078-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Jukumu la Viongozi Kuamiliana na Watu kwa Upole, Kuwanasihi, Kuwahurumia, Kukatazwa Kuwadanganya, Kuwawekea Vikwazo Bila Kuangalia Maslahi yao, Kughafilika Nao na Kutowatimizia Haja zao

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

 

باب أمر وُلاة الأمور بالرفق برعاياهم ونصيحتهم والشفقة عليهم والنهي عن غشهم والتشديد عليهم وإهمال مصالحهم والغفلة عنهم وعن حوائجهم

078-Mlango Wa Jukumu la Viongozi Kuamiliana na Watu kwa Upole, Kuwanasihi, Kuwahurumia, Kukatazwa Kuwadanganya, Kuwawekea Vikwazo Bila Kuangalia Maslahi yao, Kughafilika Nao na Kutowatimizia Haja zao

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَاخْفِضْ جَنَاحَكَ لِمَنِ اتَّبَعَكَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ ﴿٢١٥﴾

Na inamisha ubawa wako kwa anayekufuata miongoni mwa Waumini. [Ash-Shu'araa: 215]

 

إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ وَإِيتَاءِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَيَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ ۚ يَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ﴿٩٠﴾

Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan na kuwapa (msaada) jamaa wa karibu; na Anakataza machafu na munkari na ukandamizaji. Anakuwaidhini ili huenda mkapata kukumbuka. [An-Nahl: 90]

 

 

Hadiyth – 1

وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : ((  كُلُّكُمْ رَاعٍ ، وَكُلُّكُمْ مَسْؤُولٌ عَنْ رَعِيَّتهِ : الإمَامُ رَاعٍ وَمَسؤُولٌ عَنْ رَعِيَّتِهِ ، وَالرَّجُلُ رَاعٍ في أهلِهِ وَمَسؤُولٌ عَنْ رَعِيَّتِهِ ، وَالمَرْأَةُ رَاعِيَةٌ في بَيْتِ زَوْجِهَا وَمَسْؤُولَةٌ عَنْ رَعِيَّتِهَا ، وَالخَادِمُ رَاعٍ في مال سيِّدِهِ وَمَسْؤُولٌ عَنْ رَعِيَّتِهِ ، وَكُلُّكُمْ رَاعٍ وَمَسْؤُولٌ عَنْ رَعِيَّتِهِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swaalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kila mmoja ana majukumu (na ataulizwa) kwa wale walioko chini yake. Amiri ni mchunga na mwanamume ni mchunga kwa watu wake wa nyumbani na mke ni mchunga katika nyumba ya mumewe na watoto wake. Hivyo, kila mmoja wenu ni mchunga, na ataulizwa juu ya alichokichunga." [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad].

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي يعلى مَعْقِل بن يَسارٍ رضي الله عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : ((  مَا مِنْ عَبْدٍ يَستَرْعِيهِ اللهُ رَعِيَّةً ، يَمُوتُ يَوْمَ يَمُوتُ وَهُوَ غَاشٌّ لِرَعِيَّتِهِ ، إِلاَّ حَرَّمَ اللهُ عَلَيْهِ الجَنَّة )) متفقٌ عليه .

وفي رواية : ((  فَلَمْ يَحُطْهَا بِنُصْحِهِ لَمْ يَجِدْ رَائِحَةَ الجَنَّة )) .

وفي رواية لمسلم : ((  مَا مِنْ أميرٍ يلي أمور المُسْلِمينَ ، ثُمَّ لا يَجْهَدُ لَهُمْ وَيَنْصَحُ لَهُمْ ، إِلاَّ لَمْ يَدْخُلْ مَعَهُمُ الْجَنَّةَ )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Ya'laa Ma'qil bin Yasaar (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hakuna mja yeyote Allaah anampa uchungu wa raia wake, akafa siku anayokufa ameghushi raiawake, isipokuwa Allaah anamharimishia Pepo." [Al-Bukhaariy na Muslim].

Katika riwaayah nyingine: "Hakuwatizama kwa nasaha zake hatapata harufu ya Pepo." 

Katika riwaayah ya Muslim: "Hakuna Amiri anasimamia mambo ya Waislamu, kisha hakuwafanyia juhudi na hakuwanasihi, Isipokuwa hataingia pamoja nao Peponi." 

 

 

Hadiyth – 3

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول في بيتي هَذَا : ((  اللَّهُمَّ مَنْ وَلِيَ مِنْ أمْرِ أُمَّتِي شَيْئاً فَشَقَّ عَلَيْهِمْ ، فاشْقُقْ عَلَيْهِ ، وَمَنْ وَلِيَ مِنْ أَمْرِ أُمَّتِي شَيْئاً فَرَفَقَ بِهِمْ ، فَارفُقْ بِهِ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema katika nyumba yangu hii: "Ee Rabb wangu! Mwenye kusimamia chochote katika Ummah wangu, akawafanyia uzito. Mfanyie uzito. Na mwenye kusimamia chochote katika Ummah wangu, akawahurumia, Nawe mhurumie." [Muslim].

 

 

Hadiyth – 4

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  كَانَتْ بَنُو إسرَائِيلَ تَسُوسُهُم الأَنبِيَاء ، كُلَّمَا هَلَكَ نَبِيٌّ خَلَفَهُ نَبيٌّ ، وَإنَّهُ لاَ نَبِيَّ بَعْدِي ، وَسَيكُونُ بَعْدِي خُلفَاءُ فَيَكثرُونَ )) ، قالوا : يَا رسول الله ، فَمَا تَأْمُرُنَا ؟ قَالَ : ((  أَوْفُوا بِبَيْعَةِ الأَوَّل فَالأَوَّل ، ثُمَّ أعْطُوهُمْ حَقَّهُمْ ، وَاسْأَلُوا الله الَّذِي لَكُمْ ، فَإنَّ اللهَ سَائِلُهُمْ عَمَّا اسْتَرْعَاهُمْ )) متفقٌ عليه .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Uongozi miongoni mwa Bani Israaiyl ulikuwa ukitekelezwa na Manabiy. Kila anapofariki Nabiy, Nabiy mwengine alikuwa akichukua mahali pake. Na hakika hakuna Nabiy baada yangu na kutakuwa baada yangu Makhalifa ambao watakuwa wengi." Wakasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Unatuamuru tufanye nini?" Akasema: "Kuweni watiifu kwao mmoja baada ya mwengine, kisha wapatieni haki yao na muombeni Allaah kwa mambo yenu. Hakika Allaah atawauliza kwa kile walicho chunga." [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

Hadiyth – 5

وعن عائِذ بن عمرو رضي الله عنه : أَنَّهُ دَخَلَ عَلَى عُبَيْد اللهِ بن زيادٍ ، فَقَالَ    لَهُ : أيْ بُنَيَّ ، إنِّي سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : ((  إنَّ شَرَّ الرِّعَاءِ الحُطَمَةُ )) فإيَاكَ أن تَكُونَ مِنْهُمْ . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaidh bin 'Amru (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba alimtembelea 'Ubaydullaah bin Ziyaad na kumwambia: "Ee mtoto wangu, hakika nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: 'Hakika viongozi wabaya kabisa ni wale wakali (kwa raia zao). Hivyo, kuwa na tahadhari usiwe miongoni mwao." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 6

وعن أَبي مريم الأزدِيِّ رضي الله عنه : أنّه قَالَ لِمعاوية رضي الله عنه : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : ((  مَنْ وَلاَّهُ اللهُ شَيْئاً مِنْ أُمُورِ المُسْلِمِينَ ، فَاحْتَجَبَ دُونَ حَاجَتِهِمْ وَخَلَّتِهِمْ وَفَقْرِهِمْ ، احْتَجَبَ اللهُ دُونَ حَاجَتِهِ وَخَلَّتِهِ وَفَقْرِهِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ )) فجعل معاوية رجلاً عَلَى حوائج النَّاسِ . رواه أَبُو داود والترمذي .

Imepokewa kutoka kwa Abu Maryam Al-Azdiy (Radhwiya Allaahu 'anhu) ya kwamba alimwambia Mu'aawiyah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nilimsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Yeyote ambaye Allaah atamchagua kuwaongoza Waislamu katika mambo yao na akashindwa kutatua shida zao na kuwaondoshea ufakiri wao, Allaah hatamtizama haja zake (wala hatamjibu dua yake) na kumuondoshea hali yake na ufakiri wake Siku ya Qiyaamah." Hivyo, Mu;aawiyah alimchagua mtu kuangalia haja za watu." [Abuu Daawuud na at-Tirmidhiy]

 

 

 

Share