04-Shaykh Swaalih Al-Fawzaan: Mwajiriwa Benki Anataka Kufanya Hajj

 

 

Mwajiriwa Benki Anataka Kufanya Hajj

 

Shaykh Swaalih Al-Fawzaan (Hafidhwahu Allaah)

 

www.alhidaaya.com

 

 

 

SWALI:

 

Mimi ni mwajiriwa wa Benki, je naruhusiwa kufanya Hajj kwa mshahara wangu?

 

 

JIBU:

 

 

Kufanya kazi katika benki zinazohusika na riba hairuhusiwi. Hii kwa sababu ni kusaidia katika dhambi na uovu. Pia Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amelaani mwenye kula/kufaidika na riba, pia mwenye kuhusika na utendaji wa makubaliano (transaction), shahidi wa utendaji makubaliano, na mwenye kuandika utendaji wa makubaliano. 

 

Kwa hiyo, kwa mtazamo halisi, mfanya kazi huwa hasa anasaidia benki hata kama yeye ni karani tu wa benki. Hivyo hulaaniwa kutokana na kauli ya Hadiyth. Kutokana kwayo, mshahara anaopokea ni haraam na haruhusiwi kula/kufaidika nao wala kufanyia Hajj. Hii ni kwa sababu kufanya Hajj kunahitaji kipato kilichokuwa safi kutoka katika chanzo cha halaal. Lakini ikiwa tayari ameshafanya Hajj, basi Hajj yake ni sahihi lakini itaambatana na dhambi kwa maana ujira wake utakuwa ni mdogo.

 

 

[Al-Muntaqaa min Fataawa Shaykh Fawzaan – Mjalada 4, Uk. 121, Fatwa Namba 123.] 

 

 

Share