Vipopoo/Matobosho

Vipopoo/Matobosho

Vipimo

 

Unga ngano - 2 na nusu kikombe

Maji - 3 kikombe

Chumvi - kijiko nusu cha chai

Mafuta - 5 kijiko cha supu

Tui la nazi la kopo - 1000 ml

Iliki  iliyosagwa - 1 kijiko cha chai

Sukari - Kikombe nusu

 

Namna Ya Kutayarisha Na kupika

 

  1. Chemsha maji paka yatokote na hiyo chumvi
  2. Yakitokota  mimina unga uache ndani kwa dakika tano.
  3. Songa kama ugali kwa kutumia nguvu zako na kukazanisha sufuria sawa sawa kwani ugali wake huwa mgumu si kama ugali wa kawaida.
  4. Ukishakuwa ugali mimina kwenye kibao au meza au sinia pana kisha ukande kidogo ukiwa umejipaka mafuta mikononi.
  5. Menya vijidonge usukume kwa mkono moja paka iwe bakora ndefu ima  iwe nzito au nyembamba bila kutia mafuta wala unga mkavu.
  6. Uwanie kuufanya hizo bakora paka umalize bila kukauka .
  7. Zikatekate bakora kwa kisu vipande vipande ukubwa wa nusu inchi au inchi moja kama ilivyo kwenye picha.

 

  1. Kila kipande chovya mafuta kwa kidole  ukibonyeza kati ili kujenga kiduwara.
  2. Tia tui nusu kwenye sufuria ya nafasi na iliki uzichemshe mpaka zitokote   
  3. Mimina vitobosha vyote kweye mchemko wa tui na iliki .
  4. Moto mdomdogo ongeza tui lilobakia acha kwa daikika 30 kutokota.
  5. Tia sukari huku unakoroga koroga kuchanganya matobosha  na tui.
  6. Yakitokota  yakiwa mazito yaepue usiyaache yakakauka tui lote na uonje sukuari, ikiwa imetokeza utamu tayari kuliwa lakini mpaka yapowe ndio huwa mazuri zaidi.

 

Kidokezo:

Kwa wenye friji wanaweza kugawa matobosha kabla kuyapika kwa siku ya pili au ya tatu ikiwa umeyatia ndani ya mifuko ya plastiki maalum ya kuwekea vitu frijini.  Lakini siku utakayodhamiria kupika basi paka uyapashe moto kwenye  (microwavel) kwa sekunde 60 ili yalainike kwa kupikwa.

 

 

Share