Skip to main content

Mukhtasari Wa 'Aqiydah Ya Muislamu: Maswali Na Majibu11-Mukhtasari Aqiydah Ya Muislamu: Je, Allaah Yuko na sisi kwa dhati Yake au kwa ujuzi Wake?

 Mukhtasari Wa ‘Aqiydah Ya Muislamu

Maswali Na Majibu Pamoja Na Dalili Kutoka Qur-aan Na Sunnah.

Imetarjumiwa na: Alhidaaya.com

11-Je, Allaah Yuko na sisi kwa dhati Yake au kwa ujuzi Wake?

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Yuko na sisi kwa ujuzi Wake Anatuona na Anatusikia. Hayuko na sisi kwa dhati Yake.

قَالَ لَا تَخَافَا ۖ إِنَّنِي مَعَكُمَا أَسْمَعُ وَأَرَىٰ ﴿٤٦﴾

(Allaah) Akasema: “Msikhofu; hakika Mimi Niko pamoja nanyi, Nasikia na Naona. [Twaahaa: 46]

((إنَّكُمْ تَدْعونَ سَميعاً قَريباً وَهُوَ مَعَكُم)) رواه مسلم.

((Hakika nyinyi mnamuomba Mwenye kusikia, Aliye karibu, na Yeye Yuko pamoja nanyi)) [Muslim]