22-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Mlango Wa Hajj Na 'Umrah: Kunyoa Na Kupunguza Kwa Mwenye Kufanya Tamattu’u

Swahiyh Fiqh As-Sunnah

 

Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah

 

22-Kunyoa Na Kupunguza Kwa Mwenye Kufanya Tamattu’u

 

Alhidaaya.com

 

 

 

Hujaji mwenye kufanya Tamattu’u akimaliza Kusai baina ya As-Swafaa na Al-Marwah, atavua Ihraam ya (atatahalluli na) ‘Umrah yake kwa kunyoa au kupunguza. Ni bora apunguze nywele kuliko kuzinyoa, kwa kuwa atakuja kuzinyoa zote Siku ya An-Nahr (tarehe 10) baada ya kumaliza ‘amali za Hajj. Katika Hadiyth ya Jaabir, Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:

 

((حلوا من إحرامكم فطوفوا بالبيت وبين الصفا والمروة، وقصروا، وأقيموا حلالا حتى إذا كان يوم التروية فأهلوا بالحج...))

 

((Vueni Ihraam zenu, mtufu Nyumba na [msai] baina ya As-Swafaa na Al-Marwah, na punguzeni nywele, na kaeni mkiwa hamna Ihraam mpaka inapofika Siku ya At-Tarwiyah, hirimieni Hajj)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1568) na Muslim (1216)]

 

Akipunguza, anakuwa huru, na anaruhusiwa kufanya kila kitu hata kujimai mpaka Siku ya At-Tarwiyah.

 

 

 

 

Share