113-Asbaabun-Nuzuwl: Aal-'Imraan Aayah 113: لَيْسُوا سَوَاءً ۗ مِّنْ أَهْلِ الْكِتَابِ أُمَّةٌ قَائِمَةٌ يَتْلُونَ آيَاتِ اللَّـهِ

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

Aal-‘Imraan   113-Hawako sawa sawa; miongoni mwa Ahlil-Kitaabi wako

 

 

لَيْسُوا سَوَاءً ۗ مِّنْ أَهْلِ الْكِتَابِ أُمَّةٌ قَائِمَةٌ يَتْلُونَ آيَاتِ اللَّـهِ آنَاءَ اللَّيْلِ وَهُمْ يَسْجُدُونَ ﴿١١٣﴾

113. Hawako sawa sawa; miongoni mwa Ahlil-Kitaabi wako watu wenye kusimama (kwa utiifu) wanasoma Aayaat za Allaah nyakati za usiku na wao wanasujudu (katika Swalaah).

 

Sababun-Nuzuwl:

 

Aayah hii imeteremka kama alivyohadithia Ibn Mas’uwd (رضي الله عنه) kwamba: (Siku moja) Rasuli (صلى الله عليه وآله وسلم) aliichelewesha Swalaah ya ‘Ishaa, kisha akatoka kuja kuiswali Masjid na akawakuta Swahaba (رضي الله عنهم) bado wanamsubiri. Akasema: “Uhakika wa mambo ulivyo ni kuwa hakuna yoyote katika Watu wa Dini hizi anayemdhukuru Allaah katika wakati huu isipokuwa nyinyi tu.” Hapo ikateremka Aayah:

 

لَيْسُوا سَوَاءً ۗ مِّنْ أَهْلِ الْكِتَابِ

Hawako sawa sawa. Miongoni mwa Watu wa Kitabu…  

 

 mpaka mwisho wa Aayah 115. [Hadiyth ya Ibn Mas’uwd ameipokea Al-Imaam Ahmad]  

 

 

 

Share