06-Uswuul Al-Fiqhi: Asili Na Maendeleo Ya Uswuul Al-Fiqh

 

Sio rahisi kulisoma somo la Uswuul al-Fiqh na maendeleo yake bila ya kupitia kumbukumbu za Fiqhi. Mafundisho ya vitendo kwa Shariah ambazo yamekusanywa kusanywa kutokana na vyanzo mahsusi vya sheria.

 

Kubuni maana ya Uswuul  ni: shina, au asili Aswl, wingi Uswuul au kile chengine ambacho kinajengwa juu yake. Kwa mfumo wa kisheria za Kiislamu (ndipo) Fiqhi inapojengwa hapo, na mizizi kutoka kwenye mashina ya Uswuul  ambayo yanakuwa na chanzo chake cha ushahidi. Matokeo yake, ili kufahamu asili ya Uswuul al-Fiqh, tunahitaji kuwa na uoni wa jumla juu ya historia ya Sheria za Kiislamu. Tashri’iy

 

Kuanzisha vifungu vya Shariah, kuamuru sheria kufuatwa, kuweka kanuni na amri, na kufafanua miundo ni kazi ambayo ni maalumu kwa Allaah pekee. Yeyote anayejipa na kuandikia kazi hizi zaidi ya Allaah, ametenda dhambi ya Shirk. Kwani, kufanya hivyo amekwenda kinyume kabisa na imani ya Upweke wa Allaah. Tawhiyd.

 

Allaah Ameweka na kugawa thibati na vyanzo vilizo wazi za ushahidi kwa ajili ya kwamba; waumini wasiwe na matatizo kutafuta muongozo wao kwenda kwenye vipengele vya Sheria Zake. Au Ahkaam kwa kutumia baadhi ya vyanzo hivi vya ushahidi. Ummah wa Kiislamu umekubaliana juu ya usahihi na uhusiano wake kwa Ahkaam, na wameukubali hivyo hivyo. Hata hivyo, kuna tofauti nyingi kwa mnasaba wa vyanzo vyengine vya ushahidi.

 

Vyanzo vya ushahidi ambavyo Ummah wote wamekubali, na juu ya usahihi wa ambao kuna makubaliano ya jumla, inajumuisha vyanzo viwili, ambavyo vinafanya msingi wa sheria kipindi cha Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) Vyanzo hivi viwili vya sheria ni:

 

1)    Qur-aan: Hii inaweza kutafsiriwa kama ni maneno yaliyoteremshwa kwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Kuisoma pekee ni miongoni mwa tendo la ibada, Surah fupi ambayo ni changamoto kwa binaadamu kutoa chochote chenye kufanana nayo. Kila herufi ambayo imefikishwa kwetu ni kupitia kwa waandishi madhubuti wasio na pingamizi Tawaatur ambayo imeandikwa baina ya magamba mawili ya Kitabu Kitakatifu Msahafu kuanzia na Surat al-Faatihah “Sura ya ufunguzi” na kumalizia kwa Surat an-Naas.

2)    Sunnah: Inajumuisha kila kitu, nje ya Qur-aan. Ambayo imefikishwa kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), alilolisema, kutenda au kukubaliana nalo.

 

Hivyo, kila tamko la Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), zaidi ya Qur-aan, na kila kitendo chake. Kuanzia mwanzo wa kazi yake mpaka mwisho wa siku zake, zinahusisha Sunnah yake. Kwa maneno ya jumla kila neno aidha linaanzisha uamuzi ambao unatumika kwa wafuasi wa Ummah wote, au uamuzi ambao unamhusisha Mtume mwenyewe peke yake au kwa Swahaaba zake wengine.

 

Bila ya kuangalia kama alivyofanya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ni tabia nzuri au vyenginevyo, kila neno lake, tabia na idhini. Inaweza kuchukuliwa kama ni chanzo cha ushahidi kwenye uamuzi wa kisheria. Hivi ndivyo ilivyo, bila ya kuangalia kwamba lafudhi zake au vitendo vina mnasaba wa dini au mwenendo. Au ama zimejihusisha na kutoa amri au kutoa maoni, kuzuia, kukataa, au kukubali. Na bila ya kuangalia ikiwa ama lafudhi zake au kitendo, kiliegemezwa kwenye uamuzi uliotolewa kabla kwenye Qur-aan, au ama inasimama kufanya kazi pekee (bila ya tegemezi) kuanzisha sheria.

 

Kipindi cha maisha ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), maamuzi yote ya kisheria Ahkaam za Shariah, ukiunganisha na migawanyo yote, kama vile maamuzi makuu au yaliyopokelewa, elimu juu ya misingi ya imani, na mwenendo wa kanuni kuhusiana na matendo maalum na usahihi wake, yalitolewa kutokana na vyanzo viwili vya Qur-aan na Sunnah.

 

3)    Ijtihaad: Ilikuwa ikifanyiwa kazi na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na wale Maswahaba zake ikiwa na mwelekeo wa kisheria ujulikanao kama Ahl an-Nadhwar. Ijtihaad ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ilithibitishwa na Qur-aan na mara nyengine haithibitishwi. Ambapo kwa kesi hiyo, ilielezwa kwamba suluhisho lililo bora ni lile ambalo hakulifanyia kazi.

 

Ijtihaad iliyofanywa na Maswahaba, daima ilikuwa ni kujibu mazingira ambayo yametokea kwao. Baadaye, walipokutana na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), wataeleza kilichotokezea na kumwambia walichotolea uamuzi. Mara nyengine, yeye (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) anazikubali Ijtihaad zao, na uamuzi kama huo wa kwao (uliopata ruhusa ya Mtume) ulifanya sehemu ya Sunnah. Kama yeye Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) atazikataa Ijtihaad zao. Maelezo yake kuhusiana na mwenendo sahihi utakuwa ni Sunnah.

 

Hivyo, tunaweza kusema kwamba; kwa hatua hiyo sheria ilitegemea kwenye mifumo miwili ya Uteremsho Mtukufu. Wahyi:

 

  1. Uteremsho uliosomwa, Wahy Matlu, au Qur-aan yenye ukamilifu isiyoigika I’jaaz.

  2. Uteremsho usiosomwa. Wahy Ghayr Matlu, au Sunnah za Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).

 

Hakika, Ijtihaad iliyofanywa na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) itakuwa ni yenye kufuatwa (precedent) kwa Swahaaba zake na baadaye Waislamu. Ambazo kwa uwazi inathibitisha uhalali wa Ijtihaad, ili kwamba pale watakaposhindwa kupata uamuzi ulioamuliwa kwa kisheria ndani ya Qur-aan au Sunnah, walihitajika kufanya kazi ya Ijtihaad ili kufikia kwenye hukumu peke yao.

 

Juu ya hivyo, labda ili kuipa nguvu na kuianzisha dhana hii, Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiwaamrisha baadhi ya Maswahaba zake kufanya Ijtihaad kuhusiana na mambo fulani akiwepo yeye mwenyewe. Kisha atawaambia nani alikuwa sahihi na nani alikosea.

 

 

Share