10-Al-Lajnah Ad-Daaimah: Zakaatul-Fitwr Ni Fardhi Kwa Masikini Pamoja Na Familia Yake?

Zakaatul-Fitwr Ni Fardhi Kwa Masikini Pamoja Na Familia Yake?

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Mtu masikini mwenye majukumu ya familia yake ambayo ni miongoni mwa mama, baba na watoto. 'Iydul-Fitwr inawadia naye ana swaa’ (pishi moja)  tu ya chakula. Amlipie nani? 

 

 

JIBU:

 

AlhamduliLLaah

 

Ikiwa hali ya masikini huyu ni kama ilivyoelezewa katika Swali, hivyo alipe swaa’ (pishi – kilo 1 ½ - 3) ya chakula kwa ajili yake kwani ni ziada ya mahitajio yake na mahitajio ya wale ambao ni wajibu wake kuwahudumia mchana na usiku wa 'Iyd, kwa sababu Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kasema: ((Anza kwa nafsi yako kisha kwa wanaokutegemea)) [Al-Bukhaariy 2/117, 6/190, Muslim 2.717, 718, 721, 1034, 1036, 1042]

 

Kuhusu wanaomtegemea ikiwa hawana chochote cha kujitolea katika Zakaah kwa nafsi zao wenyewe, basi hawakuwajibika kulipa kwa sababu Allaah Anasema: 

((Allaah Haikalifishi nafsi yoyote ila kwa kadiri ya iwezavyo)) [2: 286]

 

Na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakuna sadaka isipokuwa kwa yule mwenye uwezo)) [Al-Bukhaariy 2/117, 6/190, Muslim 2/717 Namba 1034. Naye (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Ninapokuamrisheni kufanya jambo, basi fanyeni kadiri muwezavyo))

 

Wa biLLaahi at-tawfiyq wa Swalla Allaahu ‘alaa Nabiyyina Muhammad wa aalihi wa Swahbihi wa sallam.

 

 

[Fataawaa Al-Lajnah Ad-Daaimah]

 

 

Share