02-Buluwgh Al-Maraam: Kitabu Cha Zakaah: Mlango Wa Zakaatul-Fitwr

 

بُلُوغُ الْمَرام

Buluwgh Al-Maraam

 

كِتَابُ اَلزَّكَاةُ

Kitabu Cha Zakaah

 

بَابُ صَدَقَةِ اَلْفِطْرِ

Mlango Wa Zakaatul-Fitwr

 

 

 

505.

عَنِ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {فَرَضَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم زَكَاةَ اَلْفِطْرِ، صَاعًا مِنْ تَمْرٍ، أَوْ صَاعًا مِنْ شَعِيرٍ: عَلَى اَلْعَبْدِ وَالْحُرِّ، وَالذَّكَرِ، وَالْأُنْثَى، وَالصَّغِيرِ، وَالْكَبِيرِ، مِنَ اَلْمُسْلِمِينَ، وَأَمَرَ بِهَا أَنْ تُؤَدَّى قَبْلَ خُرُوجِ اَلنَّاسِ إِلَى اَلصَّلَاةِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

وَلِابْنِ عَدِيٍّ  مِنْ وَجْهٍ آخَرَ ، وَاَلدَّارَقُطْنِيِّ بِإِسْنَادٍ ضَعِيفٍ: {اغْنُوهُمْ عَنِ اَلطَّوَافِ فِي هَذَا اَلْيَوْمِ}

Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliamrisha Zakkaatul-Fitwr kwa mtumwa, mtu huru, mwanaume, mwanamke, kijana, na mzee miongoni mwa Waislam, pishi moja (sawa sawa na takribani kilogramu mbili na nusu) ya tende zilizokaushwa, au Swaa’ moja ya shayiri, na akaamrisha itolewe kabla watu hawajaondoka kuenda kuswali Swalaah ya ‘Iydul-Fitwr.” [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

Na Ibn ‘Adiyy na Ad-Daaraqutwniy alisimulia Hadiyth hiyo kwa Isnaad dhaifu: “Watosheni (wapeni mahitaji yao) dhidi ya kuenda njiani wakiombaomba katika siku hii.”

 

 

 

506.

وَعَنْ أَبِي سَعِيدٍ اَلْخُدْرِيِّ  رضى الله عنه  قَالَ: {كُنَّا نُعْطِيهَا فِي زَمَانِ اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم صَاعًا مِنْ طَعَامٍ، أَوْ صَاعًا مِنْ تَمْرٍ، أَوْ صَاعًا مِنْ شَعِيرٍ، أَوْ صَاعًا مِنْ زَبِيبٍ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ ‏

وَفِي رِوَايَةٍ: {أَوْ صَاعًا مِنْ أَقِطٍ}

قَالَ أَبُو سَعِيدٍ: {أَمَّا أَنَا فَلَا أَزَالُ أُخْرِجُهُ كَمَا كُنْتُ أُخْرِجُهُ فِي زَمَنِ رَسُولِ اَللَّهِ}

وَلِأَبِي دَاوُدَ: {لَا أُخْرِجُ أَبَدًا إِلَّا صَاعًا}

Kutoka kwa Sa’iyd Al-Khudriyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Wakati alipokuwepo Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ), tulikua tukitoa Pishi moja ya nafaka[1] kama Zakkaatul-Fitwr, au tende kavu, au shayiri, au zabibu kavu.” [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

Na katika Riwaayah nyingine inasema: “Au Swaa’ pishi moja ya jibini.”

 

Abuu Sa’iyd amesema: “Mimi sitaacha kutoa kama nilivyokuwa nikitoa (Pishi) wakati Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipokuwa hai.”

Na tafsiri ya Abuu Daawuwd inasema: “Sijawahi kutoa Swadaqah ila Pishi.”

 

 

 

507.

وَعَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {فَرَضَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم زَكَاةَ اَلْفِطْرِ، طُهْرَةً لِلصَّائِمِ مِنَ اَللَّغْوِ، وَالرَّفَثِ، وَطُعْمَةً لِلْمَسَاكِينِ، فَمَنْ أَدَّاهَا قَبْلَ اَلصَّلَاةِ فَهِيَ زَكَاةٌ مَقْبُولَةٌ، وَمَنْ أَدَّاهَا بَعْدَ اَلصَّلَاةِ فَهِيَ صَدَقَةٌ مِنَ اَلصَّدَقَاتِ.} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَابْنُ مَاجَهْ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ

Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliamrisha Zakkaatul-Fitwr iwe ndiyo utakaso wa mtu anayefunga Swawm dhidi ya maongezi ya kipuuzi na uchafu, pamoja na kuwa chakula kwa watu maskini. Mtu yeyote atailipa hiyo kabla ya Swalaah ya ‘Iydul-Fitwr itakubaliwa kama Zakaah. Lakini mtu akiilipa hiyo baada ya Swalaah ya ‘Iydul-Fitwr[2] itahesabika kuwa ni Swadaqah miongoni mwa Swadaqah zingine.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na Ibn Maajah na akaisahihisha Al-Haakim]

 

 

[1] Neno la Kiarabu: “طَعَامٍ” (Twa’aam) hutumika kwa aina mbalimbali za nafaka. Inaweza kutumika kwa ngano, shairi, na tende pia. Kwa ujumla yaweza kutumika kwa kila zao la kilimo.

[2] Hii inamaanisha kwamba, mtu akiilipa hiyo Zakaatul-Fitwr (Zakaah ya kufungulia Swawm), haimuondoshei wajibu wala hapati thawabu zinazohusiana na malipo hayo kama Zakaah. Hata hivyo ulipaji huu haupotei hivi hivi kwani atapata thawabu za tendo la kawaida tu la Swadaqah. Ni bora kulipa Pishi moja nzima (Kilo 2.6) kama Zakaatul-Fitwr, kwani ule usimulizi unaotaja nusu ya pishi siyo sahihi.

Share