A-Majina Ya Swahaba: Maana, Wasifu Wao Kwa Mukhtasari: 'Abbaad Bin Bishr

 

A-Majina Ya Swahaba: Maana, Wasifu Wao Kwa Mukhtasari

 

Alhidaaya.com

 

‘Abbaad Bin Bishr  (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ)

 

 

 

 

Jina Lake:  ‘Abbaad Bin Bishr

 

(Al-Answaariyy)

عبّاد بن بشر

 

 

Maana Yake: Mwenye kumwabudu Allaah (عَزَّ وَجَلَّ) mno.

 

 

Wasifu Wake:

 

 

‘Abbaad bin Bishr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) akijulikana kwa taqwa yake na ‘ibaadah zake, elimu yake na ushujaa vitani.  

 

 

’Abbaad bin Bishr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) alipofika umri wa miaka kumi na nane kwa mara ya kwanza alipomsikia Musw’ab bin Umayr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) akisoma Qur-aan alisisimkwa sana. Qur-aan ilikua na sehemu maalumu katika moyo wa ‘Abbaad.

 

 

Alikua mashuhuri sana kwa usomaji wa Qur-aan mpaka ikampelekea kutambulika na Swahaba wengineo (رَضِيَ الْلَّهُ عَنْهُمْ) kwani alijulikana kama ni rafiki wa Qur-aan.

 

‘Aaishah (رَضِيَ الْلَّهُ عَنْهَا) kuna wakati alisema “Kuna watu watatu miongoni mwa ma Answaar hakuna ambaye atawazidi kwa ubora wa fadhila kama Sa’ad bin Mu’aadh Usayd ibn Khudayr na ‘Abbaad bin Bishr.

 

 

Kufariki Kwake:

 

 

 

 

 

 

 

 

Share