04-Buluwgh Al-Maraam: Kitabu Cha Swalaah: Mlango Wa Sutrah (Kizuzi) Ya Mwenye Kuswali

 

 

بُلُوغُ الْمَرام

Buluwgh Al-Maraam

 

كِتَابُ اَلصَّلَاةِ

Kitabu Cha Swalaah

 

بَـــابُ سُــتْرَةِ اَلْمُصَــلِّي

04-Mlango Wa Sutrah[1] (Kizuzi) Ya Mwenye Kuswali

 

 

 

 

 

 

181.

عَنْ أَبِي جُهَيْمِ بْنِ اَلْحَارِثِ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ   قَالَ : قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم  {لَوْ يَعْلَمُ اَلْمَارُّ بَيْنَ يَدَيِ اَلْمُصَلِّي مَاذَا عَلَيْهِ مِنْ اَلْإِثْمِ لَكَانَ أَنْ يَقِفَ أَرْبَعِينَ خَيْرًا لَهُ مِنْ أَنْ يَمُرَّ بَيْنَ يَدَيْهِ}  مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِلْبُخَارِيِّ

وَوَقَعَ فِي "اَلْبَزَّارِ" مِنْ وَجْهٍ آخَرَ : {أَرْبَعِينَ خَرِيفًا}

Kutoka kwa Abuu Juhaym bin Al-Haarith[2] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Lau angejua anayepita mbele ya anayeswali, dhambi kubwa aliyo nayo ingekuwa bora kwake kusimama (siku) arubaini, kuliko kupita mbele yake.[3][Al-Bukhaariy, Muslim, na tamshi hili ni la Al-Bukhaariy]

 

Na imetajwa katika Al-Bazzaar kwa njia nyingine na imeongezwa: “Miaka arubaini.”

 

 

 

182.

وَعَنْ عَائِشَةَ  رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ : {سُئِلَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم   فِي غَزْوَةِ تَبُوكَ  عَنْ سُتْرَةِ اَلْمُصَلِّي . فَقَالَ : "مِثْلُ مُؤْخِرَةِ اَلرَّحْلِ"}  أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliulizwa katika vita vya Tabuwk kuhusu Sutrah (kizuizi) ya anayeswali, akasema: ni kama sehemu ya nyuma ya tandiko la mnyama[4].” [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

183.

وَعَنْ سَبْرَةَ بْنِ مَعْبَدٍ اَلْجُهَنِيِّ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ   قَالَ : قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {لِيَسْتَتِرْ أَحَدُكُمْ فِي صَلَاتِهِ وَلَوْ بِسَهْمٍ}  أَخْرَجَهُ اَلْحَاكِمُ 

Kutoka kwa Sabrah bin Ma’bad Al-Juhaniyy[5] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mmoja wenu aweke sutrah[6] katika Swalaah, japo kwa kuweka mshale.” [Imetolewa na Al-Haakim]

 

 

 

184.

وَعَنْ أَبِي ذَرٍّ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ   قَالَ : قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم  {يَقْطَعُ صَلَاةَ اَلْمَرْءِ اَلْمُسْلِمِ  إِذَا لَمْ يَكُنْ بَيْنَ يَدَيْهِ مِثْلُ مُؤْخِرَةِ اَلرَّحْلِ  اَلْمَرْأَةُ ، وَالْحِمَارُ ، وَالْكَلْبُ اَلْأَسْوَدُ . . . " اَلْحَدِيثَ}  وَفِيهِ {اَلْكَلْبُ اَلْأَسْوَدِ شَيْطَانٌ}  . أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ 

وَلَهُ : عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ   نَحْوُهُ دُونَ : "اَلْكَلْبِ

وَلِأَبِي دَاوُدَ ، وَالنَّسَائِيِّ : عَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ  رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا نَحْوُهُ ، دُونَ آخِرِهِ . وَقَيَّدَ اَلْمَرْأَةَ بِالْحَائِضِ

 Kutoka kwa Abuu Dharr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Itakapokuwa hakuna mbele yake, (Sutrah) mfano wa sehemu ya nyuma ya tandiko la mnyama[7], basi Swalaah ya Muislamu itakatika ikiwa atapita mwanamke au punda na mbwa mweusi.” Na Hadiyth inasema pia: “Na mbwa mweusi ni shaytwaan.[8][Imetolewa na Muslim]

 

Naye amepokea Hadiyth ya Abuu Hurayrah kama hiyo pasi na kutaja “mbwa.”

 

Nao Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy wamepokea Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) pasi na mwisho wake, na akafungamanisha mwanamke na hedhi.

 

 

 

185.

وَعَنْ أَبِي سَعِيدٍ اَلْخُدْرِيِّ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ   قَالَ : قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم  {إِذَا صَلَّى أَحَدُكُمْ إِلَى شَيْءٍ يَسْتُرُهُ مِنْ اَلنَّاسِ ، فَأَرَادَ أَحَدٌ أَنْ يَجْتَازَ بَيْنَ يَدَيْهِ فَلْيَدْفَعْهُ ، فَإِنْ أَبَى فَلْيُقَاتِلْهُ ، فَإِنَّمَا هُوَ شَيْطَانٌ}  مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ .

وَفِي رِوَايَةٍ : {فَإِنَّ مَعَهُ اَلْقَرِينَ}

 Kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mmoja wenu akiswali kuelekea kitu kinachomsitiri dhidi ya watu wengine, na mtu akataka kupita mbele yake, basi amzuie, akikataa, apigane naye[9], kwani huyo ni shaytwaan.” [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

Na katika Riwaayah nyingine: “Kwani shaytwaan yuko pamoja naye.”

 

 

 

186.

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ   قَالَ : قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {إِذَا صَلَّى أَحَدُكُمْ فَلْيَجْعَلْ تِلْقَاءَ وَجْهِهِ شَيْئًا ، فَإِنْ لَمْ يَجِدْ فَلْيَنْصِبْ عَصًا ، فَإِنْ لَمْ يَكُنْ فَلْيَخُطَّ خَطًّا ، ثُمَّ لَا يَضُرُّهُ مَنْ مَرَّ بَيْنَ يَدَيْهِ}  أَخْرَجَهُ أَحْمَدُ وَابْنُ مَاجَهْ ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ ، وَلَمْ يُصِبْ مَنْ زَعَمَ أَنَّهُ مُضْطَرِبٌ ، بَلْ هُوَ حَسَنٌ .

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Endapo mmoja wenu anaswali, basi aweke kitu mbele yake, na iwapo hana kitu cha kuweka, basi asimamishe fimbo, na akiwa hana fimbo basi achore msitari, ndipo hatadhuriwa na anayepita mbele yake[10].” [Imetolewa na Ahmad na Ibn Maajah, na akaisahihisha Ibn Hibbaan, wala hakupatia aliyesema ni Mudhw-twarib, bali hiyo ni Hasan]

 

 

 

187.

وَعَنْ أَبِي سَعِيدٍ اَلْخُدْرِيِّ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ   قَالَ : قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم  {لَا يَقْطَعُ اَلصَّلَاةَ شَيْءٌ ، وَادْرَأْ مَا اِسْتَطَعْتَ}  أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ ، وَفِي سَنَدِهِ ضَعْفٌ

Kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakuna chochote kinachokatisha Swalaah, lakini epusha kadiri mnavyoweza (vitu vinavyokatisha Swalaah).” [Imetolewa na Abuu Daawuwd, na katika Isnaad yake kuna udhaifu]

 

 

 

[1] Sutrah (kizuizi) ni kitu chochote ambacho mtu anayeswali hukiweka mbele yake iwe kama kizuizi kati yake yeye na wengine.

 

[2] Inasemekana kuwa huyu Abuu Juhaym jina lake ni ‘Abdullaah bin Al-Haarith bin As-Simma Al-Answaar Al-Khazraj. Alikuwa ni Swahaba anayejulikana sana, ambaye aliishi hadi wakati wa Ukhalifa wa Mu’aawiyah.

 

[3]  “Mpaka” wa mtu anayeswali ni mahala pale mahali anaposujudia. Kukatisha mbele zaidi ya mpaka huu siyo kosa. Onyo hili ni la mtu anayekatisha, siyo mtu aliyekwisha kukaa au anaswali mbele yake, na anayefanya vitendo vingine (visivyostahiki ndani ya Swalaah).

 

[4] Urefu wa Sutrah ni sharti uwe kwa uchache sawa sawa na sehemu ya nyuma ya tandiko. Hiyo ni sawa na takribani futi moja. Endapo hakuna kitu kingine, basi fimbo inaweza kufanya kazi badala ya Sutrah. Na iwapo hata fimbo hakuna, msitari waweza kuchorwa kama anavyoelezea Abuu Daawuwd.

 

[5] Sabrah bin Ma’yad Al-Juhaniyy alikuwa ni Swahaba kutoka Al-Madiynah aliyelowea kule Dhi Marwa. Alipewa jina la utani la Abuu Thuraiya. Kwanza alishiriki katika vita vya Al-Khandaq (Vita vya Handaki). Aliyekuwa ndiye mjumbe wa ‘Aliy kuenda kwa Mu’aawiyah, alipoteuliwa kuwa Khalifa, kumtaka athibitishe utii wa watu wa shaam kwa ‘Aliy. Alikufa mnamo mwish wa Ukhalifa wa Mu’aawiyah.

 

[6]  Wakati mtu anaposwali, Baraka za Allaah (عز وجل)  humuelekea yeye. Sutrah huwa kama ukingo, na Baraka za Allaah (عز وجل)  hubakia ndani ya eneo la ukingo huo. Mtu yoyote anayekatisha njia nje ya Sutrah hiyo, haikabili Baraka ya Allaah (عز وجل) na Swalaah haiathiriki. Kusipokuwepo Sutrah (kizuizi), basi huwa hakuna mpaka wa Baraka za Allaah (عز وجل), na mtu anayekatisha mbele ya mtu anayeswali hugongana na Baraka hiyo, na umakini kwa Allaah wa mtu wa anayeswali huvurugika. Kwa hivyo Sutrah ilifanywa iwe lazima.

 

[7] Inamaanisha kwamba inaathiri unyenyekevu kwa Allaah (عز وجل) tu, lakini hakuathiri Swalaah.

 

[8] Katika Hadiyth hii kuna ushahidi kuwa, bila kuwepo Sutrah viumbe vilivyotajwa hapo juu vikipita mbele ya mtu anayeswali, Swalaah yake hukatishwa. Lakini kuna Hadiyth iliyoafikiwa inayosema kuwa, Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) huku akiwa amempanda punda alipita mbele ya msururu wa Waumini wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa anaswali, naye Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) hakuirudia Swalaah yake wala hakuwaamuru Swahaba zake warudie Swalaah zao.

 

[9] Kupita mbele ya mtu anayeswali imeafikiwa kunahesabika ni kumtengeua. Iwapo mtu anaswali nyuma ya Sutrah (kizuizi), na mtu kukatisha njia apite ndani yake, asimamishwe kwa ishara, na aking’ang’ania kupita, azuiwe kwa nguvu. “Kupigana”. Endapo Muumini anaswali bila ya kuwa na Sutrah mbele yake, ni kosa na Muumini anayeswali na siyo kosa la mpitaji. Pia Hadiyth hii inaonyesha kuwa Swalaah ya Muumini huyo haikatishwi kwa kitendo hicho kidogo, lakini kitendo hicho kinaathiri umakinifu.

 

 

[10] Inaonyeshwa kuwa Swalaah haikatishwi kwa mtu kupita mbele, lakini huathiri umakinifu.

 

 

Share