Skip to main content
⌂
Alhidaaya.com homepage
slogan image
  • Log in

left sidebar menu

  • Qur-aan
  • Hadiyth
  • Sunnah
  • Tawhiyd
  • Aqiydah
  • Manhaj
  • Shirki & Kufru
  • Bid-'ah (Uzushi)
  • Salaf Wa Ummah
  • Firaq-Makundi
  • Fiqh-Ibaadah
  • Duaa-Adhkaar
  • Fataawa Za Ulamaa
  • Kauli Za Salaf
  • Akhlaaq-Aadaab
  • Raqaaiq
  • Familia-Jamii
  • Maswali-Majibu
  • Chemsha Bongo
  • Vitabu
  • Mapishi

065-Atw-Twalaaq: Utangulizi Wa Suwrah

065-Atw-Twalaaq: Utangulizi Wa Suwrah

Alhidaaya.com

Imeteremka: Madiynah kwa itifaki ya ‘Ulamaa.

Idadi Za Aayah: 12

Jina La Suwrah: Atw-Twalaaq

Suwrah imeitwa Atw-Twalaaq (Talaka), na inayodalilisha ni kutajwa kwake katika Aayah namba (5).

Miongoni Mwa Makusudio Ya Suwrah:

1-Kubainisha hukmu za Talaka na kuiheshimu mipaka (sharia) yake. [Al-Mukhtaswar Fiy Tafsiyr Al-Qur-aan Al-Kariym]

2-Kubainisha hukumu zinazofungamana na talaka, na yanayoambatana juu yake; eda ya talaka, kunyonyesha, matumizi na makazi ya mtaliki na mwana.

Miongoni Mwa Maudhui Ya Suwrah:

1-Suwrah imefunguliwa kwa kuelezewa talaka ya kisharia katika kubainishwa muda unaopaswa kumtaliki mke, na amrisho la kutokuwatoa majumbani mwao, na kutokuvuka mipaka ya Sharia za Allaah.

2-Imetolewa amri ya kuwafanyia wema wataliki na kushuhudisha mashahidi katika talaka, na katika kurejea.

3-Allaah (سبحانه وتعالى) Ameahidi kuwafanyia wepesi Waumini mambo yao, na kuwaruzuku ikiwa watamcha Yeye, na watatawakali Kwake na Amewaahidi kuwafutia madhambi yao.

4-Imeendelea kubainisha baadhi ya hukmu za talaka za kuwahudumia wataliki mpaka kumaliza kunyonyesha.

5-Imetajwa mwisho mbaya wa nyumati za nyuma waliopinga Amri za Rabb wao kuwakanusha Rusuli Wake. 

6-Waumini wamekumbushwa Fadhila ya Allaah ya kuwatumia Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم), ambaye amewasomea Aayaat za Allaah zinazofafanua haki na kutenga ubatilifu, wakaongoka na wakatolewa kutoka kizani na kuingizwa katika nuru, na wakamuamini Allaah na Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم). Kisha yakatajwa malipo mazuri ya kuingizwa Jannaat na kuruzukiwa humo neema.

7-Suwrah imekhitimishwa kwa kuthibitisha Tawhiyd ya Ar-Rubuwbiyyah (Uola; Uumbaji, Uendeshaji na kadhaalika) na kubainisha Uwezo wa Allaah (سبحانه وتعالى) na upana wa Ilimu Yake.


Book traversal links for Tangulizi Za Suwrah Za Qur-aan

  • ‹ 064-At-Taghaabun: Utangulizi Wa Suwrah
  • Up
  • 066-At-Tahriym: Utangulizi Wa Suwrah ›
moon-icon

Mafunzo Katika Miezi Ya Hijri Ya Kutekeleza Na Ya Kujiepusha

  • Muharram
    image
    مُحَرَّمْ
  • Swafar
    image
    صَفَرْ
  • Rabiy’u Al-Awwal
    Rabiy’u Al-Awwal
    رَبيعُ الْأَوًّلْ
  • Rabiy'u Al-Aakhir
    Rabiy'u Al-Aakhir
    رَبيعُ الآخِرْ
  • Jumaadaa Al-Uwlaa
    image
    جُمَادَى الْأُوْلَى
  • Jumaadaa Al-Aakhirah
    image
    جُمَادَى الْآخِرَة
  • Rajab
    image
    رَجَبْ
  • Sha'baan
    Shabaan
    شَعْبَانْ
  • Ramadhwaan
    iocn
    رَمَضَانْ
  • Shawwaal
    image
    شَوّالْ
  • Dhul-Qa’dah
    image
    ذُو الْقَعْدَةْ
  • Dhul-Hijjah
    icon
    ذُو الحِجَّةْ
Alhidaaya.com homepage
  • Kuhusu Alhidaaya
  • Maoni Yako-Wasiliana Na sisi (Contact Us)
  • Tovuti Muhimu

© 2026 Alhidaaya.com All rights reserved.