34-Hadiyth Al-Qudsiy: Mwenye Kupenda Kukutana Na Allaah Na Anayechukia Kukutana Naye

Hadiyth Al-Qudsiy

Hadiyth Ya 34

Mwenye Kupenda Kukutana Na Allaah Na Anayechukia Kukutana Naye   

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:  ((قَالَ اللَّهُ إِذَا أَحَبَّ عَبْدِي لِقَائِي أَحْبَبْتُ لِقَاءَهُ وَإِذَا كَرِهَ لِقَائِي كَرِهْتُ لِقَاءَهُ)) البخاري و مالك

 Imepokelewa kutoka kwa Abua Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Allaah Amesema: Mja wangu akipenda kukutana na Mimi, Nami Hupenda kukutana naye; na akikirihika (akichukia) kukutana na Mimi, basi nami Hukirihika kukutana naye)) [Al-Bukhaariy na Maalik]

Share