007-Unawezaje Kuupata Moyo Wa Mumeo Na Kumridhisha Mola Wako: Je, Tumbo Ni Njia Ya Kuelekea Kwenye Nyoyo

 

JE, TUMBO NI NJIA YA KUELEKEA KWENYE NYOYO?

 

Bila shaka kuwa njaa huzusha mapungufu katika mwili wa mwanaadamu na huathiri hata namna ya kufikiri kwake, huenda akapata dhiki au wakati mwengine furaha, katika hali kama hizo nafsi ikipata inachokitamani na kukipenda miongoni mwa aina za vyakula hufurahi na kwa hiyo humpenda aliyekitengeneza chakula kile.

 

Katika wasia wa Umaamah binti Al-Haarith kwa mwanawe wakati wa ndoa yake:

“Angalia kwa makini wakati wa kula na kulala kwake: kwa hakika njaa nyingi huchoma na kukosesha usingizi na hutia ghadhabu”

 

Kwa hakika mwanamke mwenye kujali wakati wa chakula cha mumewe na akajitahidi kuandaa chakula kizuri zaidi kwa kadiri ya uwezo wake ndie mtu wa karibu zaidi kuupata moyo wa mume wake na heshima yake. Sikusudii wala sipendelei kusema kuwa mwanamke apoteze masaa mengi katika kuandaa chakula, bali apike kile anachokipenda mume wake bila ya kuharibu majukumu yake mengine. 

 

Pindi anaporudi mumewe kutoka kazini na wakati huo huo njaa inamuunguza anakuta chakula kilishaandaliwa na nyumba ni safi na mkewe anamsubiri ili ashirikiane naye chakula, kwa hakika katika hali kama hii ni juu ya Mwenyezi Mungu kuwabarikiri katika mazingira haya mazuri ya kiimani na hii ndio familia iliyobarikiwa.

 

 

Share