18-Zawadi Kwa Wanandoa: Malipo Ya Kuingiliana

 

Zawadi Kwa Wanandoa 

 

18-Malipo ya Kuingiliana

 

 ثواب الجماع

 

 

Katika kuingiliana hakupatikani kwa raha peke yake bali kunabeba ndani yake malipo mtu anayolipwa na Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)  katika kufanya hivyo na mke wake au mume wake, amesema Abu Dharr (Radhiya Allaahu 'anhu) :

 

Hakika watu katika Maswahaba walimwambia Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam)  : Ee Mtume wa Allaah wameondoka wenye uwezo (ahlu duthuur) na malipo yote, huswali kama tunavyosali, hufunga kama tunavyofunga, na hutoa sadaka katika bora ya mali zao. Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam)  akawaambia, “Je, Allaah Hakuwajaalia katika ya kutoa sadaka? Hakika katika kila tasbiyh (Subhaana-Allaah) ni sadaka. Na katika kila takbiyr (Allaahu Akbar) ni sadaka, na kila tahliyl (La ilaaha illa Allaah) ni sadaka. Na kila tahmiid (AlhamduliLLaah) ni sadaka. Kuamrisha mema ni sadaka na kukataza maovu ni sadaka vile vile na kumuingilia mkeo ni sadaka.” Wakasema Maswahaba na je, katika kupata raha binafsi mmoja wetu analipwa??!. Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam)  akasema: “Je, mnaonaje lau mtu huyo angeingiza (tupu yake) katika haramu, je, ingelikuwa ni shari juu yake (ya madhambi, maradhi, adhabu)?, wakasema: ndio. Akasema  Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) : “Hivyo ndivyo atakapoweka (tupu yake) katika halali atalipwa.”  (Muslim)

Share