30-Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Ummah Wake Utakuwa Wa Kwanza Kuhukumiwa Siku Ya Qiyaamah

Fadhila Za  Nabiy  (صلى الله عليه وآله وسلم)

30-Ummah Wake Utakuwa Wa Kwanza Kuhukumiwa Siku Ya Qiyaamah

www.alhidaaya.com

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ، وَعَنْ رِبْعِيِّ بْنِ حِرَاشٍ، عَنْ حُذَيْفَةَ، قَالاَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏ "‏ أَضَلَّ اللَّهُ عَنِ الْجُمُعَةِ مَنْ كَانَ قَبْلَنَا فَكَانَ لِلْيَهُودِ يَوْمُ السَّبْتِ وَكَانَ لِلنَّصَارَى يَوْمُ الأَحَدِ فَجَاءَ اللَّهُ بِنَا فَهَدَانَا اللَّهُ لِيَوْمِ الْجُمُعَةِ فَجَعَلَ الْجُمُعَةَ وَالسَّبْتَ وَالأَحَدَ وَكَذَلِكَ هُمْ تَبَعٌ لَنَا يَوْمَ الْقِيَامَةِ نَحْنُ الآخِرُونَ مِنْ أَهْلِ الدُّنْيَا وَالأَوَّلُونَ يَوْمَ الْقِيَامَةِ الْمَقْضِيُّ لَهُمْ قَبْلَ الْخَلاَئِقِ ‏"‏ ‏.‏ وَفِي رِوَايَةِ وَاصِلٍ الْمَقْضِيُّ بَيْنَهُمْ ‏.‏

  

Kutoka kwa Abuu Hurayrah na Abuu Rib-‘iyy bin Hiraash kutoka kwa Hudhayfah kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Ilikuwa ni Ijumaa ambayo Allaah Aliigeuza kutoka kwa walio kabla yetu. Mayahudi wakawa na Siku ya Jumamosi na Manaswara Siku ya Jumapili. Allaah Akatuletea na kutuongoza sisi Siku ya Ijumaa (siku tukufu ya Swalaah ya jamaah) Akajaalia Ijumaa, Jumamosi na Jumapili (kuwa ni siku tukufu). Kwa utaratibu huu wao (Mayahudi na Manaswara) watakuja baada yetu Siku ya Qiyaamah. Sisi (ni Ummah) wa mwisho katika watu wa dunia, lakini wa kwanza miongoni mwa viumbe kuhukumiwa Siku ya Qiyaamah)) na katika riwaayah nyengine:  ((Kuhukumiwa miongoni mwao)) [Al-Bukhaariy]

 

Share