033-Aayah Na Mafunzo: Allaah Anachukia Maasi Na Huwa Na Ghera Pindi Mja Wake Akitenda Maasi

 

Aayah Na Mafunzo

 

www.alhidaaya.com

 

Al-‘Araaf 33

 

033-Allaah Anachukia Maasi Na Huwa Na Ghera Pindi Mja Wake Akitenda Maasi

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

قُلْ إِنَّمَا حَرَّمَ رَبِّيَ الْفَوَاحِشَ مَا ظَهَرَ مِنْهَا وَمَا بَطَنَ وَالْإِثْمَ وَالْبَغْيَ بِغَيْرِ الْحَقِّ وَأَن تُشْرِكُوا بِاللَّـهِ مَا لَمْ يُنَزِّلْ بِهِ سُلْطَانًا وَأَن تَقُولُوا عَلَى اللَّـهِ مَا لَا تَعْلَمُونَ ﴿٣٣﴾

Sema: Hakika Rabb wangu Ameharamisha machafu ya wazi na ya siri, na dhambi, na ukandamizaji bila ya haki, na kumshirikisha Allaah kwa ambayo Hakuyateremshia mamlaka, na kusema juu ya Allaah yale ambayo hamyajui. [Al-Araaf: 33]

 

 

Mafunzo:

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أَنَّهُ قَالَ: ((إِنَّ اللَّهَ يَغَارُ وَغَيْرَةُ اللَّهِ أَنْ يَأْتِيَ الْمُؤْمِنُ مَا حَرَّمَ اللَّه)) متفق عليه

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه  وآله وسلم ) amesema: ((Hakika Allaah Ana hisia ya  ghera, na ghera  ya  Allaah [inachomoza] pale mtu anapofanya [maasi] Aliyoyaharamisha Allaah)) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

Na pia amesema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): “Hakuna mwenye ghera zaidi ya Allaah wakati anapozini mja wake au ummah Wake uzini.” [Al-Bukhaariy]

Faida: Kuhusu haramisho la kumshirikisha Allaah (سبحانه وتعالى) rejea tanbih (4: 48)

 

 

 

Share