05-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kupendeza Kuzungumza Vizuri na Kuwa na Bashasha Wakati wa Kukutana na Mtu

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب استحباب طيب الكلام وطلاقة الوَجه عند اللقاء

05-Mlango Wa Kupendeza Kuzungumza Vizuri na Kuwa na Bashasha Wakati wa Kukutana na Mtu

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَاخْفِضْ جَنَاحَكَ لِلْمُؤْمِنِينَ﴿٨٨﴾

Na inamisha bawa lako kwa Waumini (kuwahurumia). [Al-Hijr: 88]

 

وَلَوْ كُنتَ فَظًّا غَلِيظَ الْقَلْبِ لَانفَضُّوا مِنْ حَوْلِكَ ۖ  ﴿١٥٩﴾

Na lau ungelikuwa mjeuri mwenye moyo mgumu wangelitawanyika mbali nawe. [Aal-'Imraan: 159]

 

 

Hadiyth – 1

وعن عدي بن حاتمٍ رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( اتَّقُوا النَّارَ وَلَوْ بِشِقِّ تَمْرَةٍ فَمَنْ لَمْ يَجِدْ فَبِكَلِمَةٍ طَيِّبَةٍ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Adiyy bin Haatim (Radhwiya Allaahu 'anhu) Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Jiepusheni au jikingeni na moto japokuwa kwa kutoa kipande cha tende moja." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( وَالكَلِمَةُ الطَّيِّبَةُ صَدَقَةٌ )) متفقٌ عَلَيْهِ

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Na maneno mazuri ni swadaqah." [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

Hadiyth – 3

وعن أَبي ذَرٍّ رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ لي رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( لاَ تَحْقِرَنَّ مِنَ الْمَعْرُوفِ شَيْئاً ، وَلَوْ أنْ تَلْقَى أخَاكَ بوَجْهٍ طَلْقٍ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Dharr (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Msichukie jema lolote hata ikiwa ni kukutana na ndugu yako kwa uso wa tabasamu na bashasha." [Muslim]

 

 

 

Share