14-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Kitabu Cha Ndoa: Haki Za Kutendeana Kati Ya Mke Na Mume: (ii) Haki Zinazompasa Mume Kumtendea Mkewe: Asimsuse Na Ikibidi Basi Yaishilie Ndani Ya Nyumba Tu

 

 

Swahiyh Fiqh As-Sunnah

 

كِتَابُ الزَّوَاجِ

 

Kitabu Cha Ndoa

 

الحُقُوْقُ بَيْنَ الزَّوْجَيْنِ

 

Haki Za Kutendeana Kati Ya Mke Na Mume

 

 

Alhidaaya.com

 

 

13:  Haki Zinazompasa Mume Kumtendea Mkewe:  10-Asimsuse Na Ikibidi Basi Yaishilie Ndani Ya Nyumba Tu:

 

Ni kama ilivyoeleza Hadiyth iliyotangulia nyuma:

 

"وَلَا تَضْرِبِ اَلْوَجْهَ، وَلَا تُقَبِّحْ، ولا تَهْجُرْ إِلا في البَيْتِ"

 

“Wala usipige uso, wala usimkashifu (kumwambia) ni mbaya, wala usimhame isipokuwa ndani ya nyumba tu”.  [Hadiyth Hasan.  Imechakatwa na Abu Daawuwd (2142), Ibn Maajah (1850), Ahmad (4/447) na An-Nasaaiy katika (Al-‘Ishrah) (269)]

 

Lakini kama kuna maslaha ya kisharia ya kumhama na kumsusa nje ya nyumba, basi atafanya hivyo kama alivyowahama Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wakeze nje ya nyumba zao kwa muda wa mwezi mzima.

 

 

Share