077-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuwa na Hasira Wakati Inapokiukwa Hukumu ya Sheria na Kuinusuru Dini ya Allaah Ta'aalaa

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

 

باب الغضب إِذَا انتهكت حرمات الشّرع والانتصار لدين الله تعالى

077-Mlango Wa Kuwa na Hasira Wakati Inapokiukwa Hukumu ya Sheria na Kuinusuru Dini ya Allaah Ta'aalaa

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَمَن يُعَظِّمْ حُرُمَاتِ اللَّـهِ فَهُوَ خَيْرٌ لَّهُ عِندَ رَبِّهِ ۗ  ﴿٣٠﴾

Na yeyote anayeadhimisha vitukufu vya Allaah basi hivyo ni khayr kwake mbele ya Rabb wake. [Al-Hajj: 30]

 

إِن تَنصُرُوا اللَّـهَ يَنصُرْكُمْ وَيُثَبِّتْ أَقْدَامَكُمْ﴿٧﴾

Mkisaidia kunusuru Dini ya Allaah, (Allaah) Atakunusuruni na Ataithibitisha miguu yenu. [Muhammad: 7]

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي مسعود عقبة بن عمرو البدري  رضي الله عنه ، قَالَ : جَاءَ رَجُلٌ إِلَى النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، فَقَالَ : إنِّي لأَتَأخَّرُ عَن صَلاةِ الصُّبْحِ مِنْ أَجْلِ فلانٍ مِمَّا يُطِيلُ بِنَا ! فَمَا رَأيْتُ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم غَضِبَ في مَوْعِظَةٍ قَطُّ أشَدَّ مِمَّا غَضِبَ يَوْمَئذٍ ؛ فَقَالَ : ((  يَا أَيُّهَا النَّاسُ ، إنَّ مِنْكُمْ مُنَفِّرِينَ ، فَأيُّكُمْ أمَّ النَّاسَ فَلْيُوجِزْ ؛ فَإنَّ مِنْ وَرَائِهِ الكَبِيرَ وَالصَّغِيرَ وَذَا الحَاجَةِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu Mas'uwd 'Uqbah bin 'Amru Al-Badriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Mtu mmoja alikuja kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Mimi ninachelewa Swalaah ya Asubuhi kwa ajili ya fulani anarefusha kisomo." Sijaona Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameghadhibika katika mawaidha yoyote kama alivyokasirika siku hiyo. Akasema: "Enyi watu! Hakika miongoni mwenu kuna wenye kufukuza, Anaposwalisha mmoja wenu afupishe, kwani nyuma yake kuna wazee, na watoto wadogo, na wenye haja zao (shughuli zao)." [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad].

 

 

Hadiyth – 2

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : قَدِمَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم مِنْ سَفرٍ ، وَقَدْ سَتَرْتُ سَهْوَةً لِي بِقِرَامٍ فِيهِ تَمَاثيلُ، فَلَمَّا رَآهُ رسول الله صلى الله عليه وسلم هتكَهُ وَتَلَوَّنَ وَجهُهُ ، وقال : ((  يَا عائِشَةُ ، أشَدُّ النَّاسِ عَذَاباً عِنْدَ اللهِ يَوْمَ القيَامَةِ الَّذِينَ يُضَاهُونَ بخَلْقِ اللهِ ! )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwake 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Alikuja Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kutoka safari wakati ambao nilikuwa nimeangika pazia nyembamba iliyokuwa na sura (picha) nje ya chumba changu. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipoiona hiyo pazia aliiharibu na sura zake zikabadilika, na hapo akasema: "Ee 'Aaishah! Watu watakao pata adhabu kali kutoka kwa Allaah Siku ya Qiyaamah ni wale ambao watakaokuwa wakitengeneza sura kwa mfano wa viumbe vya Allaah." [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

Hadiyth – 3

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : أن قرَيشاً أهَمَّهُمْ شَأنُ المَرأَةِ المخزومِيَّةِ الَّتي سَرَقَتْ ، فقالوا : مَنْ يُكَلِّمُ فِيهَا رسول الله صلى الله عليه وسلم ؟ فقالوا : مَنْ يَجْتَرِئ عَلَيْهِ إِلاَّ أُسَامَةُ بنُ زَيْدٍ حِبُّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ؟ فَكَلَّمَهُ أُسَامَةُ ، فَقَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  أتَشْفَعُ في حَدٍّ مِنْ حُدُودِ الله تَعَالَى ؟! )) ثُمَّ قامَ فَاخْتَطَبَ ، ثُمَّ قَالَ : ((  إنَّمَا أهْلَك مَنْ قَبْلَكُمْ أَنَّهُمْ كَانُوا إِذَا سَرَقَ فِيهِمُ الشَّرِيفُ تَرَكُوهُ ، وَإِذَا سَرَقَ فِيهِمُ الضَّعِيفُ أقامُوا عَلَيْهِ الحَدَّ ، وَايْمُ الله ، لَوْ أَنَّ فَاطمَةَ بِنْتَ مُحمّدٍ سَرَقَتْ لَقَطَعتُ يَدَهَا )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwake 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa Makureshi walishughulishwa na kesi ya mwanamke wa Makhzuum aliyeiba, wakasema: "Hakuna anayeweza kuzungumza naye ila usamah bin Zayd kipenzi cha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) juu ya jambo hilo?" wakasema: "Hakuna anayeweza kuzungumza naye ila Usamah bin Zayd kipenzi cha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)?" Usamah akazungumza naye, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Unamuombea msamaha kwa Hadd (adhabu) miongoni mwa adhabu za Allaah? Kisha akasimama akahutubia akasema: "Hakika waliangamia waliokuwa kabla yenu, walikuwa anapoiba kati yao mtukufu wanamwacha, na anapoiba kati yao dhaifu wanamuadhibu. Naapa kwa Allaah! Lau Faatimah bint Muhammad angeiba basi ningekata mkono wake." [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

Hadiyth – 4

وعن أنس رضي الله عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم رَأى نُخَامَةً في القبلَةِ ، فَشَقَّ ذَلِكَ عَلَيْهِ حَتَّى رُؤِيَ في وَجْهِهِ ؛ فَقَامَ فَحَكَّهُ بِيَدِهِ ، فَقَالَ : ((  إن أحدَكُمْ إِذَا قَامَ فِي صَلاَتِهِ فَإنَّهُ يُنَاجِي رَبَّهُ ، وَإنَّ رَبَّهُ بَيْنَهُ وَبيْنَ القِبلْةِ ، فَلاَ يَبْزُقَنَّ أحَدُكُمْ قِبَلَ الْقِبْلَةِ ، وَلَكِنْ عَنْ يَسَارِهِ ، أَوْ تَحْتَ قَدَمِهِ )) ثُمَّ أخَذَ طَرَفَ رِدَائِهِ فَبَصَقَ فِيهِ ، ثُمَّ رَدَّ بَعْضَهُ عَلَى بَعْضٍ ، فَقَالَ : ((  أَوْ يَفْعَلُ هكذا )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliona kohozi kwenye Qiblah, Jambo hilo lilimkera mpaka likaonekana katika uso wake akasimama akalikwangua kwa mkono wake, Akasema: "Hakika mmoja wenu anaposimama katika Swalaah yake anazungumza na Rabb wake, na Rabb wake yuko baina yake na Qiblah. Hivyo, asiteme mmoja wenu sehemu ya Qiblah , lakini ateme kushotoni mwake au chini ya unyao wake." Kisha akashika ncha ya shuka yake juu ya nyingine akasema: "Au anaweza kufanya hivi." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Share