029-Sifa Ya Swalah Ya Mtume (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam): Kisomo Chake (صلى الله عليه وآله وسلم) Katika Swalah Za 'Iyd Mbili - Sifa Ya Swalah Ya Mtume

 

9-   SWALAH ZA 'IYD MBILI

 

"Alikuwa   (صلى الله عليه وآله وسلم)akisoma (mara nyingine) katika Rakaa ya kwanza

 

سَبِّحِ اسْمَ رَبِّكَ الْأَعْلَى

 

((Litakase jina la Mola wako Aliye juu kabisa)) [Al-A'laa 87: 19], na katika Rakaa ya pili:

 

هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ الْغَاشِيَةِ

 

((Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?)) [88: 26] [1].  Na mara nyingine "alikuwa akisoma katika hizo Rakaa mbili:

 

ق وَالْقُرْآنِ الْمَجِيدِ

 

((Qaaf, Naapa kwa Qur-aan Tukufu))[Qaaf 50: 45], na

 

اقْتَرَبَتِ السَّاعَةُ وَانشَقَّ الْقَمَرُ

 

((Saa imekaribia na mwezi umepasuka)) [Al-Qamar 54: 55][2].

 

 

 


[1]  Muslim na Abu Daawuud.

[2]  Muslim na Abu Daawuud.

Share