivyo kiini cha tatizo hili ni mtu kujikweza na kujiona.

[7] Ikiwa mtu atamsengenya mtu, anayesikia ni lazima amkataze anayesengenya, na kama inawezekana mtu aeleze mazuri yake badala ya mabaya yake.

 

[8] Huyu ni Asmaa binti wa Yaziyd bin As-Sakan Al-Ash-haliya. Alikuwa ni msemaji wa wanawake. Alishiriki katika vita vya Yarmuk na peke yake aliuwa watu tisa siku ile akiwa na upondo.

[9] Sifa tatu zilizotajwa katika Hadiyth hii zinaitwa kuwa ni ‘Misingi ya khulqa (tabia) njema’. Ambayo inafundisha usamehevu na unyenyekevu.

[10] Huyu ni Abuu Ruqaiyah, Tamiym bin Aws bin Kharija Ad-Dar. Alisilimu mwaka wa tisa Hijriyyah. Aliishi Baytul-Maqdis (Jerusalem). Ibn Siriyn anasema kuwa: “Alikusanya Qur-aan na alikuwa akiisoma kwa usiku mmoja.” Alifariki mwaka wa 40 Hijriyyah.

 

[11] Hadiyth hii ni kiini cha msingi wa Dini hii. Ni Hadiyth inayohitaji maelezo marefu, ingawaje hapa si penyewe kwa hilo. Nasaha kwa Allaah ni mtu kuwa na iymaan kwa Allaah, asimshirikishe na chochote na afuate mafundisho yake. Nasaha katika kitabu cha Allaah ni kuamini kuwa ni maneno ya Allaah, kuchukuwa kulichokatazwa na kukatazika nalo na kulifanyia kazi lililoamrishwa, kusoma kwa umakini na kufahamu maana yake na kufanya kazi. Nasaha kwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) ni kukiri Unabii wake na kufuata Sunnah zake. Ama nasaha kwa watawala Waislaam ni kuwasaidia katika yaliyo ya haki, kufuata amri zao, kuwakumbusha na mahitaji ya raia zake, kuwashauri katika wema na kuwaheshimu na kuwahamasisha kuendelea kufanya uadilifu. Na mwisho ni nasaha kwa Waislaam wote nayo ni kuwaelezea maslahi yao katika maisha yao hapa duniani na kesho Aakhirah, kuwalinda na uharibifu wowote au madhara yoyote, kuwaamrisha mema na kuwakataza maovu.

 

[12] Khulqa (tabia) njema hapa inahusisha: kutengamana na watu kwa wema, kutowafanyia ubaya, na kutabasamu kila unapokutana nao. Neno la Kiarabu تَقْوى linasimama kwa maana ya kufuata yaliyoamrishwa na kuacha yaliyokatazwa.

[13] Mtu anajifunza kuonekana kwake iwe ni uzuri au ubaya pindi anapojiangalia katika kioo. Vivyo hivyo, Muislaam ndio kioo cha Muislaam mwenzake na anatakiwa ajifunze kutoka kwa mwenzake kwa khulqa (tabia) alizonazo ili apendeze kwa Allaah na kwa watu baada ya kuondokana na khulqa yake mbaya.

 

 

Share