Kujishika Sehemu Za Siri Na Kutazama Vitendo Vya Zinaa Ukapatwa Na Matamanio, Kunatengua Wudhuu?

 

Kujishika Sehemu Za Siri Na Kutazama Vitendo Vya Zinaa Ukapatwa Na Matamanio, Kunatengua Wudhuu? 

 

Alhidaaya.com

 

 

Swali: 

 

Swali langu linausu  twahara, nauliza kuwa mwanamke kujishika katika nafasi zake za siri simaanishi ndani ni hapa juu utakua umetenguka udhu? lingine kama umeona kwenye tv watu wana fanya kitende chandoa  ao kupatwa na matamanivu utakua umezini ? ao hunaudhu?

 

 

Jibu:

 

AlhamduliLLaah - Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salamu zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

Tanbihi: Muulizaji hakutubainishia wazi wazi katika kushika uchi huko alikokutaja.

 

Kushika sehemu zako za siri kwa matamanio au bila matamanio kuna ikhtilaaf baina ya wanachuoni kutokana na ufahamu wao wa Hadiyth mbalimbali za kukataza na kuruhusu suala hilo. Tunakuwekea hapa dalili hizo na kauli mbalimbali za wanachuoni na hoja zao. Ingawa kauli yenye nguvu zaidi ni kuwa ukishika utupu wako kwa matamanio basi wudhuu utakuwa umevunjika, ama bila matamanio ukajishika kama wakati wa kuoga, kuvaa au vinginevyo basi hakutengui wudhuu na Allaah Ndiye Mjuzi zaidi.

 

 

Yanayotengua Wudhuu

 

Katika sehemu ya pili ya swali lako ni kuwa ni madhambi kwa Muislamu mwanamme au mwanamke kukaa kwenye runinga (TV) na kuanza kuangalia vipindi vya ngono. Allaah (Subhaanahu wa Ta‘aalaa) Ametukataza hilo pale aliposema:

وَلَا تَقْرَبُوا الزِّنَىٰ ۖ إِنَّهُ كَانَ فَاحِشَةً وَسَاءَ سَبِيلًا ﴿٣٢﴾

Na wala msiikaribie zinaa. Hakika huo ni uchafu na njia mbaya kabisa. [Al-Israa: 32].

 

Jambo lolote ambalo litakukaribisha na zinaa pia ni zinaa mbali na kuwa madhambi yake ni madogo kuliko kitendo chenyewe. Unapokaa mbele ya TV na kuanza kuangalia vipindi au Video/Dvd/Vcd visivyo na adabu utakuwa una makosa. Ni makosa kwa Muislamu kutazama uchi wa mwenziwe akiwa ni wa jinsiya moja au tofauti. Uchi ulioruhusiwa kutazama ni mume kumtazama mkewe na kinyume chake.

 

Inatakiwa tujiepushe na mambo ambayo yanaweza kutupeleka karibu na zinaa yenyewe kama hivyo unavyofanya. Bila kuwa ni matamanio si kuzini lakini ikiwa utatazama TV yenye uchafu huo na ukapata matamanio utaandikiwa madhambi. Ukiwa utapata matamanio pekee hilo halivunji wudhuu lakini katika kutazama filamu hizo ukapatwa na matamanio na kutokwa na madhii itabidi uoshe tupu yako kisha uchukue wudhuu kwani utakuwa umevunjika. Ama ukashikwa na matamanio kisha ukatokwa na manii itabidi uoge josho la janaba.

 

 

Na Allaah Anajua zaidi

Share