22-Al-Lajnah Ad-Daaimah: Mume Na Mke Wamekhasimiana Je, Amlipie Mkewe Zakaatul-Fitwr?

 

Mume Na Mke Wamekhasimiana, Je Amlipie Mkewe Zakaatul-Fitwr?

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

 

SWALI:

 

Mume aliyekhasimiana na mkewe katika ukhasama mkubwa wa hatari amlipie mkewe Zakaatul-Fitwr?

 

JIBU:

 

 

Mwanamume anawajibika kujilipia Zakaatul-Fitwr pamoja na watu wote walio chini ya majukumu yake kuwahudumia akijumlishwa na mke kwa sababu amewajibika kumhudumia. Ikiwa kuna ukhasama mkubwa baina yao, hii inajulikana kama nushuwz (uasi baina ya mke na mume, kukawa na chuki baina yao na uadui) ambayo ina maana kwamba hana tena wajibu wa kumhudumia. Hivyo hawajibiki kumlipia Zakaatul-Fitwr kwa sababu inahusiana na kuwajibika kwake, na ikiwa hakuwajibika naye (kuwa katika hali hiyo ya nushuwz) basi hayuko tena katika kuwajibika kumlipia Zakaatul-Fitwr.

 

Wa biLLaahi At-Tawfiyq wa Swalla Allaahu ‘alaa Nabiyyina Muhammad wa aalihi wa Swahbihi wa sallam.

 

[Fataawaa Al-Lajnah Ad-Daaimah (9/367)]

 

 

 

Share