12-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Kitabu Cha Ndoa: Haki Za Kutendeana Kati Ya Mke Na Mume: (ii) Haki Zinazompasa Mume Kumtendea Mkewe: Ayafumbie Macho Baadhi Ya Makosa Ya Mkewe Madhali Si Yenye Kukiuka Maagizo Ya Allaah

 

Swahiyh Fiqh As-Sunnah

 

كِتَابُ الزَّوَاجِ

 

Kitabu Cha Ndoa

 

الحُقُوْقُ بَيْنَ الزَّوْجَيْنِ

 

Haki Za Kutendeana Kati Ya Mke Na Mume

 

 

Alhidaaya.com

 

 

 

11:  Haki Zinazompasa Mume Kumtendea Mkewe: 8-Ayafumbie Macho Baadhi Ya Makosa Ya Mkewe Madhali Si Yenye Kukiuka Maagizo Ya Allaah:

 

 

Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ametuongoza katika hili akituambia:

 

"لَا يَفْرَكْ مُؤْمِنٌ مُؤْمِنَةً إِنْ كَرِهَ مِنْهَا خُلُقًا رَضِيَ مِنْهَا آخَرَ"

 

“Muumini wa kiume (mume) asimbughudhikie Muumini mwanamke (mkewe).  Kama atachukizwa na baadhi ya tabia zake, basi zingine zitamfurahisha”.  [Swahiyh Muslim (1469)]

 

 

Share