062-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Mlango Wa Twahara: Ni Kipi Kinatosheleza Tayammumi?

 

Swahiyh Fiqh As-Sunnah

 

Mlango Wa Twahara

 

062-Ni Kipi Kinatosheleza Tayammumi?

 

Alhidaaya.com

 

 

Kutayamamu kunakuwa ni badala ya wudhuu na josho la janaba wakati maji yanapokosekana au kuwa vigumu kuyatumia. An-Nawawiy amesema:

 

“Haya ndiyo madhehebu yetu. Na hivi ndivyo walivyosema Maulamaa wote katika Maswahaba, Taabi’iyna na waliokuja baada yao isipokuwa ‘Umar bin Al-Khattwaab, ‘Abdullaah bin Mas-’oud na Ibrahiym An-Nakhi’y ambaye ni Taabi’iy. [Imekuja katika Swahiyh Al-Bukhaariy (345) na Muslim (796) kuwa Ibn Mas-’oud amekataza kutayamamu kwa ajili ya janaba na kuwa Abu Muusa alimpinga kwa Aayah.

 

Ninasema: “Huenda Ibn Mas-’oud kulipinga hilo, kumetolewa juu ya yale yaliyo sahihi kwake toka kwa At-Twabariy (9606) wakati alipolifasiri Neno Lake Allaah Mtukufu: ((أو لامستم النساء)) akisema kuwa الملامسة ni chini ya kujamii].

 

Hawa wamelizuia, yaani wamezuia kutayamamu kwa ajili ya hadathi kubwa”.

 

Ibn As-Swibaagh na wengine wamesema kuwa inasemekana kuwa ‘Umar na ‘Abdullaah waliachana na msimamo wao.

 

Jamaa zetu hawa na Jamhuri wametoa dalili ya Kauli Yake Allaah Mtukufu:

((إذا قمتم إلى الصلاة فاغسلوا وجوهكم))

((Mnaposimama kuswali, basi osheni nyuso zenu)).

Hadi Neno Lake:

((وأن كنتم جنبا فالطهروا))

((Na mkiwa na janaba, basi jitwaharisheni)).

 

Kisha Allaah Mtukufu Akasema:

((فلم تجدوا ماء فتيمموا))

((na hamkupata maji, basi tayamamuni)).

Na hili linarejea kwa wote wawili; asiye na wudhuu na mwenye janaba. [Al-Majmu’u (2/240)].

 

Ninasema:

“Kuna dalili nyingine juu ya usharia wa kutayamamu kwa ajili ya hadathi kubwa. Ni Neno Lake Allaah Mtukufu:

((أو جاء أحد منكم من الغائط أو لامستم النساء فلم تجدوا ماء فتيمموا صعيدا طيبا))  

((Au mmoja wenu ametoka chooni, au mmewagusa wanawake na msipate maji, basi ukusudieni mchanga safi)). [An-Nisaa (4: 43)].

 

Makusudio ya kugusana hapa ni tendo la kujamii kwa mujibu wa kauli ya mjumuiko wa Maulamaa akiwemo Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu Anhu). [Tafsiyr At-Twabariy (9583) kwa Sanad Swahiyh kutoka kwake].

 

Kisha kuna Hadiyth Swahiyh zilizopokelewa toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) zinazofahamisha kuwa kutayamamu hutosheleza janaba. Kati ya Hadiyth hizo ni:

 

1- Hadiyth tuliokwisha ielezea ya ‘Imraan bin Haswiyn wakati Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) alipomwambia mwenye janaba:

((عليك بالصعيد فإنه يكفيك))

((Tumia mchanga, kwani unakutosha)). [Imekubaliwa na Al Bukhaariy na Muslim. Imeelezewa karibuni].

 

2- Hadiyth ya ‘Ammaar bin Yaasir, amesema: “Nilipata janaba, kisha nilijigaragaza mchangani, nikamjulisha Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) juu ya hilo, akaniambia:

:إنما كان يكفيك هكذا))

((وضرب يديه على الأرض، ومسح وجهه وكفيه

((Hakika ilikuwa inakutosha hivi:

Akapiga mikono yake miwili juu ya ardhi, akaosha uso wake na viganja vyake viwili)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukaariy (338) na Muslim (798)].

 

Je, Maiti Hutayamamishwa Maji Yakikosekana?

 

Maiti hutayamamishwa kama aliyehai maji yakikosekana, kwani kuoshwa maiti ni lazima. Tumekwishaeleza nyuma kuwa mchanga hutwaharishiwa maji yakikosekana. [Angalia Al-Muhalla (2/158)]

 

 

Share