17-Al-Lajnah Ad-Daaimah: Kugawa Zakaatul-Fitwr Kwa Wanaoomba Njiani Japokuwa Hawastahiki

Kugawa Zakaatul-Fitwr Kwa Wanaoomba Njiani Japokuwa Hawastahiki

 

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

 

SWALI: 

 

Watu wanaomba Zakaatul-Fitwr njiani na hatujui kama ni wenye dini au watu waovu. Wengineo hali zao ni za kuridhisha, chochote wapatacho kutokana na Zakaatul-Fitwr huwatumilia kwa watoto wao. Wengine wanapokea mishahara lakini ni dhaifu katika msimamo wa dini. Je inaruhusiwa kuwapa Zakaatul-Fitwr au haifai?

 

JIBU

 

Zakaatul-Fitwr itolewe kwa Waislamu masikini japokuwa ni wenye kutenda madhambi madamu tu madhambi yao hayawatoi nje ya Uislamu. Iliyomaanishwa kuhusu masikini ni wale wanaoonekana kuwa ni masikini, hata kama ukweli ni matajri. Anayetoa Zakaatul-Fitwr atafute watu masikini wanaostahiki kwa kadiri awezavyo. Akijua baadaye kwamba aliyepokea ni tajiri, haitoathiri kwa aliyetoa bali amefanya wajibu wake.  

 

 

 Wa biLLaahi At-Tawfiyq wa Swalla Allaahu ‘alaa Nabiyyina Muhammad wa aalihi wa Swahbihi wa sallam.

 

 

[Fataawaa Al-Lajnah Ad-Daaimah]

 

 

 

Share