019-Hiswnul-Muslim: Du’aa Za Wakati Wa Kusujudu

Hiswnul-Muslim

019-Du’aa Za Wakati Wa Kusujudu

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[41]

سُبْـحانَ رَبِّـيَ الأَعْلـى  

 

Subhaana Rabbiyal a’-laa

 

Ametakasika Rabb wangu Aliye juu[1]     (mara 3)

  

 

 

[42]

سُبْـحانَكَ اللّهُـمَّ رَبَّـنا وَبِحَـمْدِكَ، اللّهُـمَّ اغْفِرْ لي

 

Subhaanaka Allaahumma Rabbanaa wabihamdika, Allaahummagh-firliy

 

Utakasifu ni Wako Ee Allaah, Rabb wetu, na Himdi ni Zako, Ee Allaah nighufurie [2]

 

 

[43]

سُبـّوحٌ قُـدّْوس، رَبُّ الملائِكَـةِ وَالـرُّوح

 

Subbuwhun Qudduwsun, Rabbul-Malaaikati war-Ruwh

 

Mwingi wa kutakaswa, Mtakatifu, Rabb wa Malaika na Roho[3]         

 

 

[44]

 

اللّهُـمَّ لَكَ سَـجَدْتُ وَبِـكَ آمَنْـتُ، وَلَكَ أَسْلَـمْتُ، سَجَـدَ وَجْهِـيُ لِلَّـذي خَلَقَـهُ وَصَـوَّرَهُ وَشَقَّ سَمْـعَـهُ وَبَصَـرَهُ، تَبـارَكَ اللهُ أَحْسـنُ الخـالِقيـن

Allaahumma Laka sajjadtu, wabika aamantu, walaka aslamtu. Sajada wajhiya liLLadhiy khalaqahu, wa swaw-warahu, wa shaqqa sam-’ahu wa baswarahu, Tabaaraka-Allaahu Ahsanul-Khaaliqiyn

 

Ee Allaah Kwako nimesujudu, na Wewe nimekuamini, na Kwako nimesilimu, umesujudu uso wangu kumsujudia Aliyeuumba na Akautia sura na Akaupasua usikizi wake na uwoni wake, Amebarikika Allaah Mbora wa waumbaji [4]

 

 

 

[45]

سُبْـحانَ ذي الْجَبَـروت، والمَلَـكوت، وَالكِبْـرِياء، وَالْعَظَـمَه

 

Subhaana dhil-Jabaruwti wal-malakuwti, wal-kibriyaai, wal-‘adhwamah

 

Ametakasika Mwenye Ujabari (Utawala, Utukufu), na Ufalme, na Ukubwa, na Uadhama [5].

 

 

 [46]

اللّهُـمَّ اغْفِـرْ لي ذَنْـبي كُلَّـه، دِقَّـهُ وَجِلَّـه، وَأَوَّلَـهُ وَآخِـرَه وَعَلانِيَتَـهُ وَسِـرَّه

 

Allaahummagh-firliy dhambiy kullahu diqqahu wajillahu wa awwalahu wa aakhirahu wa ’alaaniyatahu, wasirrahu

 

Ee Allaah nighufurie dhambi zangu zote, ndogo na kubwa, za mwanzo na za mwisho, za dhahiri na za siri[6]

 

 

 

[47]

 

اللّهُـمَّ إِنِّـي أَعـوذُ بِرِضـاكَ مِنْ سَخَطِـك، وَبِمعـافاتِـكَ مِنْ عُقوبَـتِك، وَأَعـوذُ بِكَ مِنْـك، لا أُحْصـي ثَنـاءً عَلَـيْك، أَنْـتَ كَمـا أَثْنَـيْتَ عَلـى نَفْسـِك

 

Allaahumma inniy a’uwdhu biridhwaaka min sakhatwika, wabimu’aafaatika min ’uquwbatika, wa a’uwdhu Bika Minka, laa uhswiy thanaa-an ’Alayka, Anta kamaa athnayta ’alaa Nafsika

 

Ee Allaah hakika mimi najikinga kwa radhi Zako kutokana na hasira Zako, na kwa msamaha Wako kutokana na adhabu Yako, na najikinga Kwako unihifadhi na Wewe, mimi siwezi kuzidhibiti sifa Zako, Wewe ni kama ulivyojisifu Mwenyewe[7].

 

 

 

[1]Hadiyth ya Hudhayfah bin Al-Yamaan (رضي الله عنه) - Ahlus-Sunan: Abu Daawuwd [871], At-Tirmdhiy [262], An-Nasaaiy (1/190) Ibn Maajah [888], Ahmad [394, 382] na angalia: Swahiyh At-Tirmidhiy (1/83)

 

[2]Hadiyth ya ‘Aaishah (رضي الله عنها) imetangulia namba 34 juu - Al-Bukhaariy (1/99), Muslim (1/350).

 

[3]Hadiyth ya ‘Aaishah (رضي الله عنها)  imetangulia juu namba 35 -Muslim (1/353), Abu Daawud (1/230)

 

[4]Hadiyth ya ‘Aliy bin Twaalib (رضي الله عنه) - Muslim (1/534) na wengineo.

 

[5]Hadiyth ya ‘Awf bin Maalik Al-Ashja’iyy (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd (1/230), An-Nasaaiy (2/191), Ahmad (6/24) na isnadi yake ni Hasan.

Abu Daawuwd (1/230), Ahmad (6/24), An-Nasaaiy (2/191) na ameipa daraja ya Swahiyh Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh Abi Daawuwd (1/166)  (Pia imetangulia katika Du’aa Namba 37)  

 

[6]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه)  - Muslim (1/350)

 

[7]Hadiyth ya ‘Aaishah (رضي الله عنها)  - Muslim (1/352)

 

 

 

 

Share