Hariys - Bokoboko La Kuku

Hariys - Bokoboko La Kuku

   

 

Vipimo

Ngano nzima  (shayiri) - 3 Vikombe

Kuku - ½  (3 LB takriban)

Thomu na tangawizi iliyosagwa - 1 kijko cha supu

Pilipili manga ya unga - ½  kijiko cha chai

Jiyrah (cumin/bizari ya pilau) - ½ kijiko cha chai

Chumvi - kiasi

Kidonge cha supu - 1

Samli ya moto - ½  kikombe

 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

  1. Roweka ngano (shayiri) tokea usiku au muda wa masaa.
  2. Katakata kuku mtie katika sufuria, tia maji kiasi viungo vyote. Mchemeshe awive na ibakie supu yake.
  3. Toa kuku, toa mifupa na umchambue chambue vipande vidogo vidogo.
  4. Chemisha ngano (shayiri)  kwa kufunika sufuria hadi iwive na kukauka maji.
  5. Tia supu ya kuku katika ngano (shayiri), na kuku uliyemechambua. Tia kidonge cha supu. 
  6. Tia samli nusu (bakisha nusu) kisha songa mchanganyiko uchanganye hadi ivurugike kuku na ngano (shayiri) vizuri.
  7. Mimina katika sahani, mwagia samli imoto ilyobakia likiwa tayari.

Kidokezo:

Ukipenda kulia na sukari

 

 

 

Share