27-Al-Arba’uwn An-Nawawiyyah: Wema Ni Katika Tabia Nzuri

 

Al-Arba’uwn An-Nawawiyyah:

 

Hadiyth Ya 27

 

الْبِرُّ حُسْنُ الْخُلُقِ

 

Wema Ni Katika Tabia Nzuri

 

Alhidaaya.com

 

 

 

Sikiliza Hadiyth:

 

 

عن النّوَّاسِ بْنِ سَمْعَانَ رضيَ اللهُ عَنْهُ عن النَّبي صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((الْبِرُّ حُسْنُ الْخُلُقِ، وَالإِثْمُ مَا حاكَ في نَفْسِكَ وَكَرِهْتَ أَنْ يَطَّلِعَ عَلَيْهِ النَّاسُ))  رَوَاهُ مُسْلِمٌ 

 

وعن وَابصَةَ بْنِ مَعْبَدٍ رضي اللهُ عَنْهُ قالَ: أَتَيْت رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم فَقَالَ: ((جِئْتَ تَسأَلُ عَنِ الْبِرِّ؟)). قُلْتُ: نَعَمْ. قَالَ: ((اسْتَفْتِ قَلْبَكَ، الْبِرُّ مَا اطْمَأَنَّتْ إلَيْهِ النَّفْسُ وَاطْمَأَنَّ إلَيْهِ الْقَلْبُ، وَالإِثْمُ مَا حاكَ في النَّفْسِ وَتَردَّدَ في الصَّدْرِ وَإنْ أَفْتَاكَ النّاسُ وَأَفْتَوْكَ)) حَدِيثٌ حَسَنٌ، رَوَيْنَاهُ في مُسْنَدَي الْإِمَامَيْنِ أَحْمَدَ بْنِ حَنْبَلٍ وَالدَّارِمِيّ بِإِسْنَادٍ حَسَنٍ. 

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu An-Nawaas bin Sam-‘aan (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Wema ni tabia nzuri, na dhambi ni kile kinachositasita katika nafsi yako na unachukia watu kukitambua. [Muslim]

 

Na kutoka kwa Waaswibah bin Ma’bad (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nilimwendea Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: “Je, umekuja kuuliza kuhusu wema?” Nikasema: Ndio. Akasema:  Ushauri  moyo wako. Wema ni kile ambacho nafsi yako inatumainika kwacho na moyo wako pia unatumainika. Na dhambi ni kile kinachositasita katika nafsi na kifua kinataradadi japokuwa watu wamekariri kukupa shauri lao la kishariy'ah (kukipendelea).” [Hadiyth Hasan, imenukuliwa katika Musnad za Imaam wawili Ahmad bin Hanbal na Ad-Daarimiyy kwa isnaad Hasan]  

 

 

 

 

Share