01-Buluwgh Al-Maraam: Kitabu Cha Zakaah: Mlango Wa Zakaah Ya Mali

 

بُلُوغُ الْمَرام

Buluwgh Al-Maraam

 

كِتَابُ اَلزَّكَاةُ

Kitabu Cha Zakaah[1]

 

Mlango Wa Zakaah Ya Mali

 

 

 

 

 

483.

عَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا: {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم بَعَثَ مُعَاذًا رضى الله عنه إِلَى اَلْيَمَنِ.‏.‏.} فَذَكَرَ اَلْحَدِيثَ، وَفِيهِ: {أَنَّ اَللَّهَ قَدِ اِفْتَرَضَ عَلَيْهِمْ صَدَقَةً فِي أَمْوَالِهِمْ، تُؤْخَذُ مِنْ أَغْنِيَائِهِمْ، فَتُرَدُّ فِي‏ فُقَرَائِهِمْ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِلْبُخَارِيِّ

Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimtuma Mu’aadh (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) kuenda Yaman.” Akaitaja Hadiyth yote, miongoni mwa maneno yaliyomo: “Allaah Aliifanya Zakaah kuwa ni jambo la fardhi kwao, katika mali zao, huchukuliwa kutoka kwa matajiri wao na kupewa masikini wao.”[2] [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni Al-Bukhaariy]

 

 

 

484.

وَعَنْ أَنَسٍ رضى الله عنه أَنَّ أَبَا بَكْرٍ اَلصِّدِّيقَ رضى الله عنه كَتَبَ لَهُ ‏ {هَذِهِ فَرِيضَةُ اَلصَّدَقَةِ اَلَّتِي فَرَضَهَا رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم عَلَى اَلْمُسْلِمِينَ، وَاَلَّتِي أَمَرَ اَللَّهُ بِهَا رَسُولَهُ فِي أَرْبَعٍ وَعِشْرِينَ مِنَ اَلْإِبِلِ فَمَا دُونَهَا اَلْغَنَمُ ‏ فِي كُلِّ خَمْسٍ شَاةٌ، فَإِذَا بَلَغَتْ خَمْسًا وَعِشْرِينَ إِلَى خَمْسٍ وَثَلَاثِينَ فَفِيهَا بِنْتُ مَخَاضٍ أُنْثَى ‏ فَإِنْ لَمْ تَكُنْ فَابْنُ لَبُونٍ ذَكَرٍ ‏ فَإِذَا بَلَغَتْ سِتًّا وَثَلَاثِينَ إِلَى خَمْسٍ وَأَرْبَعِينَ فَفِيهَا بِنْتُ لَبُونٍ أُنْثَى، فَإِذَا بَلَغَتْ سِتًّا وَأَرْبَعِينَ إِلَى سِتِّينَ فَفِيهَا حِقَّةٌ طَرُوقَةُ اَلْجَمَلِ فَإِذَا بَلَغَتْ وَاحِدَةً وَسِتِّينَ إِلَى خَمْسٍ وَسَبْعِينَ فَفِيهَا جَذَعَةٌ ‏ فَإِذَا بَلَغَتْ سِتًّا وَسَبْعِينَ إِلَى تِسْعِينَ فَفِيهَا بِنْتَا لَبُونٍ، فَإِذَا بَلَغَتْ إِحْدَى وَتِسْعِينَ إِلَى عِشْرِينَ وَمِائَةٍ فَفِيهَا حِقَّتَانِ طَرُوقَتَا اَلْجَمَلِ، فَإِذَا زَادَتْ عَلَى عِشْرِينَ وَمِائَةٍ فَفِي كُلِّ أَرْبَعِينَ بِنْتُ لَبُونٍ، وَفِي كُلِّ خَمْسِينَ حِقَّةٌ، وَمَنْ لَمْ يَكُنْ مَعَهُ إِلَّا أَرْبَعٌ مِنَ اَلْإِبِلِ فَلَيْسَ فِيهَا صَدَقَةٌ إِلَّا أَنْ يَشَاءَ رَبُّهَا.‏

وَفِي صَدَقَةِ اَلْغَنَمِ سَائِمَتِهَا إِذَا كَانَتْ أَرْبَعِينَ إِلَى عِشْرِينَ وَمِائَةِ شَاةٍ ‏ شَاةٌ، فَإِذَا زَادَتْ عَلَى عِشْرِينَ وَمِائَةٍ إِلَى مِائَتَيْنِ فَفِيهَا شَاتَانِ، فَإِذَا زَادَتْ عَلَى مِائَتَيْنِ إِلَى ثَلَاثمِائَةٍ فَفِيهَا ثَلَاثُ شِيَاهٍ فَإِذَا زَادَتْ عَلَى ثَلَاثِمِائَةٍ فَفِي كُلِّ مِائَةٍ شَاةٌ، فَإِذَا كَانَتْ سَائِمَةُ اَلرَّجُلِ نَاقِصَةً مِنْ أَرْبَعِينَ شَاةٍ ‏ شَاةً وَاحِدَةً فَلَيْسَ فِيهَا صَدَقَةٌ، إِلَّا أَنْ يَشَاءَ رَبُّهَا.‏

وَلَا يُجْمَعُ بَيْنَ مُتَفَرِّقٍ وَلَا يُفَرَّقُ بَيْنَ مُجْتَمِعٍ خَشْيَةَ اَلصَّدَقَةِ، وَمَا كَانَ مِنْ خَلِيطَيْنِ فَإِنَّهُمَا يَتَرَاجَعَانِ بَيْنَهُمَا بِالسَّوِيَّةِ، وَلَا يُخْرَجُ فِي اَلصَّدَقَةِ هَرِمَةٌ ‏ وَلَا ذَاتُ عَوَارٍ، إِلَّا أَنْ يَشَاءَ اَلْمُصَّدِّقُ، وَفِي اَلرِّقَةِ ‏ رُبُعُ اَلْعُشْرِ، فَإِنْ لَمْ تَكُنْ إِلَّا تِسْعِينَ وَمِائَةً فَلَيْسَ فِيهَا صَدَقَةٌ إِلَّا أَنْ يَشَاءَ رَبُّهَا، وَمَنْ بَلَغَتْ عِنْدَهُ مِنَ اَلْإِبِلِ صَدَقَةُ اَلْجَذَعَةِ وَلَيْسَتْ عِنْدَهُ جَذَعَةٌ وَعِنْدَهُ حِقَّةٌ، فَإِنَّهَا تُقْبَلُ مِنْهُ اَلْحِقَّةُ، وَيَجْعَلُ مَعَهَا شَاتَيْنِ إِنِ اِسْتَيْسَرَتَا لَهُ، أَوْ عِشْرِينَ دِرْهَمًا، وَمَنْ بَلَغَتْ عِنْدَهُ صَدَقَةُ اَلْحِقَّةِ وَلَيْسَتْ عِنْدَهُ اَلْحِقَّةُ، وَعِنْدَهُ اَلْجَذَعَةُ، فَإِنَّهَا تُقْبَلُ مِنْهُ اَلْجَذَعَةُ، وَيُعْطِيهِ اَلْمُصَّدِّقُ عِشْرِينَ دِرْهَمًا أَوْ شَاتَيْنِ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ

Kutoka kwa Anas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kwamba Abuu Bakr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) alimuandikia barua kuwa: “Hii ni Swadaqah ya fardhi ambayo Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliifaridhisha kwa Waislam[3] na ambayo Allaah Alimuamrisha Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) aiamrishe.[4] Kwa kila ngamia ishirini na nne au zaidi, kondoo mmoja atolewe kwa kila tano. Wakitimia kati ya ishirini na tano mpaka thelathini na tano, atolewe ngamia jike wa mwaka wa pili.[5] Iwapo hakuna ngamia jike, basi atolewe ngamia dume wa mwaka wa tatu. Wakitimia thelathini na sita hadi arubaini na tano, atolewe ngamia jike wa mwaka wa tatu. Wakitimia arubaini na sita hadi sitini, atolewe ngamia jike wa mwaka wa nne[6] ambaye yu tayari kupandwa. Wakitimia sitini na moja hadi sabini na tano, atolewe ngamia jike wa mwaka wa tano. Wakitimia sabini na sita hadi tisini, watolewe ngamia wawili majike wa mwaka wa tatu, wakitimia tisini na moja hadi mia na ishirini, watolewe ngamia wawili majike wa mwaka wa nne, ambao wako tayari kupandwa. Wakizidi idadi ya mia na ishirini, ngamia mmoja jike wa mwaka wa tatu atolewe kwa kila arubaini, na ngamia mmoja jike wa mwaka wa nne atolewe kwa kila hamsini. Iwapo mtu anao ngamia wanne tu, hatozwi Swadaqah isipokuwa kama mwenye ngamia anataka kutoa.

Kuhusu Swadaqah ya kondoo wanaolishwa, wakitimia idadi ya arubaini hadi mia moja na ishirini, atolewe kondoo mmoja. Wakizidi mia moja na ishirini hadi mia mbili, watolewe kondoo wawili. Wakiwa zaidi ya mia mbili hadi mia tatu, watolewe kondoo watatu. Wakiwa zaidi ya mia tatu, kondoo mmoja atolewe kwa kila mia moja. Mtu akiwa na idadi ya kondoo chini ya arubaini, hatozwi Swadaqah isipokuwa kama mwenye kondoo hao anapenda.

Wala hawakusanywi waliotawanyika na waliokusanyika wasitenganishwe[7] kwa sababu ya kuogopa Swadaqah. Na wanaomilikiwa na washirika wawili, watadaiana walipane kwa usawa.[8] Kondoo mzee au kondoo mwenye chongo au kondoo dume asitolewe Swadaqah isipokuwa ikiwa mkusanyaji anataka hivyo.[9] Katika fedha: kwa Dirham mia mbili,[10] ilipwe moja ya arubaini, lakini zikiwepo mia moja na tisini tu, hailipii Zakaah isipokuwa kama mwenye fedha hiyo anataka kutoa. Endapo mtu yeyote mwenye idadi ya ngamia ambayo inahitaji kulipia Zakaah ya ngamia jike wa mwaka wa tano lakini hana ngamia huyo ila anaye ngamia wa mwaka wa nne,[11] mtu huyo alipe ngamia huyu pamoja na kondoo wawili iwapo anaweza kuwapata, vinginevyo alipe Dirham ishirini. Ikiwa mtu ana idadi ya ngamia ambayo inahitaji kulipa ngamia jike wa mwaka wa nne,[12] na hana ngamia kama huyu ila anaye ngamia jike wa mwaka wa tano, amtoe ngamia huyu na mkusanyaji lazima amrudishie Dirham ishirini au kondoo wawili.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]

 

 

 

485.

وَعَنْ مُعَاذِ بْنِ جَبَلٍ رضى الله عنه {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم بَعَثَهُ إِلَى اَلْيَمَنِ، فَأَمَرَهُ أَنْ يَأْخُذَ مِنْ كُلِّ ثَلَاثِينَ بَقَرَةً تَبِيعًا أَوْ تَبِيعَةً، وَمِنْ كُلِّ أَرْبَعِينَ مُسِنَّةً، وَمِنْ كُلِّ حَالِمٍ دِينَارًا أَوْ عَدْلَهُ مُعَافِرَ} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ، وَاللَّفْظُ لِأَحْمَدَ، وَحَسَّنَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ وَأَشَارَ إِلَى اِخْتِلَافٍ فِي وَصْلِهِ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ، وَالْحَاكِمُ

Kutoka kwa Mu’aadh bin Jabal (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimtuma kuenda Yaman, na akamuamrisha achukue ndama wa ng’ombe mwenye umri wa mwaka mmoja, dume au jike kwa kila ng’ombe telathini, na amchukue ng’ombe jike mmoja wa mwaka wa tatu[13] kwa kila arubaini, na Dinari moja kwa kila mtu mzima asiyekuwa Muislam (kama Jizya),[14] au nguo zenye thamani sawa zilizotengenezwa Yaman.” [imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) na tamshi hili ni la Ahmad, na At-Tirmidhiy amesema ni Hasan, na akataja kuwa kuna kutofautiana iwapo hii ni Mawswuwl au laa. Na wakaisahihisha Ibn Hibbaan na Al-Haakim]

 

 

 

486.

وَعَنْ عَمْرِو بْنِ شُعَيْبٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ جَدِّهِ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {تُؤْخَذُ صَدَقَاتُ اَلْمُسْلِمِينَ عَلَى مِيَاهِهِمْ} رَوَاهُ أَحْمَدُ

وَلِأَبِي دَاوُدَ: {وَلَا تُؤْخَذُ صَدَقَاتُهُمْ إِلَّا فِي دُورِهِمْ}

Kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb kwa upokezi wa baba yake kutoka kwa babu yake (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Swadaqah za Waislamu zipokewe kwenye manywesheo yao (maji).” [Imetolewa na Ahmad]

 

Na katika Riwaayah ya Abuu Daawuwd: “Swadaqah zao zipokewe majumbani mwao tu.”

 

 

 

487.

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {لَيْسَ عَلَى اَلْمُسْلِمِ فِي عَبْدِهِ وَلَا فِي فَرَسِهِ صَدَقَةٌ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ ‏

وَلِمُسْلِمٍ: {لَيْسَ فِي اَلْعَبْدِ صَدَقَةٌ إِلَّا صَدَقَةُ اَلْفِطْرِ}

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Muislamu hana Swadaqah katika mtumwa wake au farasi wake.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]

 

Na katika Riwaayah ya Muslim: “Hakuna Swadaqah kwa mtumwa isipokuwa Swadaqatul-Fitwr.”

 

 

 

488.

وَعَنْ بَهْزِ بْنِ حَكِيمٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ جَدِّهِ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {فِي كُلِّ سَائِمَةِ إِبِلٍ: فِي أَرْبَعِينَ بِنْتُ لَبُونٍ، لَا تُفَرَّقُ إِبِلٌ عَنْ حِسَابِهَا، مَنْ أَعْطَاهَا مُؤْتَجِرًا بِهَا فَلَهُ أَجْرُهُ، وَمَنْ مَنَعَهَا فَإِنَّا آخِذُوهَا وَشَطْرَ مَالِهِ، عَزْمَةً مِنْ عَزَمَاتِ رَبِّنَا، لَا يَحِلُّ لِآلِ مُحَمَّدٍ مِنْهَا شَيْءٌ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ، وَعَلَّقَ اَلشَّافِعِيُّ اَلْقَوْلَ بِهِ عَلَى ثُبُوتِهِ

Kutoka kwa Bahz bin Hakiym[15] kutoka kwa baba yake[16] naye kwa upokezi wa babu yake[17] amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kwa ajili ya ngamia arubaini wanaolishwa,[18] atolewe ngamia mmoja jike wa mwaka wa tatu. Hao ngamia wasitenganishwe wakati wa kuwahesabu. Mtu anayelipa Zakaah kwa kutaka thawabu atapata thawabu na mwenye kuzuia Zakaah sisi tutaichukua pamoja na nusu ya mali yake kama fidia ile Aliyoiweka Rabb wetu. Si halali humo chochote kwa Muhammad.” [Imetolewa na Ahmad, Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy, na akaisahihisha Al-Haakim]

Ash-Shaafi’iyy[19] amesema ameongezea kauli juu ya uthibitisho wa kutwaa nusu ya mali ya mtu aliyeikwepa Zakaah.

 

 

 

489.

وَعَنْ عَلِيٍّ  رضى الله عنه  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {إِذَا كَانَتْ لَكَ مِائَتَا دِرْهَمٍ وَحَالَ عَلَيْهَا اَلْحَوْلُ فَفِيهَا خَمْسَةُ دَرَاهِمَ، وَلَيْسَ عَلَيْكَ شَيْءٌ حَتَّى يَكُونَ لَكَ عِشْرُونَ دِينَارًا، وَحَالَ عَلَيْهَا اَلْحَوْلُ، فَفِيهَا نِصْفُ دِينَارٍ، فَمَا زَادَ فَبِحِسَابِ ذَلِكَ، وَلَيْسَ فِي مَالٍ زَكَاةٌ حَتَّى يَحُولَ عَلَيْهِ اَلْحَوْلُ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَهُوَ حَسَنٌ، وَقَدِ اِخْتُلِفَ فِي رَفْعِهِ

وَلِلتِّرْمِذِيِّ، عَنِ اِبْنِ عُمَرَ: {مَنِ اِسْتَفَادَ مَالًا، فَلَا زَكَاةَ عَلَيْهِ حَتَّى يَحُولَ اَلْحَوْلُ} وَالرَّاجِحُ وَقْفُهُ

Kutoka kwa ‘Aliy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Ukiwa na Dirham mia mbili zikapitiwa na mwaka, utazilipia Dirham tano, na hupaswi kulipa chochote mpaka umemiliki Dinari ishirini kwa muda wa mwaka mzima ambapo utazilipia nusu Dinari,[20] kinachozidi idadi hiyo kitahesabiwa hivyo hivyo. Na hakuna katika mali ya Zakaah mpaka ipitiwe na mwaka.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd. Ni Hasan na wanazuoni wametofautiana kama ni Marfuw’ au la]

 

Na At-Tirmidhiy alipokea hivi kutoka kwa ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ): “Mtu anayepata mali hapaswi kuilipia Zakaah mpaka mwaka umepita.” [Hadiyth hii imepewa daraja la Mawquwf]

 

 

 

490.

وَعَنْ عَلِيٍّ رضى الله عنه قَالَ:{لَيْسَ فِي اَلْبَقَرِ اَلْعَوَامِلِ صَدَقَةٌ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَاَلدَّارَقُطْنِيُّ، وَالرَّاجِحُ وَقْفُهُ أَيْضًا

Kutoka kwa ‘Aliy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Hakuna Swadaqah kwa ng’ombe anayefanyishwa kazi.”[21] [Imetolewa na Abuu Daawuwd na Ad-Daaraqutwniyy, na ikaitwa Maawquwf]

 

 

 

491.

وَعَنْ عَمْرِو بْنِ شُعَيْبٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ جَدِّهِ، عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ عَمْرِوٍ، أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {مِنْ وَلِيَ يَتِيمًا لَهُ مَالٌ، فَلْيَتَّجِرْ لَهُ، وَلَا يَتْرُكْهُ حَتَّى تَأْكُلَهُ اَلصَّدَقَةُ} رَوَاهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَاَلدَّارَقُطْنِيُّ، وَإِسْنَادُهُ ضَعِيفٌ

وَلَهُ شَاهِدٌ مُرْسَلٌ عِنْدَ اَلشَّافِعِيِّ

Kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb kwa upokezi wa baba yake kutoka kwa babu yake ‘Abdullaah bin ‘Amr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Endapo waliy wa yatima mwenye mali, ni lazima aifanyie biashara, asiiache tu mpaka imalizwe na Zakaah.”[22] [Imetolewa na At-Tirmidhiy na Ad-Daaraqutwniyy kwa Isnaad dhaifu]

 

Ina tafsiri inayoiunga mkono ambayo ni Mursal iliyosimuliwa na Ash-Shaafi’iyy

 

 

 

492.

وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ أَبِي أَوْفَى  رضى الله عنه  قَالَ: {كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم إِذَا أَتَاهُ قَوْمٌ بِصَدَقَتِهِمْ قَالَ: "اَللَّهُمَّ صَلِّ عَلَيْهِمْ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa ‘Abdullaah bin Abiy Awfaa (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Watu walipoleta Swadaqah zao kwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa akisema: Ee Allaah! Wabaarik hawa.” [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

493.

وَعَنْ عَلِيٍّ رضى الله عنه أَنَّ اَلْعَبَّاسَ رضى الله عنه {سَأَلَ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم فِي تَعْجِيلِ صَدَقَتِهِ قَبْلَ أَنْ تَحِلَّ، فَرَخَّصَ لَهُ فِي ذَلِكَ} رَوَاهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَالْحَاكِمُ

Kutoka kwa ‘Aliy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ): “Alimuomba Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kuharakiza kutoa Swadaqah yake kabla ya wakati, naye akamruhusu[23] kuilipa.” [Imetolewa na At-Tirmidhiy na Al-Haakim]

 

 

 

494.

وَعَنْ جَابِرِ بْنِ عَبْدِ اَللَّهِ رضى الله عنه عَنْ رَسُولِ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {لَيْسَ فِيمَا دُونَ خَمْسِ أَوَاقٍ مِنَ اَلْوَرِقِ صَدَقَةٌ، وَلَيْسَ فِيمَا دُونَ خَمْسٍ ذَوْدٍ مِنَ اَلْإِبِلِ صَدَقَةٌ، وَلَيْسَ فِيمَا دُونَ خَمْسَةِ أَوْسُقٍ مِنَ اَلتَّمْرِ صَدَقَةٌ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ

وَلَهُ مِنْ حَدِيثِ أَبِي سَعِيدٍ: {لَيْسَ فِيمَا دُونَ خَمْسَةِ أَوْسَاقٍ مِنْ تَمْرٍ وَلَا حَبٍّ صَدَقَةٌ} ‏‏

وَأَصْلُ حَدِيثِ أَبِي سَعِيدٍ مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Jaabir bin ‘Abdullaah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakuna Swadaqah chini ya Uqiya[24] tano (yaani gramu 595) za fedha, na chini ya ngamia watano, na kwa idadi chini ya kapu (Wasaq)[25] tano (gramu 652) za tende.”[26] [Imetolewa na Muslim]

Na Abuu Sa’iyd alisimuliwa kuwa: Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakuna Swadaqah (Zakaah) chini ya kapu tano za tende au nafaka.”[27]

 

 

 

495.

وَعَنْ سَالِمِ بْنِ عَبْدِ اَللَّهِ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {فِيمَا سَقَتِ اَلسَّمَاءُ وَالْعُيُونُ، أَوْ كَانَ عَثَرِيًّا: اَلْعُشْرُ، وَفِيمَا سُقِيَ بِالنَّضْحِ: نِصْفُ اَلْعُشْرِ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ ‏

وَلِأَبِي دَاوُدَ: {أَوْ كَانَ بَعْلًا: اَلْعُشْرُ، وَفِيمَا سُقِيَ بِالسَّوَانِي أَوِ اَلنَّضْحِ: نِصْفُ اَلْعُشْرِ}

Kutoka kwa Saalim bin ‘Abdillaah amesimulia kutoka kwa baba yake (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Katika kilichonyeshewa na mvua au chemchem, au kwa unyevu ni moja ya kumi, na katika kilichonyeshewa kwa njia ya umwagiliaji ni moja ya ishirini au ngamia wa ukame ni moja ya ishirini.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]

 

Na katika Riwaayah ya Abuu Daawuwd: “Iwapo hayo mazao ya shambani yatakuwa yalimwagiliwa maji na unyevu wa maji ya chini ya ardhi yatalipiwa moja ya kumi; lakini iwapo yatakuwa yamemwagiliwa kwa mifereji ya umwagiliaji, magurudumu ya maji, au ngamia wa ukame yatalipiwa moja ya ishirini.”

 

 

 

496.

وَعَنْ أَبِي مُوسَى اَلْأَشْعَرِيِّ، وَمُعَاذٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، أَنَّ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم قَالَ لَهُمَا: {لَا تَأْخُذَا فِي اَلصَّدَقَةِ إِلَّا مِنْ هَذِهِ اَلْأَصْنَافِ اَلْأَرْبَعَةِ: اَلشَّعِيرِ، وَالْحِنْطَةِ، وَالزَّبِيبِ، وَالتَّمْرِ} رَوَاهُ اَلطَّبَرَانِيُّ، وَالْحَاكِمُ

وَلِلدَّارَقُطْنِيِّ، عَنْ مُعَاذٍ: {فَأَمَّا اَلْقِثَّاءُ، وَالْبِطِّيخُ، وَالرُّمَّانُ، وَالْقَصَبُ، فَقَدْ عَفَا عَنْهُ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم} وَإِسْنَادُهُ ضَعِيفٌ

Kutoka kwa Abuu Muwsaa Al-Ash’ariyy na Mu’aadh (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) wamesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema kuwaambia: “Msikusanye Swadaqah ila kwa aina hizi nne tu zifuatazo: shayiri, ngano, zabibu kavu, na tende.” [Imetolewa na Atw-Twabaraaniyy na Al-Haakim

Na katika tafsiri ya pili ya Ad-Daaraqutwniyy kwa upokezi wa Mu’aadh amesema: “Ama matango, matikiti, makomamanga na miwa ilisamehewa na Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) isilipiwe Swadaqah.” [Isnaad yake ni dhaifu]

 

 

 

497.

وَعَنْ سَهْلِ بْنِ أَبِي حَثْمَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: أَمَرَنَا رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {إِذَا خَرَصْتُمْ، فَخُذُوا، وَدَعُوا اَلثُّلُثَ، فَإِنْ لَمْ تَدَعُوا اَلثُّلُثَ، فَدَعُوا اَلرُّبُعَ} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ إِلَّا اِبْنَ مَاجَهْ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ، وَالْحَاكِمُ

Kutoka kwa Sahl bin Abuu Hatmah[28] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah alituamrisha: “Mnapokadiria Swadaqah ya matunda kama tende, chukueni na muache theluthi moja, basi acheni robo ya Swadaqah inayokadiriwa kwa wamiliki wake.”[29] [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ahmad) isipokuwa Ibn Maajah, na akaisahihisha Ibn Hibbaan na Al-Haakim]

 

 

 

498.

وَعَنْ عَتَّابِ بنِ أُسَيْدٍ  رضى الله عنه  قَالَ: أَمَرَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {أَنْ يُخْرَصَ اَلْعِنَبُ كَمَا يُخْرَصُ اَلنَّخْلُ، وَتُؤْخَذَ زَكَاتُهُ زَبِيبًا} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ، وَفِيهِ اِنْقِطَاعٌ

Kutoka kwa ‘Attaab bin Usayd[30] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amessema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliamrisha Zakaah ya mizabibu ikadiriwe kama inavyokadiriwa mitende, na Zakaah yake ilipwe kwa zabibu zilizokaushwa kama Zakaah ya mitende ilipwavyo kwa tende zilizokaushwa.” [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) lakini ina katika Isnaad]

 

 

 

499.

وَعَنْ عَمْرِو بْنِ شُعَيْبٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ جَدِّهِ، {أَنَّ اِمْرَأَةً أَتَتِ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم وَمَعَهَا اِبْنَةٌ لَهَا، وَفِي يَدِ اِبْنَتِهَا مِسْكَتَانِ مِنْ ذَهَبٍ، فَقَالَ لَهَا: "أَتُعْطِينَ زَكَاةَ هَذَا؟" قَالَتْ: لَا.‏ قَالَ: "أَيَسُرُّكِ أَنْ يُسَوِّرَكِ اَللَّهُ بِهِمَا يَوْمَ اَلْقِيَامَةِ سِوَارَيْنِ مِنْ نَارٍ؟".‏ فَأَلْقَتْهُمَا.} رَوَاهُ اَلثَّلَاثَةُ، وَإِسْنَادُهُ قَوِيٌّ

وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ: مِنْ حَدِيثِ عَائِشَةَ

Kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb kwa upokezi wa baba yake kutoka kwa babu yake amesema: Mwanamke mmoja alikuja kwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ), alikuwa pamoja na binti yake aliyevaa bangili za dhahabu mkononi mwake. Akamuambia: “Unalipa Zakaah ya bangili hizo?” Akasema: “Hapana.” Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Je, utafurahi[31] iwapo Allaah Atakuwekea bangili mbili za moto badala yake?” Akazitupa. [Imetolewa na Ath-Thalaathah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd) na Isnaad yake ni imara. Imethibitishwa na Al-Haakim kutokana na Hadiyth ya ‘Aaishah]

 

 

 

500.

وَعَنْ أُمِّ سَلَمَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا، {أَنَّهَا كَانَتْ تَلْبَسُ أَوْضَاحًا مِنْ ذَهَبٍ فَقَالَتْ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! أَكَنْزٌ هُوَ؟ فَـقَالَ: "إِذَا أَدَّيْتِ زَكَاتَهُ، فَلَيْسَ بِكَنْزٍ"} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَاَلدَّارَقُطْنِيُّ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ

Kutoka kwa Ummu Salamah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: “Yeye alikua akivaa bangili za dhahabu[32] akauliza: Ee Rasuli wa Allaah! Hii ni hazina? Akasema: “Si hazina iwapo utailipia Zakaah yake.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na Ad-Daaraqutwniyy na akaisahihisha Al-Haakim]

 

 

 

501.

وَعَنْ سَمُرَةَ بْنِ جُنْدُبٍ رضى الله عنه قَالَ: {كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَأْمُرُنَا; أَنْ نُخْرِجَ اَلصَّدَقَةَ مِنَ اَلَّذِي نَعُدُّهُ لِلْبَيْعِ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَإِسْنَادُهُ لَيِّنٌ

Kutoka kwa Samurah bin Jundub (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa akituamrisha tutoe Swadaqah katika vitu tunavyo viandaa kwa biashara.”[33] [Imetolewa na Abuu Daawuwd, na Isnaad yake ni dhaifu]

 

 

 

502.

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: "وَفِي اَلرِّكَازِ: اَلْخُمُسُ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Na katika hazina iliyofukiwa chini hutozwa moja ya tano.”[34] [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

503.

وَعَنْ عَمْرِو بْنِ شُعَيْبٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ جَدِّهِ، {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم قَالَ فِي كَنْزٍ وَجَدَهُ رَجُلٌ فِي خَرِبَةٍ: "إِنْ وَجَدْتَهُ فِي قَرْيَةٍ مَسْكُونَةٍ، فَعَرِّفْهُ، وَإِنْ وَجَدْتَهُ فِي قَرْيَةٍ غَيْرِ مَسْكُونَةٍ، فَفِيهِ وَفِي اَلرِّكَازِ: اَلْخُمُسُ "} أَخْرَجَهُ اِبْنُ مَاجَهْ بِإِسْنَادٍ حَسَنٍ

Kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb amemnukuu baba yake, kuwa babu yake (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesimulia kuwa: Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema kuhusu hazina alioipata mtu mahala pasipotumika: “Ukiipata kwenye makazi ya watu, lazima uwajulishe. Ukiipata pasipo makazi na katika hazina iliyozikwa basi ni moja ya tano.” [Imetolewa na Ibn Maajah kwa Isnaad nzuri]

 

 

 

504.

وَعَنْ بِلَالِ بْنِ اَلْحَارِثِ رضى الله عنه { أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم أَخَذَ مِنَ اَلْمَعَادِنِ اَلْقَبَلِيَّةِ اَلصَّدَقَةَ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ

Kutoka kwa Bilaal bin Al-Haarith[35] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipokea Swadaqah ya machimbo ya Al-Qabaliyyah.”[36] [Imetolewa na Abuu Daawuwd]

 

[1] Maana ya Zakaah ni “Kuongezeka na kutakasika.” Kwa sababu malipo ya Zakaah hupelekea kuongezeka kwa mali na kwa hivyo huhesabika kuwa ni sababu ya kutakasika kwake, wajibu huu umepewa jina la Zakaah na Shariy’ah. Zakaah ilifaradhishwa mwaka wa 2 A.H., kabla ya amri ya Swawm.

[2] Hadiyth inatufundisha kuwa Zakaah ni lazima kwa matajiri miongoni mwa Waislam. Zakaah hii ni ya kuwapa msaada Waislam maskini, na hawapewi wasiokuwa Waislam. Tunafunzwa zaidi kuwa, Zakaah inayokusanywa katika mji mmoja sharti wagawiwe maskini wa mji huo huo.

[3] Wakati wa Abuu Bakr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) alipomteua Anas kuwa Gavana wa Bahrayn kwa niaba yake, alimpa maagizo haya yanayohusu Zakaah kwa maandishi.

 

[4] Kuhusu usahihi wa Hadiyth hii, yaani Isnaad ni sahihi kabisa. Kuhusu maandishi, nayo ni wazi kabisa, na kuna maafikiano ya pamoja ya Maswahaba wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kuhusu usahihi wake. Hakuna Swahaba hata mmoja wa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliyewahi kuikanusha Hadiyth hii.

[5] بِنْتُ مَخَاضٍ (Bint Makhaadhw) ni neno linalotumika kwa ngamia mwenye umri wa mwaka mmoja na ameingia katika mwaka wa pili wa umri wake.

[6] حِقَّةٌ (Hiqqah) ni neno linalotumika kwa ngamia mwenye umri wa miaka mitatu na ameingia katika mwaka wa nne wa umri wake, na ana uwezo wa kupandwa.

[7] Mfano wa kuunganisha mali ya Zakaah zilizotengana ni kama ifuatavyo: “Kuna watu wawili wana kundi la mbuzi hamsini kila mmoja wao, kwa hivyo wanatakiwa kutoa mbuzi mmoja kila mtu kutoka katika hisa zao. Endapo watu hawa wawili wataunganisha makundi yao mawili kuwa kundi moja, watapata faida ya kutoa mbuzi mmoja tu kwa pamoja kama Zakaah ya mbuzi mia moja, kwa sababu Zakaah ya mbuzi mia moja ni mbuzi mmoja tu.” Mfano wa kutenganisha kesi za Zakaah zilizoungana ni kama ifuatavyo: “Watu wawili wanamiliki kundi moja la mbuzi hamsini kwa ubia wa sawa kwa sawa. Kwa hivyo Zakaah ya mbuzi hawa hamsini itakuwa ni mbuzi mmoja. Lakini wakiligawanya kundi lao na kuwatenganisha ili kila mmoja awe na mbuzi ishirini na tano tu, wataepuka kutoa Zakaah kwa kuwa idadi ya mbuzi wa kila mmoja ni chini ya mbuzi arubaini. Hali kadhalika mkusanyaji wa Zakaah asithubutu kuunganisha wala kutenganisha mali za watu, yaani akiwakuta watu wawili wakiwa na mbuzi thelathini kila mmoja na kwa hivyo wanasamehewa kutoa Zakaah, mkusanyaji hana ruhusa ya kuunganisha hayo makundi mawili mbalimbali ya watu hao wawili na kulifanya liwe kundi moja ili adai wale watu walipe mbuzi mmoja.”

 

[8] Kwa mfano watu wawili wanamiliki mbuzi mia moja na arubaini. Mmoja anamiliki arubaini wakati mwenziwe anamiliki mia moja. Zakaah hapa inakuwa mbuzi wawili. Lakini ikiwa mmiliki wa mbuzi arubaini anamuambia mwenziwe hivi: “Ni bora ulipe Zakaah ya mbuzi mmoja na nusu, na mimi nilipe nusu ya mbuzi mmoja.” Hivyo haitakuwa sahihi. Shariy’ah yataka mmiliki wa mbuzi arubaini alipe mbuzi mmoja kamili, na mmiliki wa mbuzi mia pia naye alipe mbuzi mmoja tu kamili kama Zakaah yake.

 

[9] Hii inamaanisha kwamba, mtu anayetaka kutoa Zakaah asijaribu kutoa vitu vyenye dosari, wala mkusanyaji au mpokeaji naye asijaribu kuchukua vitu vizuri zaidi kuliko vyote. Vitu vitolewe vile vyenye thamani ya wastani.

 

[10] Moja ya kumi na mbili ya Uqiya moja ya dhahabu, kwa thamani.

[11] جَذَعَةٌ (Jadha’ah) ni neno linalotumika kwa ngamia jike ambaye ana miaka mine na ameingia mwaka wa tano wa umri wake.

 

[12] حِقَّةٌ (Hiqqah) ni neno linalotumika kwa ngamia jike wa miaka mitatu na ameingia mwaka wa nne wa umri wake.

[13] Ng’ombe na nyati ni jamii moja ya wanyama. Wote hao, wa jinsia zote mbili, wanajumuishwa katika hesabu. Mtu anayemiliki chini ya ng’ombe thelathini hatozwi Zakaah, wakitimia thelathini, hutozwa ndama mwenye umri wa mwaka mmoja. Wanyama anaowamiliki mtu wakiwa kati ya arubaini na sitini na tisa, Zakaah itakuwa ndama wa miaka miwili. Wakitimia sabini Zakaah ni ile ile, yaani ndama mmoja wa miaka miwili pamoja na ndama mmoja wa mwaka mmoja.

 

[14] Jizyah ni kodi ya kichwa anayoilipa mtu asiyekuwa Muislam anayeishi katika nchi ya Kiislam.

[15] Bahz bin Hakiym ndiye Abuu ‘Abdil-Maalik Bahz bin Hakiym bin Mu’aawiya bin Haida Al-Qushayr Al-Basri. Alikuwa Taabi’i wa daraja la sita. Uaminifu au utegemewaji wake umekanushwa. Abuu Daawuwd amesema: “Ahaadiyth zake ni sahihi.” Pia Ibn Maa’in, Ibn Al-Madiniy, na An-Nasaaiy walimkubali. Lakini Abuu Haatim amesema: “Huyo siyo mtaalam wa Hadiyth.” Naye Ibn Hibbaan amesema: “Alikuwa na makosa mengi katika Hadiyth.” Alikufa baada ya miaka ya 140 A.H. au kabla ya miaka sitini.

[16] Na huyu babake Bahz pia ni Taabi’i ambaye Ibn Hibbaan alimhesabu kuwa ni mpokezi na msimuliaji mwaminifu wa Hadiyth.

 

[17] Babu yake ni Mu’aawiyah bin Hayda bin Mu’aawiya bin Qushayr bin Ka’b Al-Qushayr, na alikuwa Swahaba aliyelowea Basra na alikuwa anazo Ahaadiyth.

 

[18] Hali ya Zakaah ya ng’ombe ni kwamba sharti wawe wazima na nguvu za kutosha kijilisha wao wenyewe. Hali hii ilitajwa hususan kwa mbuzi na ngamia. Na kanuni hiyo hiyo imeamriwa kwa ajili ya ng’ombe na nyati.

[19] Hadiyth hii inadhihirisha kwamba, iwapo mtu halipi Zakaah kwa hiari yake, Serikali  ya ya Kiislam inaweza kumtoza faini yenye thamani ya nusu ya bidhaa zake na wanaweza kuichukua kwa nguvu. Kutozwa hivyo kwa nguvu kutakidhi deni alilonalo huyo mtu, lakini atanyimwa thawabu.

[20] Hadiyth hii inaongelea Zakaah inayotozwa katika dhahabu na fedha. Uzito wa fedha ni kuanzia Dirham mia mbili na zaidi. Uzito hasa wa fedha unaostahili kulipiwa Zakaah ni tola hamsini na nusu (sawa na gramu 611.5) na Zakaah inayotozwa kwa kiasi itakuwa moja ya arubaini. Halikadhalika kiasi cha dhahabu ipaswayo kutolewa Zakaah ni tola saba na nusu (sawa na gramu 87), Zakaah ipaswayo kulipwa kwa kiasi hiki ni moja ya arubaini pia. Na hata kwa pesa za noti hulipiwa hiyo hiyo 1/40.

[21] Ng’ombe wafanyao kazi za kulima, kuchota na kumwagia maji, na wasafirishaji, ndio wanaohusika.

[22] Kuna tofauti za maoni ya Wanazuoni kuhusu iwapo mali ya yatima itolewe Zakaah au laa. Juu ya kuwepo kukhitilafiana,  ni bora kuilipia Zakaah.

[23] Siku na nyakati za Hajj, Swalaah na Swawm zote zimepangwa wazi. Lakini kuhusu Zakaah hakuna wakati maalumu. Ulipaji wake unaweza kuahirishwa au pia unaweza kulipwa mapema, ingawa huwa inakuwa deni baada ya muda wa mwaka mmoja tu.

[24] Kwa kuwa thamani ya Uqiya moja ni Dirham 40 (au gramu 128), basi Waqiya tano zitakuwa sawa sawa na Dirham 200.

 

[25] Takribani kilo kumi na mbili unusu.

[26] Kwa mujibu wa vipimo vya siku hizi, kiasi cha Zakaah ipasavyo kulipwa kwa kila maund 20 za nafaka (yaani quintal 8), itakuwa maund moja ya nafaka (yaani takribani kilo 40). Iwapo kiasi cha nafaka ni chini ya quintal 8, hakuna kuilipia hiyo Zakaah hiyo. Quintal 8 ni sawa na Wasq 5 ambayo imetajwa katika Hadiyth hii. Endapo mtu atamiliki zaidi ya gramu 87 za dhahabu, huyo analazimika ailipie Zakaah. Na endapo mtu atamiliki zaidi ya gramu 611.5, basi huyu pia inapaswa ailipie Zakaah.

[27] Nafaka yoyote inayoweza kuhifadhiwa kwa mwaka mmoja, inapaswa ilipiwe Zakaah. Ngano, shayiri, mpunga, mtama, mahindi ya Kihindi, mahindi jamii ya kunde na choroko n.k. vyote vinaingia katika kundi hili. Zakaah ya hivi hutegemea kiasi cha kazi na adha itokanayo na kuzalisha hivi. Mazao ya ardhi ambayo yamemwagiliwa maji na ya mafuriko, au mbubujiko wa asili au mito, yatalipiwa moja ya kumi ya kazi ya kuyazalisha. Ikiwa ardhi imemwagiliwa na maji ya kisima au kwa kulipia pesa maji yale kama maji ya mifereji, basi mazao yake yatalipiwa Zakaah ya moja ya ishirini tu ya jumla yake.

[28] Sahl bin Abiy Hatmah, jina lake halisi ni ‘Abdullaah au ‘Aamir bin Sa’ida bin ‘Aamir Al-Answaar Al-Khazraj Al-Madaniy. Alikuwa Swahaba aliyezaliwa mnamo mwaka wa 3A.H. alilowea Kufa na anahesabika kuwa yu mkazi wa Al-Madiynah ambako alifia wakati wa ugavana wa Mus’ab bin Az-Zubayr.

 

[29] Maana ya neno la kiarabu “Kharsw” ni kubahatisha au kudhania, yaani kukisia kiasi cha matunda yanayoweza kuzaliwa baada ya kukomaa na kuiva. Mtu kama huyo ni sharti aifanye kazi yake kwa uaminifu mkubwa sana. Kanuni ya wakusanyaji Zakaah ni kiasi cha theluthi moja ya kiasi hicho alichokikadiria. Kama hakubaliani nacho basi lazima aache robo yake, au mara nyingine mmiliki anaweza kuwapa majirani zake baadhi yake.

[30] ‘Attaab bin Usayd bin Abiy Al-‘Ays bin Umayyah bin ‘Abd Shams Al-Umawi Al-Makki alikuwa Swahaba. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimteua aitawale Makkah katika mwaka wa kuiteka, kwa kuwa alikuwa akienda Humayn na akaendelea kuitawala hadi Abuu Bakr alipofariki. Inasemekana naye alifariki siku hiyo hiyo aliyofariki Abuu Bakr. Inasemwa pia kuwa aliishi hadi mwisho wa Ukhalifa wa ‘Umar.

[31] Suala la Zakaah ya mapambo ya dhahabu lina mvutano. Lakini rai ya wengi ni kuwa iyo Zakaah ni lazima ilipwe, na Hadiyth hii ni ushahidi wake.

[32] أوضاح  (Awdhwaah) ni wingi wa وضع.  Hiyo ilikuwa ni aina ya mapambo ambayo zamani yalikuwa yakitengenezwa kwa fedha. Kwa sababu ya kumeremeta kwake, ikaitwa أَوْضَاح, baadaye ikawa inatengenezwa kwa dhahabu pia. Kwa hivyo Hadiyth hii inathibitisha kuwa mapambo ya fedha na dhahabu yanapaswa kulipiwa Zakaah. Kuna mapambo mengine yasiyokuwa ya dhahabu na fedha, yasiyostahili kulipiwa Zakaah. Hayo ni mapambo ya lulu, zumaridi, johari, rubi, marijani na vito vingine.

[33] Kwa hivyo hii inatufahamisha, bidhaa zote za biashara hustahili kulipiwa Zakaah.

[34] Mali yoyote iliyofukuliwa kutoka ardhini ni اَلرِّكَازِ (Ar-Rikaaz), yaani ni hazina iliyofichwa ilimradi ni ya kutoka zama za wasiokuwa Waislam, na ni lazima kuweka moja ya tano ya mali hiyo katika hazina ya Kiislam. Hii haina lile sharti la kuwa hiyo moja ya tano iwekwe baada ya kupita mwaka mmoja.

[35] Alipewa jina la utani wa ‘Abdur-Rahmaan, na alikuwa miongoni mwa wajumbe wa kwanza kumzuru Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kule Al-Madiynah kutoka katika kabila la Muzaynah mnamo mwaka wa 5 A.H. alishika bendera ya Muzaynah wakati wa kuiteka Makkah. Aliishi nje ya Al-Madiynah na baadaye akahamia Basra. Alifariki mnamo mwaka wa 60 A.H. huku akiwa na miaka 80.

 

[36] Qabaliyyah ni jina la mahala iliyo pwani ya bahari umbali wa safari ya siku tano kwa kupanda ngamia kutoka Al-Madiynah.

Share