Mashaytwaan Wanaweza Kusababisha Kubadilisha Vipimo Vya Damu?

 

Mashaytwaan Wanaweza Kusababisha Kubadilisha Vipimo Vya Damu?

 

Alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Assalam Aleykum.

Mimi napeda kupata ufafanuzi wa juu ya swali lifuatalo.

Je Mashetani yanapokuwa ndani ya mwili wa binadamu yanaweza kusababisha vipimo (vya hospital) kama vya kifua, choo au damu (yaani vipimo vionyeshe kuwa mtu ana ukimwi wakati hana? Na pia kumsababishia mtoto kuwa mgonjwa mara kwa mara?

Alhamdulilah, Nitazidi kushukuru sana kwa majibu yatakayo tolewa pamoja na ushauri wa nini cha kufanya endapo upo kwenye Mtihani huo.

 

JIBU:

 

AlhamduliLLaah - Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Rabb wa walimwengu, Swalaah na Salaam zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho

 

 

Hakika ni kuwa kwa uwezo aliopatiwa shaytwaan na Allaah Aliyetukuka ni kuwa shaytwaan anaweza kufanya hivyo kwa kubadilisha yaliyomo ndani ya mwanaadamu.

Hata hivyo, shaytwaan hawezi kubadilisha chochote au kuleta athari yoyote katika mwili wa mwanaadamu ila kwa idhini yake Allaah Aliyetukuka.

 

Kwa minajili hiyo, Allaah Aliyetukuka Anatuelezea:

 

فَيَتَعَلَّمُونَ مِنْهُمَا مَا يُفَرِّقُونَ بِهِ بَيْنَ الْمَرْءِ وَزَوْجِهِ ۚ وَمَا هُم بِضَارِّينَ بِهِ مِنْ أَحَدٍ إِلَّا بِإِذْنِ اللَّـهِ ۚ وَيَتَعَلَّمُونَ مَا يَضُرُّهُمْ وَلَا يَنفَعُهُمْ ۚ وَلَقَدْ عَلِمُوا لَمَنِ اشْتَرَاهُ مَا لَهُ فِي الْآخِرَةِ مِنْ خَلَاقٍ ۚ وَلَبِئْسَ مَا شَرَوْا بِهِ أَنفُسَهُمْ ۚ لَوْ كَانُوا يَعْلَمُونَ ﴿١٠٢﴾

Nao wawili hawamfundishi yeyote mpaka waseme: Hakika sisi ni mtihani, basi usikufuru. Kisha wakajifunza kutoka kwa hao wawili yenye kupelekea kufarikisha kwayo baina ya mtu na mkewe. Na wao hawawezi kamwe kumdhuru yeyote kwayo isipokuwa kwa idhini ya Allaah; na wanajifunza yanayowadhuru na wala hayawanufaishi; na kwa yakini walijua kwamba atakayechuma haya hatopata katika Aakhirah fungu lolote, na ni ubaya ulioje walichojiuzia nafsi zao, lau wangelikuwa wanajua. [Al-Baqarah: 102].

 

Ikiwa mtu amesibiwa na shaytwaan itabidi apatiwe kinga kwa kusomewa na Muislamu mwenye Imani na ujuzi wa kisomo cha Ruqyah ili atolewe ndani ya mwili. Na baada ya hapo inabidi mtu mwenyewe awe atajilinda kwa kusoma Aayah, Suwrah na adhkaar ambazo zitampatia kinga hiyo.

 

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

Share