14-Malaika: Lini Waliumbwa Malaika?

 

Malaika

 

Alhidaaya.com

 

14:  Lini Waliumbwa Malaika?

 

Allaah Pekee Ndiye Ajuaye wakati Alipowaumba.  Na jambo lisilo na shaka yoyote ni kwamba Malaika hawa waliumbwa kabla ya kuumbwa baba yetu Aadam (‘alayhis salaam).  Na dalili ya hili ni Kauli Yake Ta’aalaa:

 

 "وَإِذْ قَالَ رَبُّكَ لِلْمَلَائِكَةِ إِنِّي جَاعِلٌ فِي الْأَرْضِ خَلِيفَةً"

 

“Na pale Rabb wako Alipowaambia Malaika:  Hakika Mimi Nitaweka katika ardhi khalifa”.  [Al-Baqarah: 30]

 

Khalifa anayekusudiwa hapa ni Aadam (‘alayhis salaam) kwa mujibu wa kauli ya Ibn Mas-‘uwd na Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaah ‘anhumaa).

 

Hivyo basi, Malaika walikuweko kabla ya kuumbwa baba yetu Aadam (‘alayhis Salaam) kwa miaka mingi tu.  Wao walitutangulia kuwepo.

 

 

Share