Muislamu Kuingia Kanisani Inafaa?

 

SWALI:

 

Shukurani zote zina mustahiki Allah subhanahu wataalla! 

Swali langu   nikuhusu muislam kuingiya kanisani, nasi kama anapenda ila hulazimusha na mahala anapo fanya kazi kwakushindikiza awo wasiye jiweza kwa sababu ana pasha kuwalisha. Na ayo mambo yote niliyo yauliza ninalazimika kuyafanya katika programme ya shule niliyo ichanguwa, ambayo niya u nurse, na mimi napenda sana kusomeya iyo kazi, ila tatizo ni hiyo. Tashukuru sana mukinisahidiya. Ahsante, Maasalam


 

JIBU:

 

Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

Shukrani zetu kwa swali lako kuhusu kuingia katika Kanisa.

Hakika Uislamu haujamkataza Muislamu kuingia katika Kanisa ikiwa kuna udhuru wa kufanya hivyo. Ikiwa ni kujua wanayofanya Wakristo ili uwe na maalumati ya moja kwa moja kuhusiana na ‘Ibaadah zao au kwa shughuli nyingine kama msaada wa Waislamu kuwasaidia masikini waliokumbwa na misukosuko na wakapata hifadhi katika Kanisa.

Hata hivyo, si vyema kwa Muislamu kuingia katika chuo chochote kile kama ni cha unesi au chengineko kukawa na utaratibu wa programu wa chuo kwa wanafunzi kulazimishwa kuingia huko. Kufanya hivyo vyuo hivyo ni kwa malengo ya kuwavuta Waislamu na kuwatoa katika Dini yao. Hivyo, ni vyema kwako kutafuta chuo ambacho haitakuwa na ulazima huo wa kuingia makanisani.

 

Tunaamini kuna vyuo vingi Ulaya ambavyo havina mambo ambayo umeyataja hayo kwa sharti la kuwa nesi. Hatujui vyuo vyote vinginevyo umeviacha na kuingia hicho chenye masharti kama hayo kwanini?

Hivyo tunakushauri ndugu yetu, uepukane na mambo ya haraam na mashaka mashaka katika Dini yako na utafute yale yenye usalama na Dini yako na kupata radhi za Allaah ambalo ndilo lengo kuu la kuwepo kwako hapa ulimwenguni.

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

 

Share