Skip to main content
⌂
Alhidaaya.com homepage
slogan image
  • Log in

left sidebar menu

  • Qur-aan
  • Hadiyth
  • Sunnah
  • Tawhiyd
  • Aqiydah
  • Manhaj
  • Shirki & Kufru
  • Bid-'ah (Uzushi)
  • Salaf Wa Ummah
  • Firaq-Makundi
  • Fiqh-Ibaadah
  • Duaa-Adhkaar
  • Fataawa Za Ulamaa
  • Kauli Za Salaf
  • Akhlaaq-Aadaab
  • Raqaaiq
  • Familia-Jamii
  • Maswali-Majibu
  • Chemsha Bongo
  • Vitabu
  • Mapishi

006-Unawezaje Kuupata Moyo Wa Mumeo Na Kumridhisha Mola Wako: Lawama Nyingi Hukausha Nyoyo

LAWAMA NYINGI HUKAUSHA NYOYO

Lawama zako zisiwe katika dogo na kubwa, jifunze namna bora ya kusamehe na kukubali mambo mengine bila ya kushindana, kwa hakika maisha ya ndoa huhitajia sana wanandoa kusameheana kuliko jambo lolote lingine.

‘Abdullaah bin Ja’afar bin Abi Twaalib alimuusia mwanawe wa kike alipokuwa anaolewa kwa kumwambia,

“Jihadhari na wivu kwani ni ufunguo wa talaka, na jihadhari na lawama nyingi kwani hurithisha maudhi, jilazimishe na kupaka wanja kwa kuwa ni bora na jambo lililo bora zaidi ya manukato ni maji”

Kutoka kwa Anas bin Maalik (Radhiya Allaahu ‘anhu) naye kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema,

“Je, niwaambieni kuhusu wake zenu peponi? Tukajibu: Ndio ewe Mtume wa Allaah, akasema, Ni wenye upendo na wenye kizazi, atakapoghadhibika au kukosewa, au atakapokasirika mume wake, atasema, “Mkono wangu huu uko juu ya mkono wako, sipaki wanja ukiwa na hasira na macho yangu hayatoona usingizi hadi uridhike”[1]

Acha kiburi ewe mke Muumini, na uende kwa mumeo atakapoghadhibika na umridhishe kwani atakupa hadhi na atanyanyua shani yako katika moyo wake na lililo muhimu sana katika yote ni kuwa baada ya hayo utakuwa umepata radhi za Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala) kwani radhi za mume ni katika radhi za Allaah (Subhaanahu wa Taala), katika Hadiyth tunasoma, “Mwanamke atakayekufa na mumewe akiwa radhi nae ataingia peponi”

Katika Wasia wa Asmaa bint Khaarijah Kwa Mwanae Wakati wa Ndoa Yake:

“Kuwa kwake mume wako ni ardhi, naye atakuwa kwako mbingu, na uwe kwake tandiko atakuwa kwako nguzo, wala using’ang’anie kitu akakuchukia na usiwe mbali nae akakusahau, na akikusogelea msogelee zaidi”



[1] At-Twabaraaniy


Book traversal links for Unawezaje Kuupata Moyo Wa Mumeo Na Kumridhisha Mola Wako

  • ‹ 005-Unawezaje Kuupata Moyo Wa Mumeo Na Kumridhisha Mola Wako: Mapokezi Mazuri Huingiza Furaha Moyoni
  • Up
  • 007-Unawezaje Kuupata Moyo Wa Mumeo Na Kumridhisha Mola Wako: Je, Tumbo Ni Njia Ya Kuelekea Kwenye Nyoyo ›
moon-icon

Mafunzo Katika Miezi Ya Hijri Ya Kutekeleza Na Ya Kujiepusha

  • Muharram
    image
    مُحَرَّمْ
  • Swafar
    image
    صَفَرْ
  • Rabiy’u Al-Awwal
    Rabiy’u Al-Awwal
    رَبيعُ الْأَوًّلْ
  • Rabiy'u Al-Aakhir
    Rabiy'u Al-Aakhir
    رَبيعُ الآخِرْ
  • Jumaadaa Al-Uwlaa
    image
    جُمَادَى الْأُوْلَى
  • Jumaadaa Al-Aakhirah
    image
    جُمَادَى الْآخِرَة
  • Rajab
    image
    رَجَبْ
  • Sha'baan
    Shabaan
    شَعْبَانْ
  • Ramadhwaan
    iocn
    رَمَضَانْ
  • Shawwaal
    image
    شَوّالْ
  • Dhul-Qa’dah
    image
    ذُو الْقَعْدَةْ
  • Dhul-Hijjah
    icon
    ذُو الحِجَّةْ
Alhidaaya.com homepage
  • Kuhusu Alhidaaya
  • Maoni Yako-Wasiliana Na sisi (Contact Us)
  • Tovuti Muhimu

© 2026 Alhidaaya.com All rights reserved.