061-Asbaabun-Nuzuwl: Asw-Swaff Aayah 1-3: يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لِمَ تَقُولُونَ مَا لاَ تَفْعَلُونَ

 أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

061-Asw-Swaff: 1-3

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

سَبَّحَ لِلَّـهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۖ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ﴿١﴾

1. Vimemsabbih Allaah Pekee vilivyomo katika mbingu na vilivyomo katika ardhi, Naye ndiye Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye hikmah wa yote.

 

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لِمَ تَقُولُونَ مَا لَا تَفْعَلُونَ﴿٢﴾

2. Enyi walioamini! Kwanini mnasema yale msiyoyafanya?

 

 

كَبُرَ مَقْتًا عِندَ اللَّـهِ أَن تَقُولُوا مَا لَا تَفْعَلُونَ﴿٣﴾

3. Ni chukizo kubwa mno mbele ya Allaah kwamba mnasema yale msiyoyafanya.

 

 

Sababun-Nuzuwl:

 

حَدَّثَنَا عَبْدُ اللَّهِ بْنُ عَبْدِ الرَّحْمَنِ، أَخْبَرَنَا مُحَمَّدُ بْنُ كَثِيرٍ، عَنِ الأَوْزَاعِيِّ، عَنْ يَحْيَى بْنِ أَبِي كَثِيرٍ، عَنْ أَبِي سَلَمَةَ، عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ سَلاَمٍ، قَالَ قَعَدْنَا نَفَرٌ مِنْ أَصْحَابِ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَتَذَاكَرْنَا فَقُلْنَا لَوْ نَعْلَمُ أَىَّ الأَعْمَالِ أَحَبُّ إِلَى اللَّهِ لَعَمِلْنَاهُ فَأَنْزَلَ اللَّهُ تَعَالَى‏:‏ ‏((سبَّحَ لِلَّهِ مَا فِي السَّمَوَاتِ وَمَا فِي الأَرْضِ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ * يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لِمَ تَقُولُونَ مَا لاَ تَفْعَلُونَ))‏ قَالَ عَبْدُ اللَّهِ بْنُ سَلاَمٍ فَقَرَأَهَا عَلَيْنَا رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ أَبُو سَلَمَةَ فَقَرَأَهَا عَلَيْنَا ابْنُ سَلاَمٍ.‏ قَالَ يَحْيَى فَقَرَأَهَا عَلَيْنَا أَبُو سَلَمَةَ.‏ قَالَ ابْنُ كَثِيرٍ فَقَرَأَهَا عَلَيْنَا الأَوْزَاعِيُّ‏.‏ قَالَ عَبْدُ اللَّهِ فَقَرَأَهَا عَلَيْنَا ابْنُ كَثِيرٍ.‏

 قَالَ أَبُو عِيسَى وَقَدْ خُولِفَ مُحَمَّدُ بْنُ كَثِيرٍ فِي إِسْنَادِ هَذَا الْحَدِيثِ عَنِ الأَوْزَاعِيِّ.‏ وَرَوَى ابْنُ الْمُبَارَكِ عَنِ الأَوْزَاعِيِّ عَنْ يَحْيَى بْنِ أَبِي كَثِيرٍ عَنْ هِلاَلِ بْنِ أَبِي مَيْمُونَةَ عَنْ عَطَاءِ بْنِ يَسَارٍ عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ سَلاَمٍ أَوْ عَنْ أَبِي سَلَمَةَ عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ سَلاَمٍ.‏ وَرَوَى الْوَلِيدُ بْنُ مُسْلِمٍ هَذَا الْحَدِيثَ عَنِ الأَوْزَاعِيِّ نَحْوَ رِوَايَةِ مُحَمَّدِ بْنِ كَثِيرٍ‏.‏

 

Ametuhadithia ‘Abdullaah bin ‘Abdir-Rahmaan, ametuelezea Muhammad bin Kathiyr, toka kwa Al-Awzaa’iy kutoka kwa Yahyaa bin Abiy Kathiyr kutoka kwa Abiy Salamah kutoka kwa ‘Abdullaah bin Salaam amesema: Tulikaa kundi la watu wachache katika Maswahaba wa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) tukakumbushana (masuala ya kidini). Tukasema: Lau tungeliijua 'amali yoyote inayopendeza zaidi kwa Allaah, basi tungeliifanya. Hapo Allaah Ta’alaa Akateremsha:

 سَبَّحَ لِلَّـهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۖ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ﴿١﴾

1. Vimemsabbih Allaah Pekee vilivyomo katika mbingu na vilivyomo katika ardhi, Naye ndiye Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye hikmah wa yote.

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لِمَ تَقُولُونَ مَا لَا تَفْعَلُونَ﴿٢﴾

2. Enyi walioamini!  Kwanini mnasema yale msiyoyafanya?

 

‘Abdullaah bin Salaam amesema: Akatusomea (Aayah hii) Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم). Abuu Salamah amesema: Akatusomea Ibn Salaam. Yahyaa amesema: Akatusomea Abuu Salamah. Ibn Kathiyr amesema: Akatusomea Al-Awzaa’iy. ‘Abdullaah amesema: Akatusomea Ibn Kathiyr.

 

[Abuu ‘Iysaa amesema: Muhammad bin Kathiyr amezozewa katika Isnaad ya Hadiyth hii kutoka kwa Al-Awzaa’iy. Ibn Al-Mubaarak amesimulia kutoka kwa Al-Awzaa’iy kutoka kwa Yahyaa bin Abiy Kathiyr kutoka kwa Hilaal bin Abiy Maymuwnah kutoka kwa ‘Atwaa bin Yasaar kutoka kwa ‘Abdullaah bin Salaam au kutoka kwa Abuu Salamah kutoka kwa ‘Abdullaah bin Salaam. Al-Waliyd bin Muslim ameisimulia Hadiyth hii kutoka kwa Al-Awzaa’iy kuelekea riwaayah ya Muhammad bin Kathiyr].

 

 

Share