031-Aayah Na Mafunzo: Maana Ya Al-Kabaair (Dhambi Kubwa) Na Mifano Yake

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Maana Ya Al-Kabaair Dhambi Kubwa Na Mifano Yake

Alhidaaya.com

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِن تَجْتَنِبُوا كَبَائِرَ مَا تُنْهَوْنَ عَنْهُ نُكَفِّرْ عَنكُمْ سَيِّئَاتِكُمْ وَنُدْخِلْكُم مُّدْخَلًا كَرِيمًا ﴿٣١﴾

Mkijiepusha na madhambi makubwa mnayokatazwa Tutakufutieni madhambi yenu madogo na Tutakuingizeni katika mahali patukufu. [An-Nisaa: 31]

 

Mafunzo:

 

Al-Kabaair (dhambi kubwa): ni lile lililotajiwa ndani yake laana, au haddi (adhabu) hapa duniani, au limeahidiwa juu yake ghadhabu za Allaah au moto.

 

Na Nafiy’ bin Al-Haarith Ath-Thaqafiy Abuu Bakr (رضي الله عنه) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Je, nikujulisheni Al-Kabaair?” Tukasema: “Ndio ee Rasuli wa Allaah! Akasema: “Kumshirikisha Allaah, na kuwaasi wazazi wawili.” Alikuwa ameegemea, akakaa kitako akasema: “Tanabahi! Na kusema uongo na kushuhudia uongo!” “Tanabahi! Na kusema uongo na kushuhudia uongo!” Akaendelea kusema hayo mpaka nikadhani hatonyamaza. [Al-Bukhaariy (5976)].

 

Bonyeza kiungo kifuatacho kwa faida zaidi:

 

Madhambi Makubwa Na Madogo

 

 

 

 

 

Share