05-Madhara Ya Ghiybah: Kuharamisihwa Kwake Na Na Adhabu Zake Katika Sunnah

Madhara Ya Ghiybah (Kusengenya) Na An-Namiymah (Kufitinisha)

 

05- Kuharamisihwa Kwake Na Na Adhabu Zake Katika Sunnah

 

 

 

Makatazo na uharaam wa Ghiybah na adhabu zake katika Sunnah ni kama ifuatavyo: 

 

 

 عن أبي بكرة رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال في خطبته يوم النحر بمنى في حجة الوداع: ((إنَّ دِمَاءَكُمْ وَأَمْوَالَكُمْ وَأَعْرَاضَكُمْ حَرَامٌ عَلَيْكُمْ كَحُرْمَةِ يَوْمِكُمْ هَذَا فِي شَهْرِكُمْ هَذَا فِي بَلَدِكُمْ، أَلا بَلَّغْتُ؟ )) متفق عليه

Kutoka kwa Abuu Bakrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesimulia  kuwa Rasuli wa Allaah  (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisema katika khutba yake ya siku ya An-Nahr [siku ya kuchinja] huko Minaa katika  Hijjah ya kuaga: ((Hakika damu zenu, mali zenu na heshima zenu ni haraam kwenu kama uharamu (wa kutenda dhambi) siku yenu hii katika mji wenu huu. Je nimefikisha?)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth hii imedhihirisha uharaam wa ghiybah yakiwemo makatazo na uharaam wa kuvunjiana heshima na kwamba ni sawa na kutenda dhambi mji mtukufu na siku tukufu hiyo ya Yawmun-Nahr (siku ya kuchinja).  

 

 

Haifai kumteta mtu hata ikiwa mtu huyo ana sifa mbaya unayoitaja madamu unaitaja nyuma yake basi huwa ni ghiybah kama  alivyosema Rasuli wa Allaah  (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Basi seuze iwe ni kumsengenya mtu kwa aibu asiyokuwa nayo au kumtolea aibu zake, au kumzulia kwa mabaya asiyokuwa nayo? Imeharamishwa katika Hadiyth ifuatayo:  

 

 

عن عَائِشَةَ رضي الله عنها قَالَتْ: قُلْتُ لِلنَّبِي صلى الله عليه وسلم: حَسْبُكَ مِنْ صَفِيَّةَ كَذَا وَكَذَا. فَقَالَ: ((لَقَدْ قُلْتِ كَلِمَةً لَوْ مُزِجَتْ بِمَاءِ الْبَحْرِ لَمَزَجَتْهُ)). قَالَتْ: وَحَكَيْتُ لَهُ إِنْسَانًا، فَقَالَ: ((مَا أُحِبُّ أَنِّى حَكَيْتُ إِنْسَانًا وَأَنَّ لِي كَذَا وَكَذَا))  رواه أبو داود   والترمذي   وقال: حديث حسن صحيح.

 

Kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesimulia: Nilimwambia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Achana na Swafiyyah; yuko kadhaa na kadhaa."  yaani ni mfupi – Rasuli wa Allaah  (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: ((Hakika umetamka neno ambalo lau lingalichanganywa na maji ya bahari yangelibadilika)) (kutokana na uvundo wa neno hilo). 'Aaishah alisema: "Siku moja nilimuigiza mtu mbele yake Rasuli wa Allaah  (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaniambia: ((Mimi sipendi kumuiga mtu na ilhali mimi nina kadhaa na kadhaa)) [Abu Daawuud na At-Tirmidhiy na amesema Hadiyth hii ni Hasan Swahiyh] 

 

 

Dini yetu ya Kiislam imesisitiza sana kutunziana heshima na kuhifadhiana mabaya yetu kama ilivyothibiti katika Hadiyth ifuatayo:

 

 

 عن عبد اللَّه بن عَمْرو بن الْعاص رضي اللَّه عنهما عن النَّبِيِّ صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم قال  : ((الْمُسْلِمُ مَنْ سَلِمَ الْمُسْلِمُونَ مِنْ لِسانِهِ ويَدِهِ، والْمُهَاجِرُ مَنْ هَجَرَ ما نَهَى اللَّه عَنْهُ)) متفق عليه

Kutoka kwa 'Abdullaahi bin 'Amru bin Al-'Aasw (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) ambaye amesema: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Muislam ni yule wanaosalimika Waislam kwa ulimi wake na mkono wake, na Muhaajir (mwenye kuhama) ni yule anayehama yale Aliyoyakataza Allaah)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Umuhimu wa kuhifadhi ulimi ili usimuingize mtu motoni:

 

عن معاذِ بن جبلٍ رضي الله عنه قال: قلت: يا رسول الله، أخْبِرني بِعَمَلٍ يُدْخِلُني الجنَةَ ويُبَاعِدُني عَنِ النارِ. قال: ((لَقَدْ سألْتَ عَنْ عَظيمٍ، وإنَهُ لَيَسيرٌ عَلى من يَسَّرَهُ اللهُ تعالى عَلَيْهِ : تَعْبُدُ اللهَ لا تُشْرِكُ بِهِ شَيئاً، وتُقيمُ الصَّلاةَ  ،وتُؤتي الزكاةَ، وتصومُ رمضانَ، وتَحُجُّ البيتَ)) ثم قال: (( ألا أَدُلُّكَ على أبْوَابِ الخيرِ؟: الصَّومُ جُنَّةٌ، والصَّدقةُ تُطْفِىءُ الخَطِيئةَ كما يُطْفىءُ الماءُ النارَ، وصَلاةَ الرَّجُلِ في جَوْفِ الَّليْلِ، ثم تلا: ((تَتَجَافَى جُنُوبُهُمْ عَنْ الْمَضَاجِعِ)) - حتى بلغ – ((يَعْمَلُونَ))  السجدة: 16-17 .

ثم قال:  ((ألا أُخْبِرُكَ بِرَأسِ الأمْرِ وَعَمودِهِ وَذِرْوَةِ سَنَامِهِ؟)) قلتُ: بَلىَ يا رسول الله. قال:  (( رَأْسُ الأمْرِ الإسلامُ، وعَمُودُهُ الصَّلاةُ، وَذِرْوَةُ سَنَامِهِ الجِهادُ )).ثم قال: ((ألا أخْبِرُكَ بِمِلاكَ ذَلِكَ  كلِّهِ ؟)) فَقُلْتُ بَلَى يا رَسول الله، فأخَذَ بِلِسانِهِ وقال:  ((كُفَّ عَلَيْكَ هذا)) . قلت: يا نبيَّ الله، وإنَّا لمؤاخَذُونَ بِما نَتَكَلَّمُ بِه؟)) فقال: (( ثَكِلَتْكَ أمُّكَ يَا مُعَاذُ،  وَهَلْ يَكُبُّ الناسَ في النارِ على وُجُوهِهِمْ ))  أو قال: ((على مناخِرِهِم - إلاَّ حَصَائدُ  ألسِنَتهم)) رَوَاهُ التِّرْمِذِيُّ   وَقَالَ: حَدِيثٌ حَسَنٌ صَحِيحٌ. 

Kutoka kwa Mu'aadh bin Jabal (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nilisema: Ee Rasuli wa Allaah! Niambie kitendo ambacho kitanipeleka Jannah na kitaniokoa na moto.  Akasema: ((Umeniuliza jambo kubwa lakini ni rahisi kwa yule ambaye Allaah Ta’aalaa Amemsahilishia.  Muabudu Allaah wala usimshirikishe na chochote, Swali, toa Zakaah, funga Ramadhwaan, nenda kuhiji (Makka). Kisha akasema: ((Je? Nikuonyeshe  milango ya kheri?  Swawm ni ngao, Swadaqah inazima dhambi kama vile maji yanavyozima moto, na kuswali katikati ya usiku: Kisha akasoma  ((Mbavu zao zinatengana na vitanda ….)) hadi ilipomalizikia Aayah ((…waliyokuwa wakiyatenda)) [As-Sajdah: 16 na 17]  

 

Tena akasema: ((Je, nikwambie kilele cha hilo jambo; nguzo yake na sehemu yake ya juu kabisa?)) Nikasema: Ndio ee Rasuli wa Allaah. Akasema: ((Kilele chake ni Uislaam, nguzo yake ni Swalaah na sehemu yake ya juu kabisa ni jihaad))  Kisha akasema: ((Je, nikwambie muhimili wa yote haya?)) Nikasema: Ndio ee Rasuli wa Allaah. Akaukamata ulimi wake na akasema; ((Uzuie huu)) Nikasema: Ee Nabiy wa Allaah,  yale tunayoyasema tutahukumiwa  kwayo? Akasema:  ((Mama yako akuhurumie ee Mu'aadh!  Kuna kitu zaidi kinachowaangusha watu kifudifudi motoni kama si mavuno ya ndimi zao?)) [Imesimuliwa na At-Tirmidhiy na ni Hadiyth Hasan]

 

 

Baadhi ya hizo adhabu za Aakhirah alikwishaziona Rasuli wa Allaah  (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipokwenda Israa wal Mi'raaj kama ilivyotajwa  katika Hadiyth ifuatayo:

 

 

عن أنس قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم: ((لما عُرِجَ بي مررتُ بقومٍ لهم أظفارٌ من نُحاسٍ يخْمِشون وجوهَهم وصدورَهم، فقلتُ: من هؤلاء يا جبريلُ ؟)) قال: هؤلاء الذين يأكلون لحومِ الناسِ ، ويقعون في أعراضِهم.

 

Kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Rasuli wa Allaah  (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Nilipopandishwa mbinguni (Siku ya Israa na Mi’raaj) nilipita kwa watu ambao walikuwa wana kucha za shaba nyeupe wakijichana nyuso zao na vifua vyao. Nikauliza: Nani hawa ewe Jibriyl?)) Akasema: Hawa ni watu ambao wamekula nyama za binaadamu na kuwavunjia heshima zao. [Abuu Daawuwd, Swahiyh Abiy Daawuwd (4878)]

 

 

 

Share