090-Asbaabun-Nuzuwl: Aal-'Imraan Aayah 090: إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا بَعْدَ إِيمَانِهِمْ ثُمَّ ازْدَادُوا كُفْرًا لَّن تُقْبَلَ تَوْبَتُهُمْ

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

Aal-‘Imraan  090-Hakika wale waliokufuru baada ya kuamini kwao kisha wakazidi kukufuru..

 

إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا بَعْدَ إِيمَانِهِمْ ثُمَّ ازْدَادُوا كُفْرًا لَّن تُقْبَلَ تَوْبَتُهُمْ وَأُولَـٰئِكَ هُمُ الضَّالُّونَ ﴿٩٠﴾ 

90. Hakika wale waliokufuru baada ya kuamini kwao kisha wakazidi kukufuru; haitokubaliwa tawbah yao, na hao ndio waliopotoka.

 

Sababun-Nuzuwl:

 

Aayah hii imeteremshwa kuhusu watu waliosilimu kisha wakaritadi kisha wakasilimu tena kisha wakaritadi. Wakatuma watu wao kwenda kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) kuulizia kuhusu jambo hilo. Na hapo ikateremka Aayah hii:

 

إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا بَعْدَ إِيمَانِهِمْ ثُمَّ ازْدَادُوا كُفْرًا لَّن تُقْبَلَ تَوْبَتُهُمْ وَأُولَـٰئِكَ هُمُ الضَّالُّونَ ﴿٩٠﴾ 

 

Hakika wale waliokufuru baada ya kuamini kwao kisha wakazidi kukufuru; haitokubaliwa tawbah yao, na hao ndio waliopotoka. [(3:90). Amehadithia Ibn ‘Abbaas  (رضي الله عنهما) . Ameipokea Al-Haafidhw Abuu Bakr Al-Bazzaar – Tafsiyr Ibn Kathiyr]  

 

 

Share